NEMC wamedhamiria kuua baishara ya baa na sanaa kwa ujumla. Baa itaendeshwa vipi bila muziki? Liquid Bar wamezuiwa kupiga muziki

NEMC wamedhamiria kuua baishara ya baa na sanaa kwa ujumla. Baa itaendeshwa vipi bila muziki? Liquid Bar wamezuiwa kupiga muziki

Leak

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2012
Posts
52,916
Reaction score
43,505
Rais Samia kupitia NEMC umeaamua kuuwa baishara za watu na kuuwa biashara za watu ni sawa na kuuwa watu kabisa!

Mh Rais wewe na wasaidizi wako mnakula raha kila siku na mko angani kila siku mnakula asali lakini sisi wananchi wengine burudani yetu ni muziki lakini mmeona tunafaidi sana ndio maana sasa mnaitumia NEMC kuhakikisha mnatupora hata hiki tulichobakiwa nacho!

Mh ukiwasikiliza baadhi ya wamiliki wa bar utagundua kabisa NEMC sasa hawana tofauti na TRA wanao funga biashara za watu Pia ni wazi kabisa hata wamiliki wenyewe hawajui kabisa hicho kipimo cha kelele badala yake wanashitukizwa na kuambiwa muziki umezidi kiwango hivyo wanafungiwa bar zao na biashara!

NEMC wamekwenda mbele zaidi wanazifungua baadhi ya bar na kumbi kutokupiga muziki kabisa…kupitia EFM nimewasikia baadhi ya wamiliki wa bar wakieleza kwa uchungu jinsi ambavyo wameharibiwa biashara zao!

NEMC wamekwenda mbele zaidi wamezifungia kabisa baadhi ya bar kupiga muziki kabisa ikiwemo Liquid bar ya Dar.

Hivi kweli bar gani itaendeshwa bila muziki nchi hii? Mama Samia hawafanya biashara mnataka wakale wapi? Wataishi vipi?

Hivi kwanini mnataka kuigeuza nchi hii ni ya kidini?

Jamani pesa za serikali mnazitumbua peke yenu na hakuna anayewafanya chochote sasa mnatuzuia hata sisi kuburudika na muzuki? Mnataka tukaishi wapi?
 
Nchi ina wajuaji wengi wanaonuka umasikini na wivu wa kutosha.

Wasichojua tunategemeana sana...

Unafunga bar Lakin TRA wanadai VAT returns ya 18% bado SDL na Takataka kibao...

Kelele kwa baa hapana., ila kwa maspika ya makanisa sawa..

Nchi ina mamlaka zaid ya 40 na zote zinasimamia kitu kimoja.
 
Nikiona utetezi wa aina yeyote una "mnataka tukale wapi" nakuwa na wasiwasi nao. Sheria za mazingira si unazijua? Jitetee kwa kutumia sheria badala ya kutia huruma, badala ya kusema wanaua biashara zenu ambavyo ni accusation jiulize kama umezingatia sheria za NEMC na jitetee kisheria kama umekidhi vigezo vya kutoa huduma.

Kifungu fulani cha mwaka fulani kinataka bar iwe mita kadhaa nje ya makazi ya watu, na umetimiza.
Au ukiwa kwenye makazi ya watu upige mziki chini ya decibel ngapi, na umetimiza.

Mambo ya nitakula wapi nami naweza kuja kufungua dampo la kukodisha hapo pembeni ya bar yako likatoa harufu kali kisha niwalilie NEMC wasifunge maana nitakula wapi. Kuna sheria na huruma, inashangaza wabongo tunakimbilia huruma tunaacha sheria
 
Nchi ina wajuaji wengi wanaonuka umasikini na wivu wa kutosha.

Wasichojua tunategemeana sana...

Unafunga bar Lakin TRA wanadai VAT returns ya 18% bado SDL na Takataka kibao...

Kelele kwa baa hapana., ila kwa maspika ya makanisa sawa..

