Uchaguzi 2020 NEC imecheza ngoma ya Tundu Lissu. Je, Wagombea walioenguliwa Ubunge Tume itawarudisha?

Uchaguzi 2020 NEC imecheza ngoma ya Tundu Lissu. Je, Wagombea walioenguliwa Ubunge Tume itawarudisha?

Kwa hiyo unasemaje?

Kwamba, wagombea udiwani na ubunge waliondolewa using the same ground wafanyweje?

Ni vyema wakarudishwa, right?

Yes. Kwa sbb kwa maelezo ya NEC na sababu za wasimamizi wa uchaguzi majimboni na katani kuwaengua baadhi ya wagombea ubunge na udiwani, obviously, hazisimami tena....

Mwisho, Tundu Lissu na wengine wote kina sisi huku we knew exactly kuwa, mgombea wa CCM Ndg John Pombe Magufuli hata kama angekuwa amevunja/kiuka sheria na kanuni za uchaguzi kwa kiwango gani, ASINGEWEZA KUHUKUMIWA KINYUME NA ILIVYOFANYIKA...!!

Lakini, kwa upande mwingine TL ame - achieve alichotaka kuki achieve...

Huu ni umahiri wa hali ya juu sana...
IMG-20200827-WA0019.jpg
angalia hizo forms. Acha kuamini ujinga

IMG-20200827-WA0012.jpg
je pinganizi la Loketo lina mashiko?
 
Haya ndio mambo Socrates alikuwa apendi kwenye democracy ya kila mtu kuamua. Akitolea mfano wa tukio la mahakamani kuna siku raia waliochaguliwa kuamua kesi, baada kusikiliza ushahidi wa pande zote jamaa wakaamua mtuhumiwa apewe adhabu ya kifo. Kesho yake asubuhi watu wale wale wakakimbilia kwa hakimu wakidai walikosea maamuzi jamaa aachiwe.

Tatizo kwake hapo sio adhabu ya kifo au kuachiwa huru zilitolewa kwa mtuhumiwa isipokuwa namna maamuzi ya raia wa kawaida yanavyofikiwa. Hakuna reasonable arguments kwanini mtu auwawe au aachwe kutokana na ushahidi wa kesi husika, isipokuwa watu wachache wenye makelele wanaweza shawishi wengine namna ya kuamua. Democracy ya mtindo huo aifai.

Ndio CDM na Lissu yaani jamaa anaweza ongea upuuzi ambao auna maana kabisa kama MIGA au pingamizi lake la jana lilivyo la ovyo kweli kisheria lakini CDM watashabikia huo upuuzi mpaka duh.
 
Yaani umeeleza maelezo marefu ambayo yanajirudia rudia halfu hayana substance yoyote. Kwa mfano, hukuelezea ni vifungu vipi vya sheria ambavyo Lissu amevitumia kuweka mapingamizi halafu havikujibiwa na Tume au imeenda kinyume chake.

Hujaeleza ni vifungu vipi vya sheria ambavyo Tume ilikiuka wakati wa kuwaeungua wagombea wengine ambapo sasa kwa hoja za Lissu itabidi iwarejeshe. Andiko lako lipo kama hadithi isiyo na mwanzo wala mwisho.
Ushabiki unawafanya watu wengine wakurupuke kuandika bila kufanya utafiti wa kukusanya facts kabla ya kuweka hoja zao kwa jamii. Mvumilie tu huyo mtoa uzi
 
Mkuu nadhani humjui vizuri Tundu Lissu.Kama unavichukulia vitu juu juu na kwa jinsi anavyopangilia maneno yake, unaweza ukaamini kile anachokiongea ni sahihi. Lissu ni Mwanasheria mbobezi anajua jinsi ya kucheza na maneno na vifungu vya sheria kama ilivyo mahakamani ili kuweza kamshawishi hakimu akubaliane na hoja zake. Mbinu hiyo hiyo ndo anaitumia pia kuwashawishi watu huku nje wasiopenda kutafakari ili waamini anachoongea.

Nimesikiliza hoja za Lissu vizuri sana, kwanza anasema JPM hawakuwasilisha fomu za uteuzi siku iliyotakiwa kisheria. Lakini sote tulimuona JPM siku ile ya tarehe 25 ambayo ni ya uteuzi akiwa na fomu zake, sasa jiulize alienda kufanya nini pale Tume.

