Ndugu wa Hamza, mhalifu aliyeua Askari Selander bridge watiwa mbaroni na polisi

Ndugu wa Hamza, mhalifu aliyeua Askari Selander bridge watiwa mbaroni na polisi

Wengine sisi tunaona kama watu wanapeana madini wenyewe kwa wenyewe. Wapo Barrick Gold. Wapo WaSriLanka na WaThai ambao wanachukua madini mengi. Halafu wapo wananchi. Nani hasa anafaidika na haya madini yetu ya Watanzania?...
Kuna ID nyingi sana zimeingia humu JF hivi karibuni, zinakuwa ngumu sana kueleweka wanachokieleza. Mada inaanzishwa, halafu inazungushwa weeee, unashindwa kujuwa wapi pa kuanzia na wapi pa kuishia!

Hivi hii ni staili mpya ya uandishi?

Nikirudi kwenye ID mpya kwenye jukwaa hili la siasa, naona kama kuna ngwe mpya kabisa imeingia kazini hivi karibuni. Hivi kuna utaratibu wa kuachiana majukumu kwa baadhi ya wachangiaji?
 
Ndugu wa kijana Hamza aliyeuwa polisi watatu na yeye kuuawa pale daraja la salenda wametiwa mbaroni na polisi usiku huu

Ndugu wote wamekamatwa na nyumba yao imefungwa na iko chini ya ulinzi

Source: Ayo tv
Hivi kama walitaka kujua mengi ya Kiundani njia sahihi ilikuwa ni Kutomuua Kwanza bali wampige tu Risasi za Miguuni au Mikononi wayajue au Kumuua kisha waanze Kusumbua hivi Ndugu zake? Police wetu ni very unprofessional kwakweli.
 
Mtu mweusi ni Kima aliechangamka, yaani ninyi Polisi mnamdhulumu mtu kisha anawaua halafu mnaenda kuweka familia yake ndani?!
 
Ninadhani ni sahihi ndugu na marafiki wa karibu na Marehemu, Hamza wahojiwe, pengine waliona ndugu yao au rafiki yao amebadilika tabia kwa siku za karibuni au wanajua yaliyompata siku za karibuni na kuwasimulia marafiki na ndugu zake.

Hivyo ndiyo ukisikia kulisaidia Jeshi la Polisi kupata ukweli wa tukio badala ya kusikiliza maneno ya mashuhuda pekee yanayotembea kwenye mitandao. CCM iwe makini, kwenye msafara wa mamba na kenge wapo.
 
Huyo jamaa ni mteteaji mkubwa wa lile gaidi lao lililowekwa kolokoloni hivi karibuni.
Hawa hapo sio?
IMG-20210825-WA0032.jpg
 
Kama ni kweli huu ni upumbavu wa KUKURUPUKA. Ndugu kuwa mhalifu haina maana ndugu zake wote ni wahalifu labda kama kuna ushahidi wa uhalifu wa ndugu zake. Wakamate na maccm yote basi yaliyokuwa karibu na huyo muuaji. View attachment 1908450

Wewe kibaka polisi sio gerezani, mmeshazoea mtu akienda polisi mnaalika mawakili 500, wakati anakwenda kusaidia polisi tu.
 
Kuna siku nimeona jamaa analia kakamatwa kwenye fuso,kapakia mbao zake na vibali vyote anavyo lakini bado askari wakamtoa pesa ndefu.
Ramadhan Ntunzwe wa Kariakoo alifilisiwa mtaji wake kwa kukataa kutoa rushwa kwa polisi na tra,wakamzima.
Nasubiri nisikie kuhusu huyu msomali shida ni nini hasa.

Umevunja sheria halafu unaombwa hongo unakaza!!!
 
Kama ni kweli huu ni upumbavu wa KUKURUPUKA. Ndugu kuwa mhalifu haina maana ndugu zake wote ni wahalifu labda kama kuna ushahidi wa uhalifu wa ndugu zake. Wakamate na maccm yote basi yaliyokuwa karibu na huyo muuaji. View attachment 1908450
Nadhani muandishi katumia neno kamata badala ya kushikiliwa kwa mahojiano.
Ila BAK unategemea wapate taarifa toka wapi kama siyo kwa ndugu zake?
 
Nilijua haya lazma yatokee ila wasipokua makini narudia tena wasizibe shimo la panya kwa mkate
Walishamkamata Mbowe ilitosha hakuna magaidi tena zaidi ya mbowe[emoji849][emoji849][emoji849][emoji849][emoji849]
 
Ndugu wa kijana Hamza aliyeuwa polisi watatu na yeye kuuawa pale daraja la Salenda wametiwa mbaroni na polisi usiku huu

Ndugu wote wamekamatwa na nyumba yao imefungwa na iko chini ya ulinzi.

Chanzo: Ayo tv
MNAWAONEA FAMILIA. UKWELI UMEJULIKANA, TENDENI HAKI. Kila mahali CCM/serikali ni dhuluma. Dhuluma kwenye tozo, miamala Rais na Mwigulu, polisi kwenye madini na raia, dhuluma kwa Mbowe, dhuluma kwa Lisu risasi, dhuluma kwa Azory, Mawazo, viroba sandarusi maiti, dhuluma kwenye viwanja ma DED, dhuluma kwnye kura tume ya uchaguzi, maDED..............................................kila mahali DHULUMA
 
Hili tukio kubwa, ndugu hawana kosa lakini hiyo nyumba inaweza ikawa ni crime scene. Sasa ukiacha watu humo, wanaweza wanatemper na ushahidi.
Lakini Polisi nao ni mabingwa wa kutemper usije ukashangaa kukuta wamebambika na nyaraka za Chadema na kuwaambia wanandugu wa Gaidi waseme walitumwa na Mbowe.
 
Ndugu wa kijana Hamza aliyeuwa polisi watatu na yeye kuuawa pale daraja la Salenda wametiwa mbaroni na polisi usiku huu.

Ndugu wote wamekamatwa na nyumba yao imefungwa na iko chini ya ulinzi.

Chanzo: Ayo tv
Aisee, Damu ya Mbowe itawatafuna watu, nchi ilikuwa imetulia wakamsingizia.
 
Back
Top Bottom