Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Zingegawanywa sema Rais Samia amesema Mara nyingi kugawa maeneo sio kipaombele chake kwa Sasa,Ila Jiwe angekuwepo wangeshgawanya kufuta aibu ya hako kachato angagawa Moro na Tabora.Tuombe Mungu iwe hivyo kwa kweli
Acha uzwazwa ongelea mkoaVipi kuhusu uwanja wa ndege Chato, hospitali ya kanda ya Chato , mbuga ya wanyama chato ,navyo vimeyeyuka ghafla?
Imeeleweka
Utaishi milele ibilisi weweAsante Mungu kwa kutuondolea yule Ibilisi mfitini, mbinafsi, muuaji , fisadi kubwa na lichawi likubwa lililoharibu akili za wananchi wengi ambao mpaka sasa hawawezi kukaa kutwa bila kumtaja
Kuna mpuuzi mmoja mfuasi wa Jiwe alipoziona post zangu alikasirika sana akasema nitakufa soon.Utaishi milele ibilisi wewe
😂🙄😂😂😂Kuna mpuuzi mmoja mfuasi wa Jiwe alipoziona post zangu alikasirika sana akasema nitakufa soon.
Nikamwambia kuwa Mimi sio level yake nikampa timeline kuwa baada ya muda fulani nitaenda pm nimsalimie kama tamkuta hai. Tayari hachangii Uzi wowote na pm hayupo online. Tayari ameshamfuata Jiwe
Ibilisi ni wewe mjukuu wa sheitwanUtaishi milele ibilisi wewe
Magufuli angeendelea kuishi chato ingekuwa makao makuu ya nchi by 2025!Ndoto ya wananchi wa Wilaya ya Chato kuwa Mkoa imegonga mwamba baada ya mikoa jirani ya Kigoma, Kagera na Mwanza kutokuwa tayari kuachia maeneo yake ili kuunda mkoa mpya wa Chato.
Wazo la Wilaya ya Chato kuwa Mkoa liliibuka tangu enzi za utawala wa awamu ya tano ya Hayati Rais John Magufuli, hata hivyo limekuwa likijadiliwa katika ngazi mbalimbali kabla ya leo kukataliwa rasmi.
Akiwa wilayani Chato Oktoba 14, 2021 kwenye kilele cha mbio za Mwenge, Rais Samia Suluhu Hassan alisema Serikali inaangalia vigezo vitakavyo ruhusu Chato kuwa Mkoa.
“Bado Chato haijawa mkoa kuna vigezo kadhaa bado tunaviangalia vigezo hivi vikikidhi basi tunakwenda kulimaliza jaambo hilo,” alisema.
Hata hivyo, Januari 10, 2023 imeelezwa kuwa Chato haina vigezo vya kuwa mkoa.
Hayo yamebainishwa katika Kikao cha Ushauri wa Mkoa (RCC) wa Geita, wakati Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu wa Mkoa wa Geita, Frank Mashauri aliposoma majibu ya barua ya Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) yenye kumbukumbu namba CBD.132/503/01B/26 ya Oktoba 2022.
Akifafanua kuhusu kukwama huko, Mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela amesema nia ya kuanzisha mkoa ilikuwepo na vikao vimefanyika na kupeleka mapendekezo kwenye mamlaka za juu.
Amesema Tamisemi imeandika barua kwenda kwenye mikoa jirani na mikoa hiyo imesema haipo tayari wilaya zake kwenda kuanzisha mkoa mpya wa Chato na kwa maana hiyo maombi ya Geita yamekataliwa.
“Mngeniambia mkoa ni kubwa tugawe inge- make sense (ingeeleweka), lakini mkoa huu haugawiki.
“Wakati mwingine unaweza kuwapa matumaini watu ambayo hayapo, sitaki kuwa muongo kuwapa watu matumaini ambayo hayapo nitakuwa mkuu wa mkoa wa ajabu sana,” amesema Shigela.
Shigela amesema akiwa mkuu wa Mkoa wa Tanga aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, Hayati John Magufuli alipinga masuala ya kugawa maeneo na hakuna mkoa wowote uliopendekeza kugawa maeneo yao na kuwataka viongozi kutojenga matumaini ambayo muda wake haujafika.
Amesema mkoa mwingine mkubwa ni Morogoro wenye halmashauri tisa kata 214 ukiwa na ukubwa wa eneo lenye urefu wa mita za mraba 73.
Awali akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma aliwataka wadau kutumia busara kupatikana kwa mkoa mpya wa Chato kwa kuwa hata kupatikana kwa mkoa mpya wa Geita haikuwa rahisi na kwamba kilichopo sasa ni kupingana wenywewe kwa wenyewe.
“Tusishikane uchawi na tusikatishane tamaa kuwaliza mikoa haitakubali kwakuwa kuna rasilimali lakini kama kweli mkoa upo sisi Geita tumeshatoa mapendelkezo na Tamisemi wasitutege wakiona inapendeza wataugawa,” amesema Msukuma.
Kwa upande wake Mwenyekiti halmashauri ya Mbogwe, Vicent Busigwa amesema mvutano uliopo ni wa viongozi na sio wa wananchi.