Lakini Hoja yake hii anaijenga pia kwenye uhakiki wa wadhamini, kwamba kwann wasimamizi wa uchaguzi ndo wahakiki wadhamini (membe pia wadhamini wake wamehakikiwa na hao wasimamizi wa Jimbo lakini cha ajabu hakumwekea pingamizi). Anarudi tena kusema kwamba tume ndo iliyotoa maelekezo kwa hao wasimamizi kuhakiki wadhamini katika kila jimbo lakini hapo hapo anasema maelekezo hayo yanapingana na sheria. Lakini hafafanui kwamba sheria hiyo ndo inairuhusu Tume kukasimu madaraka yake kwa kadri itakavyoona inafaa kwa wasimamizi wa uchaguzi bila kusema ni madaraka gani. Kwahiyo mpaka hapo utaona tume haikuvunja sheria. Lakini hata kama tume ingekua imevunja sheria kwa kuwapa mamlaka wasimamizi wa uchaguzi, unawezaje kumlaumu/kumuwekea pingamizi mgombea ambae alifuata maelekezo ya Tume.

Infact, Tundu Lissu aliweka mapingamizi siyo kwa maana ya mtego bali kwa kujihami kwasbb toka mwanzo alihisi atakatwa na Tume (Tweet ya mbowe siku moja kabla ya uchaguzi inathibitisha hili) . Baada ya kuona tume haikufanya hivyo, akajua CCM au chama kingine kinaweza kutumiwa kumuwekea pingamizi baada ya uteuzi. Kwsbb anajua zilikuepo sababu nyingi sana za kumuengua isipokua watu waliamua iwe fair play wamuache agombee na ili uchaguzi uende kwa amani.

Wewe huelewi hoja zake kwanza kusema na Membe alihakikiwa huko ndo kuonesha kutokukiukwa kwa sheria Kwani Membe ndiyo sheria rubbish. Pili unasema amesema tume inaruhusiwa kukasimu mamlaka lakini ruhusa hiyo ina sharti kwenye sheria isitowe maelekezo ambayo ni kinyume na sheria. Sasa sheria inataka fomu ziwasilishwe tume ya uchaguzi kwanini tume iseme zipelekwa wa wasimamaizi wa uchaguzi wakati sheria haisemi hivo huko ni kukiuka sheria.

Ndiyo maana walilazimika kuhakiki fomu zake kwa kutumia hilo takwa la sheria ingekuwa siyo hivo kwanini wapoteze muda wao kuhakiki fomu za Lissu wakati walishatoa maelezo zihakikiwe na wazimamizi wa uchaguzi wa majimbo. Tume wamejivua nguo wameona siyo vema kuwaengua wagombea kwa makosa ya maelekezo ya tume. Kama kungekuwa na kukata rufaa hapo lingekuwa anguko kwa wagombea wote waliopeleka fomu zao kwa wazimamizi wa uchaguzi kinyume kabisa na sheria ya uchaguzi.
 
CCM wanaenda kuingiza nchi kwenye machafuko makubwa.

Tume ya Uchaguzi itengue haraka matokeo ya waliopita burebure.. Tena waanze na PM.
Hakuna machafuko yatakayotokea, wenye viherehere ndio wataumia na kuzipatisha shida familia zao huku wajanja wakiendelea na maisha yao kama kawaida
 
Nilishasema watendaji wa serikali ndio wanaosababisha matatizo kwa wananchi bali sio chama cha mapinduzi

Kwa style hii,Tume ilibidi watulie kwanza kabla ya kumjibu mtu huyo,Sasa wanaleta utata mpya kabisa kwenye uchaguzi huu

Sio kila jambo inabidi kulijibu,kuna mambo unachutama kwanza

Hawa watendaji wanakiharibia chama cha mapinduzi sana kwani wao hawako mstari wa mbele kwenye kutafuta kura

Kanuni za uchaguzi haziruhusiwi kwenda kinyume na Sheria mama ya uchaguzi haya si wanayajua Tume ya uchaguzi

Kitendo cha kumuweka Tundu lisu siku ile masaa zaidi ya saba nilitegemea haya yatajitokeza tu

Hivi Tume mngepokea fomu za jamaa haraka na kumuacha aondoke si mngekiweka chama chetu salama

Nina hakika huyu mtu hakuwaza kuja na mapingamizi bali kitendo cha kumuweka pale masaa kibao ndio madhara yake hayo

Mengi tunashauri hapa,Mfano tulishauri akija toka nje aachwe si aliachwa airport na hajatupunguzia kura na heshma kwa wananchi au nje

Mfano angesumbuliwa siku ile airport wangesema ni ccm imefanya na sio watendaji

Kwanini tunaharibu image ya chama?
Kuna mambo yanafanyika sio kwa maslahi ya chama hasa kwa watendaji
Kwa hiyo tuwasaidieje nyie wakaza shingo manake
 
Yaani umeeleza maelezo marefu ambayo yanajirudia rudia halfu hayana substance yoyote. Kwa mfano, hukuelezea ni vifungu vipi vya sheria ambavyo Lissu amevitumia kuweka mapingamizi halafu havikujibiwa na Tume au imeenda kinyume chake.

