Ndoto ni matokeo ya ubongo kupumzika, hazina maana yeyote zipuuzeni

Ndoto ni matokeo ya ubongo kupumzika, hazina maana yeyote zipuuzeni

Ahsante kwa maswali mazuri

Kwanza kabisa ili uote kitu lazima kuwepo na kumbu kumbu za taarifa mbali mbali kwenye ubongo wako ( short term and long term memmory).
Hizi kumbu kumbu huhifadhiwa kwenye ubongo wa kati na ubongo wa mbele,

Taarifa zinazopakiwa kwenye ubongo hukusanywa kwa njia kuu 5
  • kuona
  • kusikia
  • Kunusa
  • Kuonja
  • Na kuhisi kwa ngozi au mitetemo
HIvyo basi mtu aliyezaliwa akiwa kipofu atapakia taarifa kwenye ubongo kwa njia nne tu, ambazo ni kusikia, kunusa, kuonja na kuhisi (mfano kumtambua mtu kwa kumshika, kutambua sehemu au njia inayoelekea chumbani kwa kugusa na fimbo n.k)

Ndoto zake zitakuwa ni za kuota anaambiwa jambo flani, kuota anatembea kwa fimbo kakutana na kitu flani, kuota amekunywa kinywaji flani kizuri, kuota amewasikia watu flani wakiongea jambo flani au kuota jambo lolote la hatari kama vile kudondoma, kuungua, ajari n.k isipokuwa taarifa zinazohusisha kuona tu ndio hataota

Kwenye ubongo kuna sehemu inayohusika na kuiga kwa mtindo wa kioo, yaani ukimuoma mtu flani anafanya jambo flani na wewe unajikuta umeiga au kufanya kama lilivyo mfano mtu akipiga miayo na wewe unaweza ukajikuta tu unapiga miayo automatic,

Hivyo hivyo kwa mzazi akitabasamu mbele ya mtoto basi na mtoto anatabasamu automatic kwa hiyo anakuwa amejifunza kwa mtindo huo wa kioo.

Sijui unanielewa mkuu??
Nimekuelewa mkuu asante kwa ufafanuzi
 
Ndoto ni matokeo ya ubongo kupumzika usizitilie maanani zitakuchanganya na kukujengea imani potofu
Hapo unazungumzia hali ya mtu ambaye amesikia usingizi au amechoka na kuamua kujipumzikia kwa maana ya kulala na ndiyo ikatokea kuota ambapo ndio unasema ni matokeo ya ubongo kupumzika, upo sahihi kwa kiasi fulani lakini tukizungumzia kuhusu ndoto unajua kwamba inawezekana kutarajia kuota kuhusu jambo fulani kabla ya kulala?(ubongo kupumzika) yani mtu anataka kujua kuhusu jambo fulani mfano kujua kitu kilichopotea au kujua ukweli wa jambo fulani basi hutumia hiyo hali ya kulala huku akitarajia apate ndoto ambayo itahusu hilo jambo ambalo yeye anataka kulijua.

Je ushawahi kusikia vitu kama hivyo?
 
Upon sawia kabisa ndoto siyo lolote wala chochote . Ndoto ni mkusanyiko wa mambo ambayo unakuwa ukiyawazia na kuyafikiria wakati ukiwa ktkshughuli za kila siku. Hivyo unapolala ubongo unapopumzika unaanza kuota ndoto ambazo chimbuko lake ni mawazo ya siku kabla ya kulala. Hayo ni mawazo yangu tu.
Mimi mara nyingi naweza nikawa naota mkojo umenibana sana hali ya kuwa kiuhalisia ni kweli mkojo umenibana, nikishtuka naona kweli mkojo umenibana. Sasa hapo mkuu utasema yalikuwa mawazo yangu kabla ya kulala kwamba nilikuwa nawaza kukojoa au nilikuwa nazungumzia issue za kukojoa?

Sisemi kuota kwangu huko kukojoa kuna maana.
 
