#COVID19 Ndugai: Chanjo ni hiyari ila hauna hiyari kuambukiza wenzako

#COVID19 Ndugai: Chanjo ni hiyari ila hauna hiyari kuambukiza wenzako

Tulishinda corona ndio maana misongamano ilikuwa kila Kona mazishi ya Magufuli Hadi chato serikali nzima hakuna aliyevaa barakoa Wala kuchanja na wazoma Hadi leo wanadunda iingekuweko Corona kwa Hawa vinara wa kuvaa vibarakoa si wangekuwa walikufa siku nyingi kipindi Cha Magufuli

Corona kipindi Cha Magufuli tuliipiga mateke Tanzania kwa maombi na kutumia dawa zetu za asili za kujitukiza na matangawizi yetu.Unanunua shilingi elfu moja mzigo wore corona inaipiga mateke .Bila hiyo michanjo Koko ya wazungu mnayoiabudu
huyo aliekua na misimamo ya kinekitile ngwale aliponza wenzie wakaenda na changamoto ya upumuaji, mwisho wa siku ikammalizia mwenyewe we unaongea ujinga gani?
 
huyo aliekua na misimamo ya kinekitile ngwale aliponza wenzie wakaenda na changamoto ya upumuaji, mwisho wa siku ikammalizia mwenyewe we unaongea ujinga gani?
Hata vilaza wanajiamaini Sana mjini, hajui kilichomuuwa JPM ni Nini?


USSR
 
Wakuu soon tamko la katibu wa bunge kwenda kwa wabunge wote wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania kuwa lazima wachanjwe la sivyo hawataruhusiwa kuingia bungeni mwenzi ujao .

Wabunge watatakiwa kuwasilisha kadi za chanjo kwa walinzi ili kuruhusiwa kuingia bungeni.

Wabunge wanatakiwa kuwa mifano ya jamii na chama Cha mapinduzi na kumuunga mkono mh. Rais ambaye tayari amesha chanjwa.

MY TAKE. Msimamamo wa gwajiboy na poleople utaonekana hasa wakigoma kuingia bungeni

USSR
Serikali imesema ni hiari, hakuna kitu kama hicho. Waliochanjwa wanaogopa nini? Wao si wako salama, wacheni ukuda.
 
Ni busara kwa wabunge wote ,wafanyakazi wa wizara ya afya,wafanyakazi wote wanaofanya kazi katika viwanja vya ndege vya JNIA,KAdCo na Zanzibar kuchanja Chanjo ya uviko-19.Ili Tanzania nayo itokomeza gonjwa hili.Maisha yaendelee
Huko walikochanja wote mbona ndio wanakufa zaidi na huo ugonjwa? Kila uchwao wanaongeza boosters tu!
 
Akifa askari anazaliwa mwanajeshi kumzoofisha gwajima na polepole sio mwisho wa sinema ndio kwanza CCM movie inachanganyia
 
Askofu Rashid na Comrade Polepole
Na hapa ndipo mpasuko unapo enda kutokea.
I'm sure hawa watu wana watu wengi wazito ndani ya chama wanao waunga mkono.
Sooner panaenda kutokea ombwe la uongozi nchini.
 
Askofu rashidi achague moja, achanje aingie bungeni apate posho au asichanje abaki kwenye godown lake aendelee kufufua misukule.
Askofu Rashid na Polepole tayari kunajambo wameling'amua. Na hawa lazima wana invisible hugely backup. Na kuna Jambo kubwa linaenda kutokea hapa nchini ambalo litapelekea ombwe la uongozi.
 
Wakuu soon tamko la katibu wa bunge kwenda kwa wabunge wote wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania kuwa lazima wachanjwe la sivyo hawataruhusiwa kuingia bungeni mwenzi ujao .

Wabunge watatakiwa kuwasilisha kadi za chanjo kwa walinzi ili kuruhusiwa kuingia bungeni.

Wabunge wanatakiwa kuwa mifano ya jamii na chama Cha mapinduzi na kumuunga mkono mh. Rais ambaye tayari amesha chanjwa.

MY TAKE. Msimamamo wa gwajiboy na poleople utaonekana hasa wakigoma kuingia bungeni

USSR
R.I.P Magufuli.
 
Mtego mkali!!itakuja kwa watumishi wa Umma!!
Watumishi wa umma ndiyo rahisi sana kuwapata Hahaha! HR anaagizwa tu ili uwekwe kwenye mkeka wa mshahara lazima uoneshe kwanza cheti cha chanjo, full stop!! Hapo waumini wa Gwajima watakimbizana mahospitalini kuchanja, and by that time chanjo zimeisha, kuna watu watapigwa na njaa street miezi sita kusubiri chanjo zije awamu ya pili
 
Na hapa ndipo mpasuko unapo enda kutokea.
I'm sure hawa watu wana watu wengi wazito ndani ya chama wanao waunga mkono.
Sooner panaenda kutokea ombwe la uongozi nchini.
Acha ramli! Mlianza oh deep state haitaki Samia apewe urais, mkaja na slogan kuwa sukuma gang watapiga kura za hapana uenyekiti wa CCM ili kutenganisha Uenyekiti na Urais!!! Now mnakuja na ramli nyingine tena, kuna faida gani kila siku kutunga uongo na unafail?
 
