Ndugu zangu Waislam mtaniwia radhi kidogo

Ndugu zangu Waislam mtaniwia radhi kidogo

Status
Not open for further replies.
Siamini kama hili andiko murua kaandika muislam.
Nimejaribu kufukua post zako za nyuma, jamaa hujihusishi na mijadala ya dini kabisa hivyo nimeshindwa kutambua dini yako.
kama kweli wewe ni muislam, basi ndio wa kwanza kukuona unayejitambua.
 
Ama kwa hakika wewe ni Mkristo. Kukosa kwako busara kwenye komenti yako kunathibitisha how much of a Christian ur.

Unaweza vipi ku show disrespectfulness kwa watu wa imani tofauti na yako kiasi hicho?

Wise up bro

Siamini kama hili andiko murua kaandika muislam.
Nimejaribu kufukua post zako za nyuma, jamaa hujihusishi na mijadala ya dini kabisa hivyo nimeshindwa kutambua dini yako.
kama kweli wewe ni muislam, basi ndio wa kwanza kukuona unayejitambua.
 
Hili suala la Bandari naona baadhi yenu mmelibeba katika namna fulani ya UDINI, kila nikimuangalia kiongozi wangu wa KIISLAM akisimama mahali analizungumzia katika upande wa UDINI.

Sikilizeni, TEC imejaa watu wenye ELIMU kuanzia ya Elimu Dunia hadi elimu ya DINI (THEOLOJIA), ndo maana utasikia Askofu Dr, Eng, Prof fulani fulani wa Parokia fulani. Sisi ukishamqliza kusoma Quran umemaliza, mengineyo ni majungu. Yaani mtu kama Prof Lipumba alitakiwa awe Imamu wa Msikiti fulani mahali fulani na kiongozi fulani katika nafasi za Bakwata taifa, lakini matokeo yake kule tumewaweka wengine. Sisemi kwamba waislam hatujasoma, hapana, PhD zilizopo katika nafasi za uongozi misikitini ni chache mno kulinganisha na wenzetu.

Ndo maana linapofikia jambo la kuongea na kiongozi mkuu wa nchi, hawa TEC, KKKT na mengineyo utaona utofauti, sisi runaomba kupunguziwa ama kuondolewa kodi za TENDE na kuomba tupatiwe VIFAA vya kisasa vya KUUTAZAMA MWEZI mtukufu. Wenzetu wanaomba mismaha ya kodi ya makontena ya vifaa tiba, vifaa vya elimu na mengineyo. Sisi tukishakunywa juisi za tende Ikulu tunashukuru na kuondoka na kushika shikashika videvu kama SUNNAH, tunaondoka.

Leo tunawaona TEC wabaya katika msimamo, mali zetu wenyewe tunashindwa kuzisimamia wenyewe, hapa Kinondoni nadhani kidogo tupigwe na wachache kwenye eneo letu ambalo Bakwata ipo. Tumshukuru Hayati Magufuli (Mkristo) alitusaidia na kutuombea msaada wa kujengewa Msikiti.

Kuna namna nawatazama viongozi kama wanafki, na mnafki siku zote maendeleo kwake yanakawia. Najua huu ujumbe mchungu na mnaweza hata kuitisha kikao mkanisomea ALBADIRI. Ndio, TEC wametoa WARAKA wenye HOJA, mbona hamzikosoi HOJA zao mnajikita katika UDINI? Kwani huu mkataba unaopingwa nyinyi hamkwenda IKULU pamoja nao kabla ya huu waraka? Mlienda kufanya nini? Si mlipeleka mapendekezo ya marekebisho?

Mbona leo mnasita kusema kwamba mlikuwa pamoja? UNAFKI mtupu! Ndo maana katika viongozi wa kidini namkubali Sheikh Nurdin Kishki, Mziwanda, Mazinge na Dr Sulle. Hawa hawana manenomaneno, kazi yao ni kutoa DAGH'AWA tu. Huu unafki nafki umebaki kwa wasiotambua wajibu wao. Kuna shule nyingi za kiislam, matokeo yake ni mabovu. Hatuangalii kuboresha shule zetu, tumekazana kuvaa kanzu na misuli kuzodoana. Tuache Unaa. Astaghafirulah!

Mmenikwaza sana. Kuna huo Sheikh mmoja amesema yeye atasambaza waraka wa kuunga mkono nchi nzima kama tamko la msikiti, huyu hasababishi UDINI, hachochei Udini? Nani katika Uislamu amemuonya aache huo ujinga?