Nchi ina mamlaka zaid ya 40 na zote zinasimamia kitu kimoja.
Sio kweli kuwa maspika kanisani yanaruhusiwa kupaza sauti.
Wachungaji wameitwa na kupewa semina kuwa hawatakiwi kuwa na kelele za kuvuka kiwango.
Haya ni maandalizi ya kufuatiliwa na kuchukuliwa hatua.
Katila hili niko na serikali 100%
 
Nikiona utetezi wa aina yeyote una "mnataka tukale wapi" nakuwa na wasiwasi nao. Sheria za mazingira si unazijua? Jitetee kwa kutumia sheria badala ya kutia huruma, badala ya kusema wanaua biashara zenu ambavyo ni accusation jiulize kama umezingatia sheria za NEMC na jitetee kisheria kama umekidhi vigezo vya kutoa huduma.
Kifungu fulani cha mwaka fulani kinataka bar iwe mita kadhaa nje ya makazi ya watu, na umetimiza.
Au ukiwa kwenye makazi ya watu upige mziki chini ya decibel ngapi, na umetimiza.

Mambo ya nitakula wapi nami naweza kuja kufungua dampo la kukodisha hapo pembeni ya bar yako likatoa harufu kali kisha niwalilie NEMC wasifunge maana nitakula wapi. Kuna sheria na huruma, inashangaza wabongo tunakimbilia huruma tunaacha sheria
Bro nchi ina watu wa ajabu, hawapendi utaratibu wala sheria...go NEMC
 
Nchi ina wajuaji wengi wanaonuka umasikini na wivu wa kutosha.

Wasichojua tunategemeana sana...

Unafunga bar Lakin TRA wanadai VAT returns ya 18% bado SDL na Takataka kibao...

Kelele kwa baa hapana., ila kwa maspika ya makanisa sawa..

Nchi ina mamlaka zaid ya 40 na zote zinasimamia kitu kimoja.
Ongezea na vipaza sauti vya adhana apo juu
 
Rais Samia kupitia NEMC umeaamua kuuwa baishara za watu na kuuwa biashara za watu ni sawa na kuuwa watu kabisa!

Mh Rais wewe na wasaidizi wako mnakula raha kila siku na mko angani kila siku mnakula asali lakini sisi wananchi wengine burudani yetu ni muziki lakini mmeona tunafaidi sana ndio maana sasa mnaitumia NEMC kuhakikisha mnatupora hata hiki tulichobakiwa nacho!

Mh ukiwasikiliza baadhi ya wamiliki wa bar utagundua kabisa NEMC sasa hawana tofauti na TRA wanao funga biashara za watu…pia ni wazi kabisa hata wamiliki wenyewe hawajui kabisa hicho kipimo cha kelele badala yake wanashitukizwa na kuambiwa muziki umezidi kiwango hivyo wanafungiwa bar zao na biashara!

NEMC wamekwenda mbele zaidi wanazifungua baadhi ya bar na kumbi kutokupiga muziki kabisa…kupitia EFM nimewasikia baadhi ya wamiliki wa bar wakieleza kwa uchungu jinsi ambavyo wameharibiwa biashara zao!

NEMC wamekwenda mbele zaidi wamezifungia kabisa baadhi ya bar kupiga muziki kabisa ikiwemo Liquid bar ya dar…

Hivi kweli bar gani itaendeshwa bila muziki nchi hii? Mama Samia hawafanya biashara mnataka wakale wapi? Wataishi vipi?
Hivi kwanini mnataka kuigeuza nchi hii ni ya kidini?

Jamani pesa za serikali mnazitumbua peke yenu na hakuna anayewafanya chochote sasa mnatuzuia hata sisi kuburudika na muzuki? Mnataka tukaishi wapi?

Ha ha ha, haya wanayofanya ni Marudio, wataruhusu tu.
 
Back
Top Bottom