Wakati kukiwa na mjadala wa baadhi ya wabunge kuhusu chanjo ya corona inayoendelea kutolewa nchini, Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema pamoja na chanjo kuwa hiari, haimfanyi mtu kuwa na hiari ya kuambukiza wengine.

Kauli hiyo imekuja kukiwa tayari kuna wabunge walioonyesha wazi kupingana na mpango huo wa chanjo wakieleza kuhofia usalama wake kwa afya ya anayechanjwa.

Hata hivyo, juzi katika mahojiano yake na BBC, Rais Samia Suluhu Hassan aliendelea kuwahakikishia Watanzania kuwa chanjo hiyo ni salama, kinyume na hapo yeye asingehatarisha maisha yake kwa kuwa wa kwanza kuchanjwa

“Nashukuru sasa hivi Watanzania wengi wameelewa na wanaulizia chanjo, nalazimika kutuma maombi kwa nchi wahisani wanaosaidia chanjo waiangalie Tanzania wakati na sisi tukiendelea na mpango wa kununua chanjo kupitia nchi za Umoja wa Afrika (AU),” alisema Rais.

Pamoja na kauli hiyo ya Samia na uthibitisho wa wataalamu wa nchini na kimataifa, baadhi ya watu, wakiwemo wabunge kadhaa, wanaeleza waziwazi wasiwasi wao dhidi ya chanjo hiyo.

Akinukuliwa na kituo kimoja cha runinga, Spika Ndugai ambaye amekwishachanja, alisema, “tuna mabanda tayari yameshajengwa, wapo wataalamu na chanjo za kutosha zipo, kwa hiyo kila atakayekuja kwenye Bunge lijalo…(hakumalizia).

Aliongeza, “Ni hiari. “Ni hiari” alisema huku akionyesha ishara ya alama za funga usemi kwa vidole.

Kisha, Ndugai akasema, “...lakini hiari hii haikufanyi uwe na hiari ya kuchukua risk ya kuambukiza wengine.”

Mwananchi lilimtafuta Spika Ndugai jana ili aeleze alichokuwa anamaanisha, ambapo alifafanua zaidi kuwa vikao vya Bunge lijalo litakaloketi Agosti 30, ofisi yake itatoa mwelekeo huku akiwasisitiza wabunge wote kuchanja.

“Kuanzia Jumatatu (Agosti 16), wabunge wote watakuwepo (Dodoma) na uchanjaji utakuwa mkubwa. Tunaanza kwa kuhakikisha huduma zinakuwepo maana hata ukisema unachukua hatua, lazima huduma zipatikane, wenyewe ndiyo washindwe kwenda kuzipata. Natoa wito kwa wabunge wote kuchanja,” alisema Ndugai.

Miongoni mwa wabunge walioonyesha msimamo dhidi ya chanjo hiyo ni pamoja na aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, ambaye kwa sasa ni mbunge wa Kuteuliwa, Humprey Polepole.

“Ni muhimu sana watu wetu wakumbushwe tena na tena namna ya kujenga kinga ya mwili, ikiwemo elimu ya chakula na lishe bora kama hatua ya msingi ya kukabiliana na magonjwa na maambukizo yanayoweza kuzuiwa na kinga imara ya mwili. Kuchanja ni hiari lakini si kila kitu, mimi nitaimarisha kinga ya mwili na chanjo kwangu hapana,” aliandika Polepole kwenye ukurasa wake wa Instagram na kupongezwa na baadhi wafuasi wake, huku wengine wakimshukia.

Naye mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima mara kadhaa ametamka hadharani kuwa hatachanjwa chanjo hiyo kwa kuwa hana uhakika na usalama wake.

“Chanjo ni hiari anayependa aende, ila hapa hachanjwi mtu, lazima kondoo wangu niwalinde kwa namna yoyote ile, siko tayari kondoo wangu hata mmoja aangamie. Wajibu wa kulinda afya yako ni wako, huwezi kuwekewa kitu mwilini bila kutaka. Sichanjwi na sitachanjwa,” alisema Gwajima, ambaye ni askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima.

Mbunge huyo, kinyume na kauli za kitaalamu, alisisitiza kuwa hadi sasa hakuna tafiti za kutosha zilizofanywa na wataalamu wa ndani kuhusu chanjo hiyo inayotolewa nchini na kuwataka wataalamu kuweka wazi kemikali zilizomo kwenye chanjo hiyo.

