Ndugu zangu wa Yanga timu mnayo kweli lakini kwanini mnaingiza mabasi uwanjani bila wachezaji na mnapitia milango isiyo rasmi, shida ni nini?

Ndugu zangu wa Yanga timu mnayo kweli lakini kwanini mnaingiza mabasi uwanjani bila wachezaji na mnapitia milango isiyo rasmi, shida ni nini?

Leonel Ateba Mbinda

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2023
Posts
644
Reaction score
2,695
Kwa kweli mmekamilika kweli sio utani, ila yapo mambo yanatufanya tuwe na wasiwasi wazee wa Jangwani.

Timu mnayo na mnaonyesha kweli mnataka bao, ile move ya Boka hadi mtu akajifunga sio masihara, yule ni Usain Bolt kabisa.

Lakini kwanini Azam jana wajifunge mabao yote matatu huku nyie mkionekana mmeingia na basi likiwa tupu halina wachezaji halafu mnapenda sana kupita milango isiyo rasmi, nyie hamuoni kuwa tunapata wasiwasi na ushindi wenu.

Soma Pia:
Kwamba kuna kitu nyuma ya pazia kinawasukuma na kuwatia nguvu wachezaji, mimi nawajua wazee wenu tena walikuwa wamekaa mbele ya jukwaa kuu, niliwaangalia weee nikasema wale ndio wale wakati wa mzee Ngozoma Matunda wamerudishwa.

Toeni ufafanuzi wazee kwanini wakati nyie mna timu nzuri lakini mnaingiza basi likiwa tupu halina wachezaji halafu wachezaji wanapandishwa magari mengine huku mkifika uwanjani mnaingia mlango mwingine tofauti na ule wa wenzenu ambao kikawaida kila timu huwa inaingilia.

Jana, kwa kweli ilikuwa kali, goli la Dube lile ukiangalia vizuri wamejifunga, Boca wamejifunga, Aziz Ki akajifunga Bangala labda la nne ndio halikuwa la kujifunga.

Mkiendelea kukaa kimya watu wataendelea kuwa na mashaka na nyie na wataamini mnashinda kwa nguvu za giza, wekeni wazi jamani
 
Kikosi kipo lakini powered na nguvu za majini,hilo lipo wazi.
Ndio maana wakikutana na timu inayotoa kafara za damu kama wao,wanalazimika kuongea na mwamuzi
 
Kwa kweli mmekamilika kweli sio utani, ila yapo mambo yanatufanya tuwe na wasiwasi wazee wa Jangwani.

Timu mnayo na mnaonyesha kweli mnataka bao, ile move ya Boka hadi mtu akajifunga sio masihara, yule ni Usain Bolt kabisa.

Lakini kwanini Azam jana wajifunge mabao yote matatu huku nyie mkionekana mmeingia na basi likiwa tupu halina wachezaji halafu mnapenda sana kupita milango isiyo rasmi, nyie hamuoni kuwa tunapata wasiwasi na ushindi wenu.

Kwamba kuna kitu nyuma ya pazia kinawasukuma na kuwatia nguvu wachezaji, mimi nawajua wazee wenu tena walikuwa wamekaa mbele ya jukwaa kuu, niliwaangalia weee nikasema wale ndio wale wakati wa mzee Ngozoma Matunda wamerudishwa.

Toeni ufafanuzi wazee kwanini wakati nyie mna timu nzuri lakini mnaingiza basi likiwa tupu halina wachezaji halafu wachezaji wanapandishwa magari mengine huku mkifika uwanjani mnaingia mlango mwingine tofauti na ule wa wenzenu ambao kikawaida kila timu huwa inaingilia.

Jana, kwa kweli ilikuwa kali, goli la Dube lile ukiangalia vizuri wamejifunga, Boca wamejifunga, Aziz Ki akajifunga Bangala labda la nne ndio halikuwa la kujifunga.

Mkiendelea kukaa kimya watu wataendelea kuwa na mashaka na nyie na wataamini mnashinda kwa nguvu za giza, wekeni wazi jamani
Mbwembwe tu zile mtani!
 
Kikosi kipo lakini powered na nguvu za majini,hilo lipo wazi.
Ndio maana wakikutana na timu inayotoa kafara za damu kama wao,wanalazimika kuongea na mwamuzi
Na nyie mlitoa kafara za damu mkapigwa Bambi ya 5-1, Kisha mkachapika Tena 2-1, aikutosha mkabutuliwa Tena 1-0, mpaka mtasema mtayamaliza yaani mechi 3 mmeambulia tugoli 2 uku mkishindiliwa magoli 8 na bado unapata ujasiri wa kuhoji ubora wa yanga?
 
Hizo ni mind game tu, mpira sio uchawi bali ni kikosi imara na benchi imara. Ingekuwa Yanga inategemea uchawi basi ungeona huko nchi za watu anavyopigiga kama ngoma kwasababu hana uwezo wa kuingia uwanjani kwa namna hiyo wala kufanya mbinu zinazoashiria ushirikina. Lakini Yanga wakiwa Tanzania ni moto na wakiwa nje ya Tanzania ni moto vile vile. Jibu ni Yanga ni timu bora na uchawi hauna nafasi kwenye mpira wa miguu, ungekuwa una nafasi basi timu zilizopo Sumbawanga zingekuwa zinabeba ligi kuu, na pia nchi zinazoongoza kwa uchawi zingekuwa zinabeba klabu bingwa na kombe la dunia.
 
Back
Top Bottom