Hujaeleza ni vifungu vipi vya sheria ambavyo Tume ilikiuka wakati wa kuwaeungua wagombea wengine ambapo sasa kwa hoja za Lissu itabidi iwarejeshe. Andiko lako lipo kama hadithi isiyo na mwanzo wala mwisho.
Halafu kasifiwa kifala kweli na nyumbu wenzie
 
Wewe huelewi hoja zake kwanza kusema na Membe alihakikiwa huko ndo kuonesha kutokukiukwa kwa sheria Kwani Membe ndiyo sheria rubbish. Pili unasema amesema tume inaruhusiwa kukasimu mamlaka lakini ruhusa hiyo ina sharti kwenye sheria isitowe maelekezo ambayo ni kinyume na sheria. Sasa sheria inataka fomu ziwasilishwe tume ya uchaguzi kwanini tume iseme zipelekwa wa wasimamaizi wa uchaguzi wakati sheria haisemi hivo huko ni kukiuka sheria.

Ndiyo maana walilazimika kuhakiki fomu zake kwa kutumia hilo takwa la sheria ingekuwa siyo hivo kwanini wapoteze muda wao kuhakiki fomu za Lissu wakati walishatoa maelezo zihakikiwe na wazimamizi wa uchaguzi wa majimbo. Tume wamejivua nguo wameona siyo vema kuwaengua wagombea kwa makosa ya maelekezo ya tume. Kama kungekuwa na kukata rufaa hapo lingekuwa anguko kwa wagombea wote waliopeleka fomu zao kwa wazimamizi wa uchaguzi kinyume kabisa na sheria ya uchaguzi.
Acha ushabiki wewe, fungua akili yako. Maelekezo gani ya Tume ambayo yameenda kinyume na Sheria. Tatizo lenu hamsomi, mmezoea kukaririshwa. Majukumu ya Tume yameelezwa kwenye Sheria ikiwa ni pamoja na hilo la kuhakiki wadhamini wa wagombea. Sheria hiyo hiyo imeipa tena mamlaka Tume kukasimu baadhi ya majukumu yake kwa wasimamizi wa uchaguzi. Sasa utarudije kinyume nyume useme maelekezo ya Tume yamevunja Sheria Kwasbb jukumu la Tume ni kuhakiki wagombea. Kwahiyo lile la kukasimu majukumu linakua lina maana gani kisheria. Bora sheria ingesema wazi kwamba Tume inaweza kukasimu majukumu yake isipokua la kuhakiki wagombea. Hapo kweli Tume ingekua imevunja sheria.

Fomu za Lissu zilihakikiwa na Tume kwasbbu hakuzipaitisha kwa wasimamizi wa majimbo kama wenzake walivyofanya. Lakini hilo halikua kosa kwasbbu bado Tume inaweza kutekeleza jukumu hilo kama sheria inavyoelekeza.
 
Members, Tundu Lissu makusudi ameitega tume ya uchaguzi nayo imetegeka na kujiweka mahali penye maswali magumu na utata.

Kitendo cha tume kuyatupilia mbali mapingamizi ya Tundu Lissu juu ya wagombea urais wa CCM na CUF ni mtego mzito sana ambao Tundu Lissu alifanya kusudi kuwatega Tume ya uchaguzi.

Lengo la Tundu Lissu amefanikiwa kwa asilimia 100 kwani ameshapata msingi wa kuwaambia wananchi Tume ina ndimi mbili na hawazingatii sheria ya uchaguzi pale itakapotokea wagombea walioenguliwa hawajarudishwa na Tume ya uchaguzi.

Hoja za Tundu Lissu alizozitoa ni hoja za kisheria ambazo Tume ya uchaguzi wamejibu kwa kutofuata sheria bali kwa utashi binafsi,

Kitendo cha Tume ya uchaguzi kujibu hoja za mapingamizi mazito kisheria sasa rasmi wanaleta utata mitaani wa kisheria.

Kuokoa jahazi hapa na kujiondoa kwenye mtego huu na vurugu Tume lazima iwarudishe wagombea wote wa ubunge na udiwani walioengulia kijanja kijanja kwa utashi binafsi.