Matamshi hayo yamemwibua Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Shaka Hamdu Shaka akisema msimamo wa chama hicho unaweka wazi kuwa chanjo ni sehemu ya utekelezaji wa ilani yao kwenye kipengele cha utoaji wa huduma za afya kwa Watanzania.

“Kwa hiyo sisi ukituuliza CCM msimamo wetu, tunasimama na Rais kwamba lazima tuwakinge Watanzania dhidi ya maradhi ya mlipuko, ikiwemo Uviko-19... tuna kanuni ya maadili, hii inawamulika viongozi wote ambao mienendo yao haiendi vizuri, ikionekana kuna mtu amekiuka kanuni, misingi ya chama ipo na haibagui, hatua zinaweza kuchukuliwa kwa yeyote,” alisema Shaka.
Huu ndio msimamo wa Dunia,hata Tzn ni hivyo.. kanakwamba haitoshi nilimsikia RPC wa Arusha akisema hivyo pia.

Kwamba kuvaa barakoa ni lazima na tahadhari nyingine kwa sababu kinyume chake unakiuka sheria ya adhabu insuohusu kuambukiza na kueneza magonjwa lazima.Alitaja vifungu vya kutosha na adhabu zake.

Ni hivi chanjo ni lazima ila ni lugha tuu inatumika kwa sababu wanaopinga hawana sababu za msingi na waliochanja hakuna shida imewapata.
 
Askofu Rashid na Polepole tayari kunajambo wameling'amua. Na hawa lazima wana invisible hugely backup. Na kuna Jambo kubwa linaenda kutokea hapa nchini ambalo litapelekea ombwe la uongozi.
Hata Kama Wana back up wanapaswa kujifunza kwa Edward Lowassa pia Fred Mpendazoe.Kwenye siasa usikubali kutangulizwa mbele eti tupo nyuma yako.Ukigeuka utajikuta mwenyewe
 
Na ikiletwa hoja kwamba wachungaji na wahubiri wote lazima wachanjwe ili kuendelea kutoa huduma, atatokea wapi?
Kuna vitu Ni rahisi kufanyika Rwanda alikoenda kutembelea kuliko Tanzania !!! Watanzania sio wapole Kama wanavyodhaniwa Ni wakinywa.Mkimya na mpole Ni watu tofauti .Mpole Ni wa kuzaliwa mkinywa anakulia Timing ukiingia anga zake anga zake ayakachokufanyia hutaamini . Watanzania Ni wakinywa unasema mabasi yote level sit wanakugomea kimya kimya Kuna mahali wanakusibiri walipuke ukijitia mjuaji

Level ya Sasa ya obedience kwenye measures za Corona ijo jui to kwa viongozi wa serikali na wafanyakazi wake. Mitaani watu hawataki .Kuna bomu litalipuka serikali ikijitia kutumia ubabe Hii tafsiri ya viongozi kuwa ndio obedient na wananchi hawataki ina Mambo Mengi Ukienda kwenye dini kubwa Kama katoliki Hali Ni hiyo hiyo barakoa anavaa padri na askofu tu waumini hawataki Misikitini hivyo hivyo..


Mama Samia anatengeneza bomu haya Mambo hayataki papara na kuiga tu Nchi zingine kwa kisingizio ohh Tanzania Sio kisiwa .Kuna Mambo Tanzania Ni kisiwa .
 
Noma Sana hata misikitini na kanisani .bila chanjo huuingii kuswali


USSR
Viongozi wa dini watakuja juu sadaka watapata wapi? Naona wewe lengo lako ninkuchonganisha serikali na viongozi wa dini.Mama Samia Akifika huko atajjijua mwenyewe.

Kwenye dini Ni eneo nyeti hasa kwa watanzania
 
Noma Sana hata misikitini na kanisani .maca bila chanjo huuingii kuswali


USSR
Hilo chanjo Ni shetani pepo la kuzimu limekuja kuleta Vita Tanzania

Baada ya kuona Tanzania imekuwa Nchi ya amani na utulivu kwa miaka nenda Rudi wazungu wameona watumie chanjo Kama njia ya kuligawa taifa la Tanzania na kuchochea Vita na Mama Samia kaingia kichwa kichwa.Ila Mungu yupo hii agenda haitafanikiwa waambieni wazungu wenu kabisa

Tanzania Sio ulaya Wala marekani wala Rwanda ndio maana tunaitwa Tanzania hatuitwi Ulaya,Marekani Wala Rwanda

Mama Samia anataka kupasua taifa vipande vipande kupitia chanjo zake

Somebody must stand up and tell her No no no no boldly.
 
Back
Top Bottom