Nehemia Mchechu bila ya ‘speed governor’ ni tatizo. Ndugu zangu wa mitaa ya ‘Al Muntazir’ Upanga mjipange

Nehemia ni aina ya watendaji wapendao sifa za kijinga na mshirika wa mafisadi na ndiyo maana JPM alimla kichwa.

Vilevile, huyo ni mmoja wa waliorejeshwa na Samia ili kumkomoa marehemu JPM 😄
Heee! hii mpya, unamkomoaje mtu aliyekufa?
 
Tuwache porojo, hilo shirika asili yake ni nyumba walizodhulumiwa watu, kinachowashangaza nini? Waliodhulumu wakajiweka kwenye majunba kama vile walijenga wao au baba zao na wao zqmu yao ya kulipa dhuluma imafika.

Waliotaifishwa hayo majumba wengine walikufa kwa shock. Wengine wakawa masikini hawana hata pakuishi.

Sasa ni zamu ya wenye asili ya majunba na viwanja hivyo kurudisha tena haki yao kwa njia aliyoiona Mwenyewe mgawaji mali inafaa.

Iwe Msechu au mwengine yeyote, zitqrudi tu kwa wenye haki nazo. Haki ya ntu haipotei duniani.
 
Mleta mada hauko sahihi, nahisi una maslahi binafsi.

Kuweka sawa hili, ngoja niandike machache kufafanua.

1. Hatuwezi kuwapangia nini cha kufanya NHC kwenye nyumba wanazozimiliki. Lolote watakaloliamua ni haki yao, kwa kuwa nyumba ni zao.

2. Hakuna upangaji wa kudumu au milele kwenye nyumba za NHC. Mpangaji yoyote anaweza kuondolewa mkataba wake ukiisha. Shirika litakupa notice ya miezi mitatu kabla ya mkataba wako kwisha kuwa uondoke, baada ya hapo utajua utakapokwenda, na shirika haliwajibiki.

3. Unapopangishwa ndani ya nyumba za NHC kisheria hupaswi kuendeleza, kukarabati au kuboresha chochote. Mambo hayo ni jukumu la shirika sio la kwako, na ikitokea umefanya hayo kwa nia njema kabisa hiyo itakuwa ni hisani (hupaswi kudai kufidiwa chochote) otherwise uwe na mapatano ya kisheria katika hilo na NHC. Na ikiwa sheria/mkataba utakiukwa ni vyema kukimbilia mahakamani kupinga.

4. Sehemu kubwa ya wapangaji wa asili kwenye nyumba za NHC (nyingi zikiwa Prime area) ni kama wanakaa bure, kodi wanayolipishwa ni ndogo mnoo kuliko kodi ya kupangishwa mitaa ya uswahili tena nyumba iliyochoka vibaya sana. Na kwa hali hiyo hakuna mpangaji wa NHC ambaye yuko tayari kutoka kwenye nyumba za NHC kirahisi.

5. NHC ilishabadilisha sera zake kutoka kwenye ujamaa (umaskini, huduma, hisani, umma) na kuingia kwenye ubebari (soko, ushindani, biashara, faida), hivyo ni lazima wawe na nyumba za kisasa na mwenye nguvu ya pesa ndio akae kwenye nyumba zake. Hayo yalifanyika ili NHC iweze kufufuka baada ya kuwa imeshakufa!

6. Pamoja na ufisadi mwingi, makando makando mengi ya Mchechu, lakini kiukweli ndio mtu aliyeweza kuinua upya NHC kuwa ya kisasa na kuweza kuwekeza kibebari. Yule jamaa ni mwizi kweli lakini ni mwamba haswaa.

7. Suala la NHC kuwekeza kwa ubia au kibebari haliwezi kuepukika kwa sasa, ndio dunia ya real estate ilipofikia. Japokuwa katika uwekezaji huo kuna upigaji wa kutisha, suluhisho sio kuzuia ubebari au ubia wa uwekezaji, suluhisho ni kuwa na uwazi na umakini katika uwekezaji huo.
 
Sasa kama wajua yote haya na sheria zipo si uende mahakamani kama unahisi haki yako itadhulikiwa?
Fudia ndo nini wee ma.laya
Umeelewa ndio maana unakwepa kujibu.
 
Wewe kama ni mnyonge tafuta maeneo ya wanyonge sio ukae eneo ambalo linaweza kuwa productive kwa kisingizio cha unyonge..

Ujinga wa dizaini hii haukubaliki.kwenye Dunia ya Sasa.
Pumbav...wenye pesa wanaenda kuanzisha miji mipya ambayo ni ya kisasa......ndo maana ukienda katikati ya jiji la London utakuta majengo ya kale yenye miaka zaidi ya miatano, makazi ya kisasa yanajengwa pembezoni
 
Pumbav...wenye pesa wanaenda kuanzisha miji mipya ambayo ni ya kisasa......ndo maana ukienda katikati ya jiji la London utakuta majengo ya kale yenye miaka zaidi ya miatano, makazi ya kisasa yanajengwa pembezoni
NHC sio ya wenye pesa ni shirika la umma la kuleta faida sio kutumiwa vibaya na nyie mnaojiita wanyonge kufilisi shirika..