Mnahitaji semina! Mnahitaji kujitokeza na tamko lenye mashiko la aidha kwa nini mnaunga mkono ama mnapinga huu mkataba na muwe na sababu za kujitosheleza. Msijitokeze kwa sababu TEC wametoa WARAKA, mnatengeneza mashindano na mtachochea vurugu zisizo na msingi wowote.

Tuache UDINI, huu mkataba haupingwi kwa sababu ulisainiwa Msikitini au mbele ya imamu na wala huu mkataba hauhusiani na msikiti kwa maana DP World hawaji kujenga misikiti wala kueneza Quran. Wanakuja kuwekeza katika bandari zetu. Tukipinga tupinge kwa hoja na tukikubali tukubali kwa hoja. Tunahitaji kueleweshana, inawezekana mimi sijaelewa na pengine akijitokeza mtu akanielewesha nitamuelewa na nitaunga mkono lakini ukitumia UDINI sintokuelewa. Maana naona kila anaesimama anasema "NYUMA YA PAZIA"; hiyo nyuma ya pazia kwenye ule waraka hiyo "NYUMA YA PAZIA " iko wapi?

Asalaam alaykum!
Tuache unafiki wenzetu upande wa Phd na Dr wametuacha hatua kidogo ukitaka kuliamini hili angalia mikutano ya rais akikaa na viongozi wa dini namna ya uchangiaji mada. Nakazia kama mtoa mada sijasema waislam hatujasoma
 
Tuache unafiki wenzetu upande wa Phd na Dr wametuacha hatua kidogo ukitaka kuliamini hili angalia mikutano ya rais akikaa na viongozi wa dini namna ya uchangiaji mada. Nakazia kama mtoa mada sijasema waislam hatujasoma
BAKWATA ni sawa ila sio waislamu.
 
Umeongea ukweli! hizi taasisi nyingi waumini hawatetei dini kazi kupambania vyeo na kufanya uwizi hamna cha maana ..

Watu wenye akili wengi wamejitoa hawahusiki na taasisi ila wanasaidia watu maskini sio kufanya uwizi na uroho wa madaraka.
Ni aina mbili ya watu aidha umuogope Mungu kwa dhati au wanafiki wanaojifocha kwa kujionyesha wana hofu ila ni majizi

Kweli kabisa bora kusaidia wanaohitaji kwa mali zako za halali na kuwa na hofu ya Mungu

Watu wanaona utajiri duniani ndio nguvu wapo wanadiriki na kusema eti kanisa la Roman lina nguvu baada ya serikali tu sasa unajiuliza je zote ni halali?
 
TEC wakosolewe kwa Hoja sio kwa mipasho!
 
Kwa Elimu ipi ajuza, nyie ambao mnakataza wanawake wasisome shule na hapo wanahitaji madaktari wa kike wazalishe wake zao.
Anasema mtume👇

"Yeyote atakayewalea mabinti wawili hadi wakakua, yeye na mimi Siku ya Kiyama tutakuwa kama hivi. (Akaonesha vidole vyake viwili iii kupigia mfano watakavyokuwa karibu sana huko Peponi).


Lengo Ia mafundisho haya ya Mtume (s.a.w) ni kuwaondosha watu katika zile fikra dhaifu za kuwaona watoto wa kike kama kwamba si watu. Na katika Hadith nyingine iliyosimuliwa pia na Ahmed, Mtume (s.a.w) amesema: Yeyote ambaye amemzaa binti, na hakumzika yungali hai, na hakumtukana au kumkashfu, na hakumpendelea mtoto wake wa kiume zaidi kuliko huyo wa kike, Allah atamuingiza Peponi. (Ahmad)


Zaidi ya mafundisho haya Mtume (s.a.w) alionesha mfano katika maisha yake mwenyewe, kwa kuwaheshimu na kuwatendea vizuri binti zake, kiasi ambacho aliwahi kusema juu ya binti yake, Fatma; "Fatma ni sehemu yangu mimi, furaha yake ni yangu, na ghadhabu zake ni uchungu wangu ".
 
1692820373473.png
 
Itakuwa hujanielewa kilichosemwa mkuu , ongeza kufikiria walioalikwa viongozi wa dini kwa waislamu huwa wanaenda akina nani? This is public
Kwamba hamna waislamu wenye PhD ? Pia angalia walioko kweny system na wale ambao hawajulikani kabisa..
 
Hili suala la Bandari naona baadhi yenu mmelibeba katika namna fulani ya UDINI, kila nikimuangalia kiongozi wangu wa KIISLAM akisimama mahali analizungumzia katika upande wa UDINI...
Hili suala ni zaid ya ulijuavyo p1 na kasoro zilizopo lkn haya majamaa kamwe hayatokua radhi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom