NEC: Jina la Tundu Lissu liko mwisho wa karatasi ya kupiga kura kwasababu alirejesha fomu akiwa wa mwisho

NEC: Jina la Tundu Lissu liko mwisho wa karatasi ya kupiga kura kwasababu alirejesha fomu akiwa wa mwisho

Hii Kali, kwamba kwenye urais walifata nani alianza kuingia ofisi za tume lakini kwenye ubunge walifata alphabet
 
Tena wameturahisishia sn kulijua hilo ukifika kituoni ukipewa karatasi yako moja kwa moja nyooka hadi chini ya karatasi utalikuta jina la lisu piga tiki mchezo kwisha
 
kwahiyo walimweka mwisho kurudisha fomu ili ku justify kumweka mwisho kwenye karatasi!


Hawakupokea fomu zake mapema MPAKA alilalamika KUWEKWA chumba cha MAPOKEZI KWA MUDA MREFU.

ILI KUHALALISHA KUWA WA MWISHO.

LAKINI KUMBUKA "WA KWANZA ATAKUWA WA MWISHO NA WA MWISHO ATAKUWA WA KWANZA"
 
Kwa kawaida majina huwa yanapangwa kwa alphabet

Nilitegemea waanze na ACT
 
Ni leo tu au ndio utaratibu miaka yote huo? Maana angerudisha wa kwanza mngemuweka mwisha kwa kigezo cha herufi ya jina lake ‘T’ iko chini sana kwenye mtiririko wa alphabet
Kwani waliopanga ratiba ya kurudisha form si ni NEC?
 
Wameweka mwishoni bila hata wao kujua reason ule ni unabii ni lzm utimie wa kwanza atakuwa wa mwisho na wa mwisho atakuwa wa kwanza. Utawala huu dhalimu umefanya makufuru mengi Sana ya kumtukana Mwenyezi Mungu nae ameuondolea kibali machoni pa Mbingu na duniani. Ameufuta kwenye anga thus umefurukuta lzm utaanguka
 
Hawakupokea fomu zake mapema MPAKA alilalamika KUWEKWA chumba cha MAPOKEZI KWA MUDA MREFU.

ILI KUHALALISHA KUWA WA MWISHO.

LAKINI KUMBUKA "WA KWANZA ATAKUWA WA MWISHO NA WA MWISHO ATAKUWA WA KWANZA"
Imenenwa na Mungu. AMEN
 
Akihojiwa na kituo cha redio Kagera Community Radio(KCR FM) leo asubuhi Ofisa elimu kwa umma kutoka Tume ya uchaguzi (NEC Bw Titus Mwanzalila amesema kigezo kilichotumika ni urejeshwaji wa fomu za wagombea Urais ambapo mgombea wa Urais kupitia CCM John Magufuli alirejesha fomu akiwa wa kwanza na Tundu Lissu alirejesha akiwa wa mwisho.

Ameongeza kuwa kwa ngazi za ubunge na udiwani wagombea walipangwa katika karatasi za kura kwa maelekezo ya Tume

Hata hivyo amesema hiyo si sababu ya mpiga kura kutompigia kura mgombea anayemtaka.

Katika hatua nyingine amesema tume imejipanga kikamilifu kuondoa changamoto katika mchakato huu wa uchaguzi.

Nikipata nafasi nitawawekea audio clip
mbarikiwe

Byabato
Bukoba.
Ha ha ha
 
Back
Top Bottom