Serikali inaweza twaa eneo lolote la jamhuri inapoona linafaa kwa maslahi zaidi ya wengi hata ikibidi kuharibu maslahi yenu nyie wachache mnaojificha kwenye koti la unyonge..
 
Ndipo tulipofikia hapo yaani hawa watu, hawana utu wala huruma.

Ni tamaa kwenda mbele
Hizo ni dili za upigaji, watu wanataka kuvuta rushwa kubwakubwa kwa kuwakandamiza wanyonge. Hao matajiri wakatafute maeneo pembezoni wajenge hizo prime areas, siyo kukandamiza wanyonge.
 
Nyie ndo wale mlisema hamjengi mtakaa City Centre ama?

Kwa Shirika hayo ni maamuzi ya manufaa zaidi..

Mmenunua hapo au ni wapangaji?
 
Zinataka kutofautishwa sehemu za mabwana na watwana !! Mchechu from North ??!!
Hilo shirika lilianzishwa kutoa unafuu wa makazi kwa wafanyakazi na watu wa kawaida wakazi wa mjini, lakini tunashanga limebadilika kuwa la kuwajengea matajiri nyumba na sasa wanataka kumilikisha matajiri maeneo wanayoita prime areas kwa kujificha kwenye kichaka cha ubia.​
 
Embu tuwaze tu kisayansi.
Kuna jengo la ghorofa mbili la kizamani (chakavu!)la NHC lipo Upanga ambalo lina wapangaji watatu, kwa mwezi linaipa NHC jumla ya kodi ya shilingi laki tatu tena kwa kushikana mashati!

Anatokea mwekezaji anataka hilo eneo ili kujenga jengo jipya la kisasa kwa ubia na NHC. Atavunja hilo jengo na ndani ya mwaka mmoja Atajenga jengo jipya lenye urefu wa ghorofa 15, ghorofa tano za juu atawapa NHC (ambazo zitapangishwa kwa wapangaji 20, kwa mwezi wapangaji hao kwa jumla watailipa NHC wastani wa shilingi 10milioni bila longolongo!).


Sasa utawashauri NHC wabakie na jengo lao la kizamani ili kuvuna laki tatu kwa mwezi, au waingie ubia ili kuvuna milioni 10 kwa mwezi?
 
Mikataba inasemaje?

Kama mna haki nendeni mahakamani..ni issue ndogo tu mbona
Hapo hakuna cha mikataba inasemaje, shirika linakusanya kodi kwa nini lisikarabati na kujenga nyumba badala ya kutaka kuwapa matajiri hizo nyumba kwa kisingizio cha kuingia ubia, yanajengwa mazingira ya upigaji na rushwa nono nono.​
 

Hiyo ni moja ya sheria amongst several others inazo regulate hilo shirika jinsi litakavyoendeshwa na right of occupancy za wapangaji.

Mimi sio mwanasheria wa wapangaji kusema nipitie zote ila kwa kuwa ni nchi ya kufanya copy and paste ya sheria; ukipitia zote hitimisho litakuwa ni hilo hilo sio sahihi kutoa watu kiholela holela.

Kuna angle nyingi huu mjadala ungeweza ongelewa financial appraisal ya hiyo miradi au uhalali wa sheria kuvunja nyumba na kuwatoa watu kama mbwa.

Binafsi sikuwa na shida na ya angle hizo; isopokuwa ethics za hiyo sera ni shida na za unyanyasaji hakuna serikali makini inayoheshimu watu wake au CSR demands za dunia ya leo inayoweza ruhusu ata private business kuvunja mikataba ya wapangaji na kubomoa nyumba bila ya kuelewa tenants wanaenda wapi.

Mimi sitakuwa muhanga wa hilo zoezi isipokuwa hiyo sio approach sahihi ya uwekezaji wa serikali ni watu waliokosa ubinifu na utu ndio wanapenda suluhisho za ivyo zenye kuwaumiza wengine.

As for me usiku mwema and thanks all for your input.
 
Naona anagengeneza MAZINGIRA ya kampuni inaitwa AMBONI GROUP kuwa mnufaika.
 
Hapo hakuna cha mikataba inasemaje, shirika linakusanya kodi kwa nini lisikarabati na kujenga nyumba badala ya kutaka kuwapa matajiri hizo nyumba kwa kisingizio cha kuingia ubia, yanajengwa mazingira ya upigaji na rushwa nono nono.​
Sasa km unataka kukwepa mikataba unakua unaukataa uhalisia na haya ni malalamiko baseless kabisa
We mtu anaweza kukupangia nyumba yako uifanyeje/uitumie vipi?

Cha kuazima hakistiri matako jmn mjenge..waliojenga Boko Bunju nk si kwamba UN Road AlMuntazir hawakupaona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…