Nesi aliyempokea Lissu Hospitalini anadai kuwa Antony Mtaka alimtukana 'Fala wewe' na akamuweka mahabusu siku tatu wakati ni Mgonjwa

Nesi aliyempokea Lissu Hospitalini anadai kuwa Antony Mtaka alimtukana 'Fala wewe' na akamuweka mahabusu siku tatu wakati ni Mgonjwa

Tangu 2005 CCM imewahi kuchaguliwa tena au inajichagua yenyewe toka shina lake la NEC? kuwa mkweli wewe ni mkristo na leo ni j2
It's very unfortunately, Tanzania tuna chama kimoja tuu. Chama kwa maana halisi ya chama cha siasa, ni kimoja tuu, the one and only, na kitatawala milele! Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!.
- Je, CCM Itatawala Milele Au?
-https://www.jamiiforums.com/threads/watch-tbc-live-william-malecela-na-ndoto-ya-ccm-kutawala-miaka-50.290455/
Kinachoifanya CCM itawale milele ni kwasababu CCM kutumia Hooks & Crooks Kushinda Chaguzi, Inajua Ikishindwa Ndio Itakufa Jumla, Itakubali? na pia kwasababu CCM sio tu ni chama tawala, bali pia ni chama Dola!
P
 
Ni kweli uongo ukisemwa sana, na kuachwa ukarudiwa rudiwa, hugeuka ukweli, lakini sio uongo wa kijinga!. Dawa ya uongo wa kijinga ni kuupuuzia tuu, utajifia wenyewe!. Mfano shetani kakupitia, ukapita na dada zetu wale wa ile biashara, kisha akataka pesa zaidi na wawe huna, akaamua kukuchafua kwa kusema hujafanyiwa sunna!, vipi wewe ili kukanusha, utafungua zipu kuonyesha kuwa sii kweli?. Vitu vingine vya kujinga mno ni vya kupuuzwa tuu!.
P
Huo mfano hauendani na suala hili kwa kuwa jambo hili linaweza kutihibishwa na kutolewa ufafanuzi bila shida ya aina yoyote ile na ukweli ukafahamika
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimeendelea kuisikiliza video ya muuguzi aliyedai kuwa ni miongoni mwa wauguzi waliompokea Lissu hospitalini siku alipokimbiziwa hapo baada ya kushambuliwa kwa Risasi na watu wasiojulikana 2017.

Ambapo katika mazungumzo hayo na Lissu muuguzi huyo ambaye anadai alishafukuzwa kazi kwa madai ya utoro kazini .anasema kuwa siku ya sheria Dunia mwaka 2022 aliingilia hotuba ya Mheshimiwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hasssan ili aweze kusikilizwa .ambapo hata hivyo muuguzi huyo anadai ya kuwa Rais aliamuru aende kwa wasaidizi wake ili wamchukue maelezo na wao watayawasilisha kwake.

Ambapo baada ya kuwa amekaa kwenye gari pale chini kwa ajili ya kusikilizwa ,anadai kuwa aliitwa mkuu wa mkoa wa Dodoma wa wakati huo Mheshimiwa Antony Mtaka ambaye kwa sasa ni mkuu wa mkoa wa Njombe,ambapo muuguzi huyo anadai ya kuwa baada ya Mheshimiwa Mtaka kuja alimtukana kwa kumwambia FALA WEWE. Ambapo muuguzi huyo anasema akasema yeye siyo fala na kwamba amefanya hivyo kwa kuwa amekuwa hasikilizwi. Anasema akamwambia Mheshimiwa Mtaka kuwa hata wewe utaondoka hapa yaani Dodoma.

Ameendelea kueleza kuwa alitoa maelezo kwa wasaidizi wa Mheshimiwa Rais ambapo anaamini pengine ni katika maelezo yake yale ndio maana Mheshimiwa Mtaka alipewa kama adhabu kwa kupelekwa mkoani Njombe. Ameendelea kusema kuwa Mheshimiwa Mtaka alimuweka central police kwa Amri kwa siku tatu wakati alikuwa anaumwa na kwa muda wote huo hakupewa dawa wala maji na kuendelea kupata maumivu makali sana Mwilini mwake yaliyotokana na kukosa dawa alizokuwa anazitumia kwa wakati huo.

Hoja yangu mimi ni kuwa hoja na tuhuma hii ni nzito sana ,kwa kuwa Mheshimiwa Mtaka amejijengea heshima kubwa sana hapa nchini juu ya utendaji wake ambao umejengwa katika taswira ya uchapa kazi.ambapo amekuwa akipongezwa na kusifiwa na viongozi wengi sana pamoja na wananchi mbalimbali nikiwepo mimi mwenyewe Mwashambwa Lucas mwanachama na kada kindaki ndaki wa CCM.

Kwa sababu inamchafua sana Mh Mtaka hasa kwa namna jina lake lilivyo kubwa miongoni mwa wakuu wa mikoa waliopo hapa nchini. Maana hata leo ukimwambia mtu akutajie wakuu wa mikoa walau watatu tu wachapa kazi ,basi jina la Mh Mtaka lazima litakuwepo. Sasa siamini kama Mheshimiwa Mtaka anaweza kuacha na kushindwa kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kwenda kumsikiliza mwananchi mwenye shida ili apatiwe majibu , na badala yake Mh Mtaka aende kumtukana huyo mwananchi kuwa ni FALA. Jambo ambalo naamini si sahihi kwa sababu hata fala anayo nafasi ya kusikilizwa katika ufala wake. Maana katika ufala wake kunaweza kukawa na maumivu katikati yake yanayohitaji msaada.

