Ndoto tunazoota na tafsiri zake

Ndoto tunazoota na tafsiri zake

Usiku wa kuamkia leo nimeota ndoto ambayo siyo nzuri sana na imenitisha sana.

Nimeota nimekufa niko ndani ya jeneza kwenda kuzikwa na watu wanalia sana. Ghafla nikashtuka toka usingizini. Nikajaribu kuinua kichwa kikawa kizito baada ya muda kichwa kikaniuma sana.

Naomba unipe tafsiri ya hii ndoto maana imeninyima raha kabisa.

Nawasilisha.
 
Mkuu nibwakati gani ndoto huja?
Usiku tuuu au hata Mchana?
Sababu Kama ni Kulala unawwzakuta Umetoka Kazini Kukesha Usiku ukaridi nyumbani Asubuhi kulala na Ukaota,
Au Kama ni Weekend umepumzika na Ukaota!
Sasa Ndoto huja wakati gani?
Wengine husema haaaaa hiyo ndoto itakuwa ni ya mchana!!!
Ina Maana Ndoto ya Mchana ina mushkeli...
Muda wowote inakuja.
 
Je hii ndoto yangu inamaana gani
Niliwahi kuota napita kwenye kundi la mbwa wakali waliokuwa wamelala alfu wakashtuka na kuanza kunimbwekea na kunikmbiza theni nikashtuka nikiwa na hofu

Na hii ya pili
Nikiwa usingizini nikiota nipo juu angani mara nmeanguka toka juu na kushuka kwa kasi huku nikipiga makelele na kushtuka nikiwa kitandani
 
Habari za muda huu wana JF.

Niende moja kwa moja kwenye mada, ndoto ni jambo la kawaida kwa mwanadamu yoyote, lakini si kila ndoto ni yakupuuza (Ninavyoamini mimi).

Usiku huu, kuna ndoto nimeota, ila nahisi ni kama maono fulani, maana nimepewa location halisi na majina ya watu halisi (Maarufu nisio kuwa nawafahamu) ila baada ya kuamka nikaserch kwenye mtandao, hao watu wapo...na shughuli zao ni hizo hizo kama nilivyoota.

Tafadhali, hii kitu sio ya kupuuza, kuna kundi kubwa la watu linapotea katika eneo hilo kwa sababu ya kafara inayofanywa na mtu mmoja kwa makosa yake aliyoyoyafanya huko nyuma zaidi ya miaka kumi imepita.

Mshana Jr my bro, nahisi huu ni uwanja wako pengine una jambo unaweza nifafanulia, na wengine pia mnakaribishwa.

Kabla sijaeleza story nzima kuhusu hii ndoto, naomba nijue kuhusu hii kafara ina maana (Katika ulimwengu wa roho) gani, na ipo kweli.

Huyo muhusika aliwahi uwa mtu...alidhani ni mtu wa kawaida, ila baada ya kufanya hilo tukio alijiingiza kwenye maagano makubwa sana. Maagizo nayoyatekeleza kila baada ya muda fulani ni kama ifuatavyo[emoji116]

Anaambiwa achongeshe kajeneza kadogo (Kazuri) ni kama toy tu hakafai kuingiza hata binadamu labda fedha na vitu vingine vidogo.

Ndani ya hilo jeneza aweke kitambaa cheupe, halafu ajichange kidoleni ahakikishe tone moja tu limedondoka kwenye hicho kitambaa...na baada ya hapo aweke na vito (Madini/Fedha), dhamani yake isipungue, Milioni moja (1,000,000Tzs).Akisha kamilisha hivyo vitu..usiku wa manane Ana end a kuweka hilo eneo ambalo ni makutano ya barabara,
Wakati huo huo hata dakika haiishi hivyo vitu hutoweka na yeye akishuhudia.

Baada ya hapo, ndio kilichonifanya nije hapa, hutokea ajali za kutisha sana hilo eneo, na haipiti miezi mitatu lazima jamaa afanye hiyo kafara.

Tafadhali naomba kujuzwa maana ninachokishangaa kwa nini niletewe majina ya eneo halisi na sijawahi kufika (Ila lipo kweli) na majina ya wahusika na yapo kweli huyo anaefanya hilo jambo...anatambulika kama mtumishi anajiita (Kuhani...) Naomba kujuzwa nahisi nimeoteshwa kuokoa roho za watu zinazopotea bila hatia.