Probability of events yaani ni sawa na kubet
Hapo unazungumzia mfano mtu kuota jirani kuna msiba na kweli kukatokea msiba au kaota ugomvi na kweli ukatokea ugomvi, hiyo ndio unaita ni probability kwamba ni sawa na kubet?
 
Hapo unazungumzia hali ya mtu ambaye amesikia usingizini au amechoka na kuamua kujipumzikia kwa maana ya kulala na ndiyo ikatokea kuota ambapo ndio unaita ni matokeo ya ubongo kupumzika, upo sahihi kwa kiasi fulani lakini tukizungumzia kuhusu ndoto unajua kwamba inawezekana kutarajia kuota kihusu jambo fulani kabla ya kulala?(ubongo kupumzika) yani mtu anataka kujua kuhusu jambo fulani mfano kujua kitu kilichopotea au kujua ukweli wa jambo fulani basi hutumia hiyo hali ya kulala huku akitarajia apate ndoto ambayo itahusu hilo jambo ambalo yeye anataka kulijua.

Je ushawahi kusikia vitu kama hivyo?
Ukishajua aina za usingizi hilo swali lako utakuwa umelipatia jibu

Nakupa assignment google usome aina za usingizi
 
Ukishajua aina za usingizi hilo swali lako utakuwa umelipatia jibu

Nakupa assignment google usome aina za usingizi
Kwanini nikagoogle tena wakati wewe umeleta humu hii mada ya ndoto na ndio tunajadili na si kwamba sikuwa najua kuhusu google.
 
Kwanini nikagoogle tena wakati wewe umeleta humu hii mada ya ndoto na ndio tunajadili na si kwamba sikuwa najua kuhusu google.

the-four-stages-of-sleep-2795920_FINAL-5c05c2fc46e0fb00018dac3d.png

Pitia hiyo
 
Sasa hapo jibu la swali nilichokuuliza ndio lipi hapo? hebu nisaidie basi ili niweze kukuelewa.
Ipo hivi kuna aina mbili za usingizi
Usingizi usioambatana na macho kucheza
Usingizi unaoambatana na macho kucheza

Huu usioambatana macho kucheza upo wa aina tatu,

Wewe swali lako limejikita kwenye usingizi unaoMbatana na macho kucheza ambao mtu huupata hatua za mwisho labla hajaamka completely
 
Ipo hivi kuna aina mbili za usingizi
Usingizi usioambatana na macho kucheza
Usingizi unaoambatana na macho kucheza

Huu usioambatana macho kucheza upo wa aina tatu,

Wewe swali lako limejikita kwenye usingizi unaoMbatana na macho kucheza ambao mtu huupata hatua za mwisho labla hajaamka completely
Kwahiyo huo usingizi wa macho kucheza ndio unahusika na issue ya mtu kutarajia kuota kuhusu jambo fulani kabla hata hajalala wala kusinzia?
 
Kwahiyo huo usingizi wa macho kucheza ndio unahusika na issue ya mtu kutarajia kuota kuhusu jambo fulani kabla hata hajalala wala kusinzia?
Mkuu nitakujibu vizuri nikitulia leo sijisikii vizuri
 
Upon sawia kabisa ndoto siyo lolote wala chochote . Ndoto ni mkusanyiko wa mambo ambayo unakuwa ukiyawazia na kuyafikiria wakati ukiwa ktkshughuli za kila siku. Hivyo unapolala ubongo unapopumzika unaanza kuota ndoto ambazo chimbuko lake ni mawazo ya siku kabla ya kulala. Hayo ni mawazo yangu tu.
unaweza kuota kitu ambacho hujawahi kuwaza hata siku moja.
 
