NEMC wamedhamiria kuua baishara ya baa na sanaa kwa ujumla. Baa itaendeshwa vipi bila muziki? Liquid Bar wamezuiwa kupiga muziki

NEMC wamedhamiria kuua baishara ya baa na sanaa kwa ujumla. Baa itaendeshwa vipi bila muziki? Liquid Bar wamezuiwa kupiga muziki

Pia kelele za alaakbaaaaar alaaa akbaaar saa 11 alfajiri zinakera sana
 
Rais Samia kupitia NEMC umeaamua kuuwa baishara za watu na kuuwa biashara za watu ni sawa na kuuwa watu kabisa!

Mh Rais wewe na wasaidizi wako mnakula raha kila siku na mko angani kila siku mnakula asali lakini sisi wananchi wengine burudani yetu ni muziki lakini mmeona tunafaidi sana ndio maana sasa mnaitumia NEMC kuhakikisha mnatupora hata hiki tulichobakiwa nacho!

Mh ukiwasikiliza baadhi ya wamiliki wa bar utagundua kabisa NEMC sasa hawana tofauti na TRA wanao funga biashara za watu…pia ni wazi kabisa hata wamiliki wenyewe hawajui kabisa hicho kipimo cha kelele badala yake wanashitukizwa na kuambiwa muziki umezidi kiwango hivyo wanafungiwa bar zao na biashara!

NEMC wamekwenda mbele zaidi wanazifungua baadhi ya bar na kumbi kutokupiga muziki kabisa…kupitia EFM nimewasikia baadhi ya wamiliki wa bar wakieleza kwa uchungu jinsi ambavyo wameharibiwa biashara zao!

NEMC wamekwenda mbele zaidi wamezifungia kabisa baadhi ya bar kupiga muziki kabisa ikiwemo Liquid bar ya Dar.

Hivi kweli bar gani itaendeshwa bila muziki nchi hii? Mama Samia hawafanya biashara mnataka wakale wapi? Wataishi vipi?

Hivi kwanini mnataka kuigeuza nchi hii ni ya kidini?

Jamani pesa za serikali mnazitumbua peke yenu na hakuna anayewafanya chochote sasa mnatuzuia hata sisi kuburudika na muzuki? Mnataka tukaishi wapi?
Hamjazuiwa kupiga mziki ila mmeambiwa mfunge sound proof. Kiu ya pombe hailetwi na muziki
 
Kuna tofauti kubwa sana huku na huko
Nyie naona bila kelele hamuwezi kuishi mkuu
Nikija likizo kuna machinga mmoja huwa ananikera kwa spika yake ya siku nzima yaani ni kila siku
Hata Pub zote zikifungwa Wazaramo na ngoma zao huburudisha sana. Watanganyika bila ya makelele hatupati burdani ya maisha.
 
NAIPONGEZA SERIKALI KWA KUKUMBUKA KUSIMAMIA SHERIA ZILIZOPO TATIZO MSIPO SIMAMA KIDETE WATAWAZUNGUKA MAANA WAVUNJA SHERIA WANANGUVU YA PESA NA WANAZITUMIA KUVUNJA SHERIA.
HUYU MTU WA AJABU KUMUUNGANISHA MH.RAIS NA JAMBO LA KISHERIA TENA ZA SIKU NYINGI.
 
Rais Samia kupitia NEMC umeaamua kuuwa baishara za watu na kuuwa biashara za watu ni sawa na kuuwa watu kabisa!

Mh Rais wewe na wasaidizi wako mnakula raha kila siku na mko angani kila siku mnakula asali lakini sisi wananchi wengine burudani yetu ni muziki lakini mmeona tunafaidi sana ndio maana sasa mnaitumia NEMC kuhakikisha mnatupora hata hiki tulichobakiwa nacho!

Mh ukiwasikiliza baadhi ya wamiliki wa bar utagundua kabisa NEMC sasa hawana tofauti na TRA wanao funga biashara za watu…pia ni wazi kabisa hata wamiliki wenyewe hawajui kabisa hicho kipimo cha kelele badala yake wanashitukizwa na kuambiwa muziki umezidi kiwango hivyo wanafungiwa bar zao na biashara!