Busigwa alisema Tamisemi ishauriwe kuliangalia upya jambo hili ili kupeleka huduma za wanachi karibu.
Naye Mbunge wa Mbogwe, Nicodemas Maganga, amesema, “Mwenyekiti Kanda hii ya Ziwa wananchi wote wanasubiri Chato kutangazwa kuwa mkoa na ukumbuke, Rais akizima mwenge Chato wananchi walikua wakisubiri mkoa kutangazwa jambo hili limekuwa siku nyingi.”
Chanzo: Mwananchi
yule jamaa angejenga hadi IKULU ya nchi kule, hakuwa na mshipa wa woga wala aibu.Magufuli angeendelea kuishi chato ingekuwa makao makuu ya nchi by 2025!
Mengi tu, samaki, dhahabu, misitu na mbuga ya wanyama.Chato ina mapato gani ya kuifanya iwe Mkoa?
Yule ni mbinafsi na gaidi wa kwanza kutokea tanzania. Alihamishia wanyama burigi chato na kujenga uwanja wa ndege katika kijiji chake, mambo ya kishamba kama hospitali ya rufaa, benk kubwa kubwa vitabaki tembo weupe tu.Yaani yule DIKTETA ali- misuse raslimali za nchi kwa kwenda kujenga miundombinu mikubwa kuliko mahitaji halisi ya kitongoji cha Chato, isitoshe kila alichofanya hakikuwa na approval ya Bunge, bado wanataka watushawishi TUBARIKI MAKOSA yake kwa kuipa Chato hadhi ya Mkoa? They are not serious.
Mungu ametuepushia hiyo DHAHMA kwa kuchukua roho ya mtu mwongo, mwizi na katili na mbinafsi ili tujipange vizuri, kama tutaupa Chato hadhi ya mkoa itakuwa ni KUFURU kwa Mungu wetu.
Ile Chato ni ya kubaki hivyo hivyo kama GBADOLITE ya Mobutu, ili vizazi vijavyo vije vitambue kuwa tuliwahi tawaliwa na mtu KICHAA kwa miaka 5 na siku 131
Mimi siyo wa Chato ila tunasema kwamba mikoa mipya yote Tanzania ilianzishwa kisiasa siyo uhalisia. Kwa hiyo Chato imekosa mtetezi tu vinginevyo ingekuwa ni mkoa tu kama ilivyokuwa kwa Njombe na Katavi. Hata hiyo Manyara ilianzishwa kwa ushawishi wa Waziri Mkuu wa wakati ule. Ndio maana wilaya kama Simanjiro kupelekwa Manyara ni uonevu maana iko karibu sana na Arusha. Aidha, jiulize kwanini Sengerema iwe mkoa wa Mwanza badala ya Geita ambayo ilizaa Sengerema mwaka 1975 ? Na zote ziko ng'ambo ya Ziwa.Saizi unaugulia tuu huko [emoji1787][emoji1787]
Mbona hayo hadi sasa hayajafanya pachangamke bado pamelala Zzzzzzzzzz hadi mwendazake akalazimishaMengi tu, samaki, dhahabu, misitu na mbuga ya wanyama.
Siyo kweli Katavi kuna uchumi gani kuizidi Chato na maeneo yaliyopendekezwa ya Ngara, Kakonko, Biharamulo na Chato yenyewe ? Aidha, hiyo Njombe yenye watu wachache zaidi katika mikoa ya Tanzania bara ina nini cha ajabu zaidi ya miti ya mbao ? Uwe serious kidogo unapotoa hoja.Njombe na Katavi Wana Uchumi mkubwa kuliko Mkoa pendekezwa na Sababu za msingi za kugawa zipo ikiwemo ukubwa wa Mikoa husika.
Sasa Kagera,Geita na Kigoma Zina ukubwa gani wa kuhitaji kugawanywa?
Ndio nakukatalia Sasa ,vigezo vya kuanzisha maeneo ni umbali/Ukubwa,nature of terrain,Idadi ya watu na Potential ya eneo kiuchumi/mapato.Mimi siyo wa Chato ila tunasema kwamba mikoa mipya yote Tanzania ilianzishwa kisiasa siyo uhalisia. Kwa hiyo Chato imekosa mtetezi tu vinginevyo ingekuwa ni mkoa tu kama ilivyokuwa kwa Njombe na Katavi. Hata hiyo Manyara ilianzishwa kwa ushawishi wa Waziri Mkuu wa wakati ule. Ndio maana wilaya kama Simanjiro kupelekwa Manyara ni uonevu maana iko karibu sana na Arusha. Aidha, jiulize kwanini Sengerema iwe mkoa wa Mwanza badala ya Geita ambayo ilizaa Sengerema mwaka 1975 ? Na zote ziko ng'ambo ya Ziwa.
Narudia tena uanzishwaji wa mikoa mipya Tanzania ni siasa tu wala hakuna uhalisia.
Njombe ilipendelewa tu we nyau usilete ujinga hapa. Mkoa gani wenye watu laki nane ?Acha uongo wewe kenge,hata ramani tuu ya Mikoa unayoitaja inasomeka vizuri na ilistahili Tena kwa sababu za kimsingi kabisa.