Najuwa kuwa kiongozi huwezi ukajibu kila kitu kinachotokea na kuendelea mitandaoni,najuwa siyo kila jambo linaloibuliwa mitandaoni linaweza kuwa la kweli. Lakini katika hili jambo zito la tuhuma tena ambalo lilitolewa maagizo na Mheshimiwa Rais natamani Mheshimiwa Mtaka angelitolea hata majibu kidogo tu hata kupitia mtandao wake wa kijamii kama vile kupitia twitter au njia yoyote ile. japo tamaa yangu siyo lazima kutimizwa au kupata majibu au kujibiwa.maana inategemea na mhusika atakavyojisikia na kulichukulia jambo hili. Maana hata kukaa kimya nako ni jibu na ni haki ya mtu na sehemu ya mbinu za kiuongozi na kuwa kama kiongozi siyo lazima uzungumze kila kitu na kutolea ufafanuzi kwa kila kitu.

Lakini pia suala la kupelekwa Njombe ningependa kusema kuwa ni jambo la kawaida katika utumishi wa umma au uongozi.maana hata Njombe ni sehemu ya Tanzania na ina watanzania wanaohitaji viongozi bora na wachapa kazi ili kuinua mkoa huo. na siyo kwamba ni mkoa wa kutumikia adhabu kwa wenye makosa na wala siyo Magereza ya viongozi waliotenda makosa sehemu nyingine za utumishi wao.. Kwa hiyo hoja ya kupelekwa Njombe siichukulii kama hoja ya msingi au adhabu bali naichukulia kama mabadiliko ya kawaida tu.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mambo ni mengi sana
 
Usiusemee moyo wa mtu,nani alitegemea Rais Samia angeweza kumtukana waziri wake Profesa Mkenda kumuita nonsense tena hadharani. Kuna siku pia aliwatukana wateule wake kuwaita stupid? Usiusemee moya wa mtu. Wewe hukuwepo jee huyo mama akileta ushahidi usiotia shaka kuwa Mtaka aliyasema hayo utauweka wapi uso wako. Wakati mwingine mami unajitafutia aibu ya bure kutetea kila uovu wa makada wa CCM.
Kuna wakati watu wanaacha professional zao na kuweka ushabiki au mahaba mkuu , na vitu kama hivi ndio huwa vinawapunguzia watu heshima.
 
CCM hatujawahi kuunga mkono Vitendo vinavyokiuka na kuvunja haki za binadamu. CCM na wana CCM tunapenda haki nakutaka kuona kila mtanzania akitendewa haki. Ndio maana hata mwenyekiti wetu na Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mama Samia ameendelea kusisitiza na kuvisihi vyombo vya dola kama vile jeshi la polisi kutenda haki kwa watu.
Haki ya Tundu Lissu ya:

1. Kulipwa mafao yake ya ubunge iko wapi? Si ni CCM hawahawa mnaminya haki hiyo?

2. Polisi kuchunguza tukio la kujaribu kumuua kwa risasi mwaka 2017 , kuwakamata na kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wote waliohusika na tukio hilo hiyo haki yake Iko wapi? Si ni CCM nyie wenyewe mnahusika?

3. Kulipiwa gharama zake za matibabu baada ya tukio lile baya na la kishenzi. Je waliokataa si nyie wenyewe CCM kupitia Rais wetu hayati J. P. Magufuli na Spika wa Bunge la CCM Job Ndugai? Unasemaje hapo?

NB: Huu ni mfano tu wa raia mmoja maarufu sana Ndugu Tundu Lissu kunyanyaswa, kuwa brutalized na kisha kunyimwa haki zake na serikali iliyo chini ya CCM.

Sasa kama mnaweza kuutendea mti mkavu uovu mbaya hivi, vipi kwa miti mibichi ndugu Lucas Mwashambwa?
 
Haki ya Tundu Lissu ya:

1. Kulipwa mafao yake ya ubunge iko wapi? Si ni CCM hawahawa mnaminya haki hiyo?

2. Polisi kuchunguza tukio la kujaribu kumuua kwa risasi mwaka 2017 , kuwakamata na kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wote waliohusika na tukio hilo hiyo haki yake Iko wapi? Si ni CCM nyie wenyewe mnahusika?

3. Kulipiwa gharama zake za matibabu baada ya tukio lile baya na la kishenzi. Je waliokataa si nyie wenyewe CCM kupitia Rais wetu hayati J. P. Magufuli na Spika wa Bunge la CCM Job Ndugai? Unasemaje hapo?

NB: Huu ni mfano tu wa raia mmoja maarufu sana Ndugu Tundu Lissu kunyanyaswa, kuwa brutalized na kisha kunyimwa haki zake na serikali iliyo chini ya CCM.

Sasa kama mnaweza kuutendea mti mkavu uovu mbaya hivi, vipi kwa miti mibichi ndugu Lucas Mwashambwa?
Huyo mchuna ngozi hawezi kukuelewa moyo wake umejaa ushetani tupu
 
Back
Top Bottom