Kwahiyo huo usingizi wa macho kucheza ndio unahusika na issue ya mtu kutarajia kuota kuhusu jambo fulani kabla hata hajalala wala kusinzia?
Ipo hivi,

Ili uote ni lazima hicho kitu kiwe kwenye kumbu kumbu kwenye ubongo wako, unapowaza jambo flani sana meams kumbu kumbu zinakuwa stronng

Ndoto huwa inauwezo wa kufanya extension of memories (ideas) kupitia arts

Yaani mfano unaweza kuota umemuona tembo mwenye mabawa maana yake ni kwamba kuna extension ya idea imefanyika kwa tembo, umekopa idea ya ndege ukachukua mabawa ukayapachika kwa tembo,

Hivo hivo kwenye kitu ulichokuwa unakifikiria kinaweza kufanyiwa extension ukiwa usingizini
 
Tuondolee upumbavu wako hapa. Sijui unaishi dunia gani ambayo hujawahi kusikia kuna watu wanaota na walichokiota kinatokea. Acha ubishi wa kipumbavu.
hakuna kitu kama hicho,hiyo ni probality tu,sawasawa wewe uote utaoga halafu uje uoge kweli,au mimi niote siku nitapata ajali halafu nipate kweli kumbe ni ajali tu hata nisingeota ingetokea
 
Ni mjinga na mpumbv ndye atasikiliz takataka za mtoa mada kitu kama hukijui uliza upewe elimu sio kupinga, icho kijielemu chako usijione basi umemaliza kila kitu hapa dunian, ndoto ni jambo pana ambalo huwez lizungumza kwa kubase upande mmja, maana linaweza chambuliwa, kisayansi na kiimani, kama sayans inaamini kuna time travel basi ujue kuwa hata imani inaproof uwepo wa maono na ndoto za kwel ambazo mtu huona matukio ya wakat ujao, uliopo ama uliopita akiwa ktk wakat uliopo, hili jambo kisayans linawezekana, kiimani ni zaid ya hivyo,

tatzo la utandawazi watu wa kileo mnajifanya kupuuza mambo ya msingi ndiomaana mnabaki ktk utumwa wa akili sabb ya kukataa nature ya maisha ya kweli...Funguka kijana wenzako tunaheshimu ndoto na kuzijali maana hapo ndpo yalpo maisha yako na ya jamii yako..hakuna ndoto isiyo na maana kwakuwa zote zina ashiria jambo fulan na zmetokea kwa sbbu fulan, kama huna macho ama nguvu yakufunua maana za ndoto, bas usitegemee kuja kujua umuhimu wake,,endelea kuwa litumwa la utandawazi
 
Ipo hivi,

Ili uote ni lazima hicho kitu kiwe kwenye kumbu kumbu kwenye ubongo wako, unapowaza jambo flani sana meams kumbu kumbu zinakuwa stronng

Ndoto huwa inauwezo wa kufanya extension of memories (ideas) kupitia arts

Yaani mfano unaweza kuota umemuona tembo mwenye mabawa maana yake ni kwamba kuna extension ya idea imefanyika kwa tembo, umekopa idea ya ndege ukachukua mabawa ukayapachika kwa tembo,

Hivo hivo kwenye kitu ulichokuwa unakifikiria kinaweza kufanyiwa extension ukiwa usingizini
Sasa mimi nazungumzia mtu kutaka kujua jambo ambalo halifahamu na hivyo hutumia ndoto kama njia ya kuweza kulijua hilo jambo, nimetoa mfano kama mtu anataka kujua kilipo kitu kilichopotea au kutaka kujua jambo ambalo halifahamu.

Kwahiyo ni tofauti na hali ya kufikiria tu jambo na kuja kuliota bali nazungumzia hali ya kutumia ndoto kama njia ya kupata kujua jambo fulani na hivyo analala huku akiwa anataraji kuota aina fulani ya ndoto.
 
Sasa mimi nazungumzia mtu kutaka kujua jambo ambalo halifahamu na hivyo hutumia ndoto kama njia ya kuweza kulijua hilo jambo, nimetoa mfano kama mtu anataka kujua kilipo kitu kilichopotea au kutaka kujua jambo ambalo halifahamu.

Kwahiyo ni tofauti na hali ya kufikiria tu jambo na kuja kuliota bali nazungumzia hali ya kutumia ndoto kama njia ya kupata kujua jambo fulani na hivyo analala huku akiwa anataraji kuota aina fulani ya ndoto.
Unazungumzia mambo ya Memory
 
Back
Top Bottom