Hakika hoja za Tundu lisu za kisheria ambazo ni sheria za Tume ya Uchaguzi kuhusu mapingamizi zimeizamisha Tume ya uchaguzi yenyewe kwani Tume hawajaainisha vipengele vya sheria ya uchaguzi katika majibu yao ili kupinga hoja za Lissu.

Kuondoa sintofahamu hii sasa Tume ya uchaguzi Tundu lisu amewatega na nyinyi mmetegeka na kuingia mazima.

Ili mueleweke kwa wananchi na kuondoa utata mliofanya kwa mtego wa Tundu Lissu inawalazimu kuwarudisha wagombea wote wa udiwani na ubunge walioenguliwa na wakurugenzi.

Hoja za kisheria hupingwa kwa hoja za kisheria na vifungu vya kisheria.

Sheria tulizotunga wenyewe sasa zinageuka na kuwa msumari wa moto kwa Tume yenyewe ya uchaguzi.

Je sheria hizi zilitungwa ili kumtega nani? Tundu Lissu ametoa hoja kwa kufuata sheria za uchaguzi lakini Tume imetoa hoja kupinga mapingamizi kwa kuikwepa sheria yenyewe.
Wazee wakipita bila kupingwa huu uzi unawahusu
 
Nilishasema watendaji wa serikali ndio wanaosababisha matatizo kwa wananchi bali sio chama cha mapinduzi

Kwa style hii,Tume ilibidi watulie kwanza kabla ya kumjibu mtu huyo,Sasa wanaleta utata mpya kabisa kwenye uchaguzi huu

Sio kila jambo inabidi kulijibu,kuna mambo unachutama kwanza

Hawa watendaji wanakiharibia chama cha mapinduzi sana kwani wao hawako mstari wa mbele kwenye kutafuta kura

Kanuni za uchaguzi haziruhusiwi kwenda kinyume na Sheria mama ya uchaguzi haya si wanayajua Tume ya uchaguzi

Kitendo cha kumuweka Tundu lisu siku ile masaa zaidi ya saba nilitegemea haya yatajitokeza tu

Hivi Tume mngepokea fomu za jamaa haraka na kumuacha aondoke si mngekiweka chama chetu salama

Nina hakika huyu mtu hakuwaza kuja na mapingamizi bali kitendo cha kumuweka pale masaa kibao ndio madhara yake hayo

Mengi tunashauri hapa,Mfano tulishauri akija toka nje aachwe si aliachwa airport na hajatupunguzia kura na heshma kwa wananchi au nje

Mfano angesumbuliwa siku ile airport wangesema ni ccm imefanya na sio watendaji

Kwanini tunaharibu image ya chama?
Kuna mambo yanafanyika sio kwa maslahi ya chama hasa kwa watendaji
Mkuu usipanic, hapo hakuna lolote. Hakuna Sheria yoyote iliyovunjwa. Lissu anacheza na akili zenu. Sheria inaitaka Tume pia kujibu hayo mapingamizi baada ya kupata ufafanuzi kutoka kwa wahusika na siyo kukaa kimya. Wangeakaa kimya angekuja tena kusema sheria imevunjwa kwsbb mapingamamizi yake hayakujibiwa.Tume pia ilipaswa kujibu haya mapingamizi kwa wakati kulingana na ratiba ya uchaguzi ilivyo.
 
Tume iko sahihi katika maamuzi yake dhidi ya mapingamizi za Lissu kwa vile hazikuzingatia facts za matukio, makosa ya kiufundi kuhusu picha( iwapo ni kweli madai yake)- na ukubwa wa athari au madhara ya ukiukwaji ( gravity of the breach ) na kama itaathiri haki za msingi za mpiga kura chini ya sheria ya uchaguzi hadi kupelekea kutengua uteuzi. Aidha hakuzingatia kanuni ya kukasimu madaraka kwenye sheria ya uchaguzi wakati wa kujenga hoja.Jambo lingine kuhusu maamuzi ya mapingamizi au rufaa za majimbo zitaamuriwa kwa msingi wa merits kwa kila shauri na si vinginevyo. Cha msingi wasimamizi waruhusu rufaa kuifikia Tume na si kuzizuia ie Morogoro iwapo ni kweli. Mapingamizi ya Lissu ni ya kisiasa zaidi kutafuta umaarufu na upotoshaji.
Hivi nyie mlisoma shule gani unawezaje kuja hapa na utetezi wakisiasa kama watume kwenye hoja za kisheria weka vifungu vya sheria hapa vinavyosema makosa ya kiufundi yasamahewe na tume

ccm kutofautisha sheria na propanganda kwenu ni mtihani mkubwa napata wasiwasi hata midege mliyonunua tukipitia documents moja baada ya nyingine zitapigwa mapingamizi urais mnauchulia poa sana
 
Members, Tundu Lissu makusudi ameitega tume ya uchaguzi nayo imetegeka na kujiweka mahali penye maswali magumu na utata.

