Ndugu yangu amekuwa mlevi wa kupindukia, nataka nimpeleke sober house

Ndugu yangu amekuwa mlevi wa kupindukia, nataka nimpeleke sober house

Natumai wote hamjambo humu.

Nina ndugu yangu amekuwa mlevi wa kupindukia, hapo awali alikuwa ni mtu smart na mpambanaji wa maisha, sijui kitu gani kimemkuta, anakunywa pombe muda wote hata kazi ameacha kwa sababu ya pombe.

Watu wengi wamenishauri nimpeleke sober house {Kwa kiswahili sijui inaitwaje}

Najipanga nimpeleke japo ni gharama lakini nitajitahidi kwa sababu hali yake inanihuzunisha sana, wahusika wameniambia anaweza kukaa huko wa muda wa miezi mitatu hadi minne, na atakuwa sawa kabisa.

Wenye uzoefu na sober house, unaweza kuwa ulimpeleka ndugu yako au kama una uelewa wowote je zinasaidia kubadilisha maisha ya waraibu wa mihadarati na kurudi kwenye hali zao za kawaida?

Nb.Maoni yenu ni muhimu,

Natanguliza shukrani za dhati.

Asanteni.🙏🙏
Kuna jambo kama limejificha.
Anyway
Kama upo Dar nenda salasala kituo cha mbuyuni....Kuna ofisi ya wa missionaries wanaitwa Changamoto ni matumaini
 
Ninawajua watu wawili waliopelekwa sobb.
Wa kwanza alivyorudi alikuwa amenawiri lakini akaanza mdogo siku hizi anakunywa hadi gongo ya sogodo huko.

Wa pili tulikuwa tunakunywa wote mwaka 2015 bia, chibuku na komoni mara moja moja. Ila baadaye mimi nilihama yale mazingira. Nikasikiaga kwamba kiwango kimepanda, anakunywa sana pombe zote. Familia ikaamua kumpeleka soba na akarudi na bado anakunywa.
Mwaka huu tumeenda kuonana, nikapelekwa hadi kwenye vijiwe vyake vyote hadi tukampata kwenye ubanda mmoja maana amekuwa mnywaji kiasi hadi simu hatumii ndio maana tulimtafuta kianalojia.

Kwanza nilipofika nikamkuta yupo tungi kiasi halafu kanisahau. Jamaa yangu alivyomkumbusha vizuri ndio akanikumbuka.
Yeye kwa kinywa chake alisema ni kweli alipelekwa soba na alirudi akiwa kanenepa na alikuwa hanywi. Upweke ukamrudisha kwenye pombe hasa nyeupe au gongo. Alipoonja alijilaumu kwamba alikuwa wapi siku zote! Maana alijisikia raha iliyoje.
Mpaka muda huu ninavyoandika jamaa anakunya gongo anapumzika wakati wa kulala tu.
 
Ninawajua watu wawili waliopelekwa sobb.
Wa kwanza alivyorudi alikuwa amenawiri lakini akaanza mdogo siku hizi anakunywa hadi gongo ya sogodo huko.

Wa pili tulikuwa tunakunywa wote mwaka 2015 bia, chibuku na komoni mara moja moja. Ila baadaye mimi nilihama yale mazingira. Nikasikiaga kwamba kiwango kimepanda, anakunywa sana pombe zote. Familia ikaamua kumpeleka soba na akarudi na bado anakunywa.
Mwaka huu tumeenda kuonana, nikapelekwa hadi kwenye vijiwe vyake vyote hadi tukampata kwenye ubanda mmoja maana amekuwa mnywaji kiasi hadi simu hatumii ndio maana tulimtafuta kianalojia.

Kwanza nilipofika nikamkuta yupo tungi kiasi halafu kanisahau. Jamaa yangu alivyomkumbusha vizuri ndio akanikumbuka.
Yeye kwa kinywa chake alisema ni kweli alipelekwa soba na alirudi akiwa kanenepa na alikuwa hanywi. Upweke ukamrudisha kwenye pombe hasa nyeupe au gongo. Alipoonja alijilaumu kwamba alikuwa wapi siku zote! Maana alijisikia raha iliyoje.
Mpaka muda huu ninavyoandika jamaa anakunya gongo anapumzika wakati wa kulala tu.
Duuu
 
Ninawajua watu wawili waliopelekwa sobb.
Wa kwanza alivyorudi alikuwa amenawiri lakini akaanza mdogo siku hizi anakunywa hadi gongo ya sogodo huko.

Wa pili tulikuwa tunakunywa wote mwaka 2015 bia, chibuku na komoni mara moja moja. Ila baadaye mimi nilihama yale mazingira. Nikasikiaga kwamba kiwango kimepanda, anakunywa sana pombe zote. Familia ikaamua kumpeleka soba na akarudi na bado anakunywa.
Mwaka huu tumeenda kuonana, nikapelekwa hadi kwenye vijiwe vyake vyote hadi tukampata kwenye ubanda mmoja maana amekuwa mnywaji kiasi hadi simu hatumii ndio maana tulimtafuta kianalojia.

Kwanza nilipofika nikamkuta yupo tungi kiasi halafu kanisahau. Jamaa yangu alivyomkumbusha vizuri ndio akanikumbuka.
Yeye kwa kinywa chake alisema ni kweli alipelekwa soba na alirudi akiwa kanenepa na alikuwa hanywi. Upweke ukamrudisha kwenye pombe hasa nyeupe au gongo. Alipoonja alijilaumu kwamba alikuwa wapi siku zote! Maana alijisikia raha iliyoje.
Mpaka muda huu ninavyoandika jamaa anakunya gongo anapumzika wakati wa kulala tu.
You are very right....hapo ni Mungu tu.
Kimsingi wanaopona ni 2% .
Kweli wananenepa lakini shida haipo kwenye mwili.
 
walimpiga wenzie alikua ana kaukorofi na kaubishi ka maudhi, alitandikwa vibaya sana karibu afe ila yeye alisema eti amepata ajali.

actually wale jamaa wa pale sober walikua wakitupatia taarifa zake ila yeye anageuza anatia uongo
kaubishi ka maudhi[emoji1787][emoji1787]
 
kaubishi ka maudhi[emoji1787][emoji1787]
kichwa yake ikipoa pombe kidogo, huwa anahadithia ukweli mambo yalivyo mule ndani, utaskia anasema namnukuu

"uncle acha thu, jamaa wa mulye ndani hawanya hurthuma wanaweztha kukuua kabithaa ukiletha ubisthi, wanapiga matheke hayo ni balaa"

mwisho wa kunukuu.

anayasema hayo huku akiwa amezishika na kuzipapasapapasa taya zake zilizopishana"
 
Back
Top Bottom