N'golo Kante sifa zimemzidi hadi kiburi kinamnyemelea

N'golo Kante sifa zimemzidi hadi kiburi kinamnyemelea

Arsene Wenger;
"Kwa mtazamo nafikiri N'Golo Kante ndiye kiungo bora zaidi kwasasa kwa bara zima la Ulaya. Kuna kitu amekiongeza kwenye soka lake."

"Hapo kabla alikuwa ananyang'anya mipira vizuri na anatoa pasi nzuri, alikuwa ni mchezaji bora sana kwenye kupora mipira. Nasema ni mchezaji bora kwenye kunyang'anya mipira sababu anaweza kuunasa mpira bila kucheza madhambi."

"Lakini kwasasa ana uwezo pia wa kuunasa mpira kisha akakimbia na kwenda kutoa pasi nzuri kwenye eneo la timu pinzani. Na ndiyo maana nasema kwasasa yeye ndiye kiungo aliyekamilika kwenye bara zima la Ulaya."
#d1905_updates
 
Thierry Henry;
"Ni nadra sana kuona mchezaji anafika kabla ya mpira kufika. Kama ambavyo (Kante) amekuwa anafanya, anajua kabisa kwamba mpira utaenda kutua pale."

"Kuna wakati anafika eneo ambalo mpira baadae unafika, huwa nabaki kujiuliza, kwani alijuaje?"

"Ana uwezo wa kuusoma mchezo na kunyang'anya mpira bila kucheza madhambi, na ana uwezo wa kukata mashambulizi yanayosababishwa na timu pinzani."

"Ana uwezo wa kubadilisha shambulizi la hatari linalosababishwa na timu pinzani na kulifanya liwe shambulizi la kushtukiza kwenda kwa timu pinzani."

"Unaweza kutengeneza shambulizi kuwashambulia, lakini anaupora mpira na kusababisha hatari kubws tena dhidi yako.
 
Mzuka wanajamvi!

Nyodo, ngebe, dharau, majigambo, majivuno vinaweza kumpata asipojiangalia.

Ngolo Kante mchezaji wa mpira mstaarabu na muungwana kuliko wote inaonekana sifa zimemjaa hadi utanashati wake uliotukuka kwa mbali unaanza kuingia na doa. Hii ni kutokana na mtazamo wangu.

Siku hizi anacheza rafu sana. Anatembeza ngwala bila huruma hii siyo sawa kwa mchezaji wa kaliba yake.


Pia matanuzi na kujionesha sana mali zake mitandaoni. Asiende kasi sana. Tulimzoea na magari ya kawaida sasa hivi anapiga picha na magari ya ghali na ya ajabu ajabu.


Ajiangalie sana asipoteze focus kwa sifa kedekede anazopata sasa hivi na huenda akawa mchezaji bora wa mwaka duniani na hadhi yake iliyotukuka kushuka.

Licha ya yote namtakia mafanikio mema na tunasuport sana na tunamkubali.

Senior JF Local and International sports analyst and correspondent

Masters

Cc The Icebreaker
Wacha afaidi matunda ya jasho lake. Unateseka ukiwa kidimbwi gani wewe?
 
Thierry Henry;
"Ni nadra sana kuona mchezaji anafika kabla ya mpira kufika. Kama ambavyo (Kante) amekuwa anafanya, anajua kabisa kwamba mpira utaenda kutua pale."

"Kuna wakati anafika eneo ambalo mpira baadae unafika, huwa nabaki kujiuliza, kwani alijuaje?"

"Ana uwezo wa kuusoma mchezo na kunyang'anya mpira bila kucheza madhambi, na ana uwezo wa kukata mashambulizi yanayosababishwa na timu pinzani."

"Ana uwezo wa kubadilisha shambulizi la hatari linalosababishwa na timu pinzani na kulifanya liwe shambulizi la kushtukiza kwenda kwa timu pinzani."

"Unaweza kutengeneza shambulizi kuwashambulia, lakini anaupora mpira na kusababisha hatari kubws tena dhidi yako.
Na hiki ndio alichowafanyia madrid nje ndani na city
 
Thierry Henry;
"Ni nadra sana kuona mchezaji anafika kabla ya mpira kufika. Kama ambavyo (Kante) amekuwa anafanya, anajua kabisa kwamba mpira utaenda kutua pale."

"Kuna wakati anafika eneo ambalo mpira baadae unafika, huwa nabaki kujiuliza, kwani alijuaje?"

"Ana uwezo wa kuusoma mchezo na kunyang'anya mpira bila kucheza madhambi, na ana uwezo wa kukata mashambulizi yanayosababishwa na timu pinzani."

"Ana uwezo wa kubadilisha shambulizi la hatari linalosababishwa na timu pinzani na kulifanya liwe shambulizi la kushtukiza kwenda kwa timu pinzani."

"Unaweza kutengeneza shambulizi kuwashambulia, lakini anaupora mpira na kusababisha hatari kubws tena dhidi yako.
Uchambuzi mzuri sana
 
Kama ushabiki wa Man city au Real Kwanza pole mana huyo kiumbe mnajua alichokuwa anakifanya uwanjani mlipokutana nae.

Kwenye hizo rafu unazosema wewe, jee anakadi nyekundu ngapi?

Hizo picha pia nizamiaka mingi .
naona kweli umeanza mjua kante alipowafanya kitu kibaya kipindi hichi.
Ila huyo ndo kante wa kila kipindi
Kipimo cha rough ni red card sasa kantetele mnyama anakadi ngapi..?
 
Humjui Ngolo Kante tulia

Ngolo Kante aliamua kuiacha Mini Copper yake nyumbani akaamua kuchukua treni wakati akiripoti kambini kwa ajili ya maandalizi ya EURO juzi.

Kwa bahati mbaya treni ilichelewa kwasababu ya hitilafu iliyotokea katika kituo kimoja. Ngolo Kante akachelewa kuripoti kambini.

Alipofika kambini, kikao kilishakwisha na wachezaji walikuwa wanaendelea na mambo mengine.

Alifika kwa kocha Didier Deschamps na kumpa tabasamu kama kawaida yake kisha akamuambia nimecheleweshwa na treni.

Didier Deschamps hakuwa mkali kwake. 'Anajua tu huyu ni Ngolo Kante na hawezi kuchelewa nje ya taratibu kwasababu za kihuni'.

Didier Deschamps alimpa tabasamu na kumuambia, "Lakini Ngolo Kante upo fasta kuliko treni kwanini hukuiacha kisha ukaja mwenyewe??" [emoji1783]. Walicheka wote kisha kesi iliishia hapo.

NGOLO KANTE ALISAMEHEWA KWASABABU NI NGOLO KANTE.
Hahahahahaha
 
Back
Top Bottom