Wale wa kubeza sioni kama hapa ni sehemu sahihi, ni issue serious inahitaji majibu na utekelezaji wa haraka sana.

Karibuni kwa maoni[emoji120]
 
Nimesabuskraibu kabisa ili nije nisome maoni ya Mshana Junia na wengine wenye utaalamu na mambo haya. Nami kuna wakati huwa naota mandoto haya ya ajabu ajabu ila mimi huwa napambana tu kivyangu; na huwa sijali sana!
 
Nimesabuskraibu kabisa ili nije nisome maoni ya Mshana Junia na wengine wenye utaalamu na mambo haya. Nami kuna wakati huwa naota mandoto haya ya ajabu ajabu ila mimi huwa napambana tu kivyangu; na huwa sijali sana!
Ngoja tusibiri brother aamke akutane na hichi kisanga pengine analo la kutuambia[emoji848]
 
Umekosea kuleta huku unatakiwa uende kwa wataalam ukazuie
 
Ni suala la Kiroho sana mkuu. Wengi hapa si wajuzi wa ndoto. Unaweza pata muda wa kutulia na Mungu ili akauelekeze jinsi ya kuomba? Au la tafuta msaada kutoka kwa kiongozi wa Imani. Anyways kama wapo wenye uelewa watakuja.
 
Ndoto yako ipo straight mbona...

Kuna mtu ambaye wewe umemtaja anajulikana kama kuhani, anafanya ibada ya makafara kwa kutoa sadaka (umeitaja huwekwa kwenye kijeneza)...

Sadaka yoyote ya manuizo huwa inakabidhiwa kwenye mahali paliposimikwa kama madhabahu (si lazima liwe jengo), zipo madhabahu za aina nyingi mathalani njia panda, miti, makaburi, vyooni n.k...

Hivyo akitoa hizo sadaka anazotoa, ni lazima agano la damu lifanyike ili kuisindikiza sadaka aliyotoa na kawaida agano la damu huambatana na kutolewa uhai kwa kiumbe hai kama kuku, mbuzi, ng'ombe na kiumbe kilicho sadaka kubwa zaidi ni mwanadamu...

Nini cha kufanya?

Maadamu umeweka habari hizo hapa basi taja eneo na taja muhusika, inagwaje inaweza isiwe approach nzuri sana lakini maadam imeandikwa usimuache mwanamke mchawi akaishi, maana yake huyo mchawi anakuwa anatambulikana...

Au kama waogopa watafute watu wa makanisani wale wanaofanya maombi ya kitaifa (dizaini ya huduma za kina Mwl Mwakasege)...

Mwisho, ufalme wa giza haujawahi ushinda ufalme wa nuru.
 
Nina ndoto yangu moja tu ambayo huwa ni ya kweli, nikiota then nikapuuzia lazima linikute jambo.

Mara zote nikiota napata hela basi mchongo wowote wa hela nitakaoupata siku za karibuni ni fake.nikiingia kichwa kichwa napoteza.

Usiku mmoja nimelala,yaani vile nimepitiwa tu na usingizi nikaanza kuota nimepata mchongo wa hela ndefu,usiku mzima ndoto inaendelea tu nikishtuka nikilala tena inaendelea ilipoishia.

Asubuhi nimeamka nikaanza kutafakari ni kwanini ile ndoto inisumbue vile usiku?na ni mchongo gani huo.

Mama wee,mida ya saa 5 asubuh kaja mtu wangu wa karibu kabisa kuniletea mchongo wa hela,aisee sikuamini macho yangu kama ni yeye anayetaka kuniingiza mkenge zaidi ya mil.8[emoji29][emoji29][emoji29][emoji29][emoji29][emoji29][emoji29][emoji29][emoji29][emoji29]

Ninachotaka kukwambia mtoa mada hilo ni jambo la kiroho,kama wewe ni muombaji mambo ya kiroho yanamalizwa kiroho ingia kwenye maombi.mbivu na mbichi zitajulikana hukohuko ulimwengu wa roho.
 
Huyo Mshana Jr ni mlozi sasa yeye na mambo ya kilokole wapi na wapi. Mpaka unafikia kuoteshwa hivo huna connection na watumishi wenzio mnaosali wote
 
Taka kwanza eneo husika..

Halafu umesema kila miezi mitatu au kila miaka kumi??
 
Back
Top Bottom