Kitendo cha tume kuyatupilia mbali mapingamizi ya Tundu Lissu juu ya wagombea urais wa CCM na CUF ni mtego mzito sana ambao Tundu Lissu alifanya kusudi kuwatega Tume ya uchaguzi.

Lengo la Tundu Lissu amefanikiwa kwa asilimia 100 kwani ameshapata msingi wa kuwaambia wananchi Tume ina ndimi mbili na hawazingatii sheria ya uchaguzi pale itakapotokea wagombea walioenguliwa hawajarudishwa na Tume ya uchaguzi.

Hoja za Tundu Lissu alizozitoa ni hoja za kisheria ambazo Tume ya uchaguzi wamejibu kwa kutofuata sheria bali kwa utashi binafsi,

Kitendo cha Tume ya uchaguzi kujibu hoja za mapingamizi mazito kisheria sasa rasmi wanaleta utata mitaani wa kisheria.

Kuokoa jahazi hapa na kujiondoa kwenye mtego huu na vurugu Tume lazima iwarudishe wagombea wote wa ubunge na udiwani walioengulia kijanja kijanja kwa utashi binafsi.

Hakika hoja za Tundu lisu za kisheria ambazo ni sheria za Tume ya Uchaguzi kuhusu mapingamizi zimeizamisha Tume ya uchaguzi yenyewe kwani Tume hawajaainisha vipengele vya sheria ya uchaguzi katika majibu yao ili kupinga hoja za Lissu.

Kuondoa sintofahamu hii sasa Tume ya uchaguzi Tundu lisu amewatega na nyinyi mmetegeka na kuingia mazima.

Ili mueleweke kwa wananchi na kuondoa utata mliofanya kwa mtego wa Tundu Lissu inawalazimu kuwarudisha wagombea wote wa udiwani na ubunge walioenguliwa na wakurugenzi.

Hoja za kisheria hupingwa kwa hoja za kisheria na vifungu vya kisheria.

Sheria tulizotunga wenyewe sasa zinageuka na kuwa msumari wa moto kwa Tume yenyewe ya uchaguzi.

Je sheria hizi zilitungwa ili kumtega nani? Tundu Lissu ametoa hoja kwa kufuata sheria za uchaguzi lakini Tume imetoa hoja kupinga mapingamizi kwa kuikwepa sheria yenyewe.
Kuna watu mnaamini Tundu lissu Anaakili kuliko Watanzania wrote hahahhaa mtoa taarifa Wa Tume kasema wamekizi Vigezo kwa maelrkezo ya Time kumbuka Mamlaka ya Tume ya sheria Pamoja na Taratibu zake sasa Kama Tundu Mapingamizi yake hayana Mashiko mnataka kulazimisha
 
NEC walivompitisha Lissu kugombea mlimsifia na mkashauri mwenyekiti wake apewe tuzo ya amani. Leo mambo yameenda kinyume na maslahi yenu mnakuja na uzi kila baada ya dk 5 kuilaumu tume.. Acheni upuuzi tume haitahukumiwa juu ya utendaji wake kwa kipimo cha imeifanyia nini chadema tu. Tume ni ya wananchi wa Tanzania sio bavicha
 
CCM wanaenda kuingiza nchi kwenye machafuko makubwa.

Tume ya Uchaguzi itengue haraka matokeo ya waliopita burebure.. Tena waanze na PM.
Ndoto Hizo hii inch haendeshwi na wendawazimu Machafuko kwa Sababu zipi za msingi
 
NEC walivompitisha Lissu kugombea mlimsifia na mkashauri mwenyekiti wake apewe tuzo ya amani. Leo mambo yameenda kinyume na maslahi yenu mnakuja na uzi kila baada ya dk 5 kuilaumu tume.. Acheni upuuzi tume haitahukumiwa juu ya utendaji wake kwa kipimo cha imeifanyia nini chadema tu. Tume ni ya wananchi wa Tanzania sio bavicha
Hawa Tabia Yao Kulalamika Kuanzia mwenyeketi Wa Chama mpka mwanachama Wa Kawaida
 
Back
Top Bottom