Uchaguzi 2020 NEC imecheza ngoma ya Tundu Lissu. Je, Wagombea walioenguliwa Ubunge Tume itawarudisha?

angalia hizo forms. Acha kuamini ujinga

je pinganizi la Loketo lina mashiko?
 
Haya ndio mambo Socrates alikuwa apendi kwenye democracy ya kila mtu kuamua. Akitolea mfano wa tukio la mahakamani kuna siku raia waliochaguliwa kuamua kesi, baada kusikiliza ushahidi wa pande zote jamaa wakaamua mtuhumiwa apewe adhabu ya kifo. Kesho yake asubuhi watu wale wale wakakimbilia kwa hakimu wakidai walikosea maamuzi jamaa aachiwe.

Tatizo kwake hapo sio adhabu ya kifo au kuachiwa huru zilitolewa kwa mtuhumiwa isipokuwa namna maamuzi ya raia wa kawaida yanavyofikiwa. Hakuna reasonable arguments kwanini mtu auwawe au aachwe kutokana na ushahidi wa kesi husika, isipokuwa watu wachache wenye makelele wanaweza shawishi wengine namna ya kuamua. Democracy ya mtindo huo aifai.

Ndio CDM na Lissu yaani jamaa anaweza ongea upuuzi ambao auna maana kabisa kama MIGA au pingamizi lake la jana lilivyo la ovyo kweli kisheria lakini CDM watashabikia huo upuuzi mpaka duh.
 
Ushabiki unawafanya watu wengine wakurupuke kuandika bila kufanya utafiti wa kukusanya facts kabla ya kuweka hoja zao kwa jamii. Mvumilie tu huyo mtoa uzi
 

Wewe huelewi hoja zake kwanza kusema na Membe alihakikiwa huko ndo kuonesha kutokukiukwa kwa sheria Kwani Membe ndiyo sheria rubbish. Pili unasema amesema tume inaruhusiwa kukasimu mamlaka lakini ruhusa hiyo ina sharti kwenye sheria isitowe maelekezo ambayo ni kinyume na sheria. Sasa sheria inataka fomu ziwasilishwe tume ya uchaguzi kwanini tume iseme zipelekwa wa wasimamaizi wa uchaguzi wakati sheria haisemi hivo huko ni kukiuka sheria.

Ndiyo maana walilazimika kuhakiki fomu zake kwa kutumia hilo takwa la sheria ingekuwa siyo hivo kwanini wapoteze muda wao kuhakiki fomu za Lissu wakati walishatoa maelezo zihakikiwe na wazimamizi wa uchaguzi wa majimbo. Tume wamejivua nguo wameona siyo vema kuwaengua wagombea kwa makosa ya maelekezo ya tume. Kama kungekuwa na kukata rufaa hapo lingekuwa anguko kwa wagombea wote waliopeleka fomu zao kwa wazimamizi wa uchaguzi kinyume kabisa na sheria ya uchaguzi.
 
CCM wanaenda kuingiza nchi kwenye machafuko makubwa.

Tume ya Uchaguzi itengue haraka matokeo ya waliopita burebure.. Tena waanze na PM.
Hakuna machafuko yatakayotokea, wenye viherehere ndio wataumia na kuzipatisha shida familia zao huku wajanja wakiendelea na maisha yao kama kawaida
 
Kwa hiyo tuwasaidieje nyie wakaza shingo manake
 
Halafu kasifiwa kifala kweli na nyumbu wenzie
 
Acha ushabiki wewe, fungua akili yako. Maelekezo gani ya Tume ambayo yameenda kinyume na Sheria. Tatizo lenu hamsomi, mmezoea kukaririshwa. Majukumu ya Tume yameelezwa kwenye Sheria ikiwa ni pamoja na hilo la kuhakiki wadhamini wa wagombea. Sheria hiyo hiyo imeipa tena mamlaka Tume kukasimu baadhi ya majukumu yake kwa wasimamizi wa uchaguzi. Sasa utarudije kinyume nyume useme maelekezo ya Tume yamevunja Sheria Kwasbb jukumu la Tume ni kuhakiki wagombea. Kwahiyo lile la kukasimu majukumu linakua lina maana gani kisheria. Bora sheria ingesema wazi kwamba Tume inaweza kukasimu majukumu yake isipokua la kuhakiki wagombea. Hapo kweli Tume ingekua imevunja sheria.

Fomu za Lissu zilihakikiwa na Tume kwasbbu hakuzipaitisha kwa wasimamizi wa majimbo kama wenzake walivyofanya. Lakini hilo halikua kosa kwasbbu bado Tume inaweza kutekeleza jukumu hilo kama sheria inavyoelekeza.
 
Wazee wakipita bila kupingwa huu uzi unawahusu
 
Mkuu usipanic, hapo hakuna lolote. Hakuna Sheria yoyote iliyovunjwa. Lissu anacheza na akili zenu. Sheria inaitaka Tume pia kujibu hayo mapingamizi baada ya kupata ufafanuzi kutoka kwa wahusika na siyo kukaa kimya. Wangeakaa kimya angekuja tena kusema sheria imevunjwa kwsbb mapingamamizi yake hayakujibiwa.Tume pia ilipaswa kujibu haya mapingamizi kwa wakati kulingana na ratiba ya uchaguzi ilivyo.
 
Hivi nyie mlisoma shule gani unawezaje kuja hapa na utetezi wakisiasa kama watume kwenye hoja za kisheria weka vifungu vya sheria hapa vinavyosema makosa ya kiufundi yasamahewe na tume

ccm kutofautisha sheria na propanganda kwenu ni mtihani mkubwa napata wasiwasi hata midege mliyonunua tukipitia documents moja baada ya nyingine zitapigwa mapingamizi urais mnauchulia poa sana
 
Kuna watu mnaamini Tundu lissu Anaakili kuliko Watanzania wrote hahahhaa mtoa taarifa Wa Tume kasema wamekizi Vigezo kwa maelrkezo ya Time kumbuka Mamlaka ya Tume ya sheria Pamoja na Taratibu zake sasa Kama Tundu Mapingamizi yake hayana Mashiko mnataka kulazimisha
 
NEC walivompitisha Lissu kugombea mlimsifia na mkashauri mwenyekiti wake apewe tuzo ya amani. Leo mambo yameenda kinyume na maslahi yenu mnakuja na uzi kila baada ya dk 5 kuilaumu tume.. Acheni upuuzi tume haitahukumiwa juu ya utendaji wake kwa kipimo cha imeifanyia nini chadema tu. Tume ni ya wananchi wa Tanzania sio bavicha
 
CCM wanaenda kuingiza nchi kwenye machafuko makubwa.

Tume ya Uchaguzi itengue haraka matokeo ya waliopita burebure.. Tena waanze na PM.
Ndoto Hizo hii inch haendeshwi na wendawazimu Machafuko kwa Sababu zipi za msingi
 
Hawa Tabia Yao Kulalamika Kuanzia mwenyeketi Wa Chama mpka mwanachama Wa Kawaida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…