NEMC wamekwenda mbele zaidi wanazifungua baadhi ya bar na kumbi kutokupiga muziki kabisa…kupitia EFM nimewasikia baadhi ya wamiliki wa bar wakieleza kwa uchungu jinsi ambavyo wameharibiwa biashara zao!

NEMC wamekwenda mbele zaidi wamezifungia kabisa baadhi ya bar kupiga muziki kabisa ikiwemo Liquid bar ya Dar.

Hivi kweli bar gani itaendeshwa bila muziki nchi hii? Mama Samia hawafanya biashara mnataka wakale wapi? Wataishi vipi?

Hivi kwanini mnataka kuigeuza nchi hii ni ya kidini?

Jamani pesa za serikali mnazitumbua peke yenu na hakuna anayewafanya chochote sasa mnatuzuia hata sisi kuburudika na muzuki? Mnataka tukaishi wapi?
Kunawanywaji wengi hawataki kelele za muziki, mbona hoteli zina baa na hazina makelele.
Hao wanaopiga muziki wameambiwa wakanunue mita ya kupima kiwango cha sati(db) ila hawataki kwani tunaishi kwa mazoea ya ujeuri, na hili la sauti mbona lipo miaka yote.
 
NAIPONGEZA SERIKALI KWA KUKUMBUKA KUSIMAMIA SHERIA ZILIZOPO TATIZO MSIPO SIMAMA KIDETE WATAWAZUNGUKA MAANA WAVUNJA SHERIA WANANGUVU YA PESA NA WANAZITUMIA KUVUNJA SHERIA.
HUYU MTU WA AJABU KUMUUNGANISHA MH.RAIS NA JAMBO LA KISHERIA TENA ZA SIKU NYINGI.
Sheria zinazosema. CAG akishawataja wezi wa mali za Umma wachukuliwe hatua mbona hazifuatwi?
 
Kati ya sheria iliyokuwepo lakini haitekekezwi ni ya kuzuia makelele na mitetemo.
Nchi hii si usiku si mchana mtu anaweza kuamua kufunga mifumo yake ya sauti na mitetemo. Na akavifungulia maximum capacity. Na hajali wengine wanakerwa ama laah!
Si makanisa. Si bar. Si Misikiti. Si wamiliki wa subru na boda boda. Si TRA na matangazo yao!
Hiyo siyo sawa!
Hawa watu wanatakiwa washtakiwe na walipe fedha nyingi sana!
 
Ishu si makelele, then hata ya kanisa wazuiliwe
Kuna watu wanaweka alarm saa 11 waamke nazo zinawapigia kelele pia ata hyo adhana Kuna watu sio waislam lakin inawasaidia kuamka asubuh pia adhana ni dakika 5 ila Kuna watu wanapiga kelele Zaid ya dakika 20
 
Bunge lao lenyewe ni makelele matupu ya kuzomea hoja za maana.

Kwanini MEMC wasiende kulifungia wakati linamzomea Mpina?
 
Huna hoja.
Bar lazima waweke mziki wa juu?
Kama mnataka muziki wajuu jengeni bar nje ya mji pasipo makazi ya raia.

Wananchi pembezoni mwa bar wanateseka sana.
Katika hili niko na serikali
Uzi huu umefungwa kwa comment hii.
 
Huna hoja.
Bar lazima waweke mziki wa juu?
Kama mnataka muziki wajuu jengeni bar nje ya mji pasipo makazi ya raia.

Wananchi pembezoni mwa bar wanateseka sana.
Katika hili niko na serikali
Basi na maspika ya matangazo ya wamachinga yafungwe yanapiga kelele
 
Huna hoja.
Bar lazima waweke mziki wa juu?
Kama mnataka muziki wajuu jengeni bar nje ya mji pasipo makazi ya raia.

Wananchi pembezoni mwa bar wanateseka sana.
Katika hili niko na serikali
Mkuu nakuunga mkono 100%. Mtaani kwetu kuna baa inapiga mziki full blast mpaka saa 11 asubuhi. Kama ni biashara, lakini biashara zao zisiwe kero kwa watu wengine. Wenye kutaka kuendesha baa za mziki mkubwa wajenge kumbi za sound proof.
 
Back
Top Bottom