N'golo Kante sifa zimemzidi hadi kiburi kinamnyemelea

N'golo Kante sifa zimemzidi hadi kiburi kinamnyemelea

Mzuka wanajamvi!

Nyodo, ngebe, dharau, majigambo, majivuno vinaweza kumpata asipojiangalia.

Ngolo Kante mchezaji wa mpira mstaarabu na muungwana kuliko wote inaonekana sifa zimemjaa hadi utanashati wake uliotukuka kwa mbali unaanza kuingia na doa. Hii ni kutokana na mtazamo wangu.

Siku hizi anacheza rafu sana. Anatembeza ngwala bila huruma hii siyo sawa kwa mchezaji wa kaliba yake.


Pia matanuzi na kujionesha sana mali zake mitandaoni. Asiende kasi sana. Tulimzoea na magari ya kawaida sasa hivi anapiga picha na magari ya ghali na ya ajabu ajabu.


Ajiangalie sana asipoteze focus kwa sifa kedekede anazopata sasa hivi na huenda akawa mchezaji bora wa mwaka duniani na hadhi yake iliyotukuka kushuka.

Licha ya yote namtakia mafanikio mema na tunasuport sana na tunamkubali.

Senior JF Local and International sports analyst and correspondent

Masters

Unaumia chelsea kubeba Kombe ?? Kafir mbali
 
Acha ujinga Ngolo kante anaenda kutupa kombe jingine ufaransa pale.
 
Humjui Ngolo Kante tulia

Ngolo Kante aliamua kuiacha Mini Copper yake nyumbani akaamua kuchukua treni wakati akiripoti kambini kwa ajili ya maandalizi ya EURO juzi.

Kwa bahati mbaya treni ilichelewa kwasababu ya hitilafu iliyotokea katika kituo kimoja. Ngolo Kante akachelewa kuripoti kambini.

Alipofika kambini, kikao kilishakwisha na wachezaji walikuwa wanaendelea na mambo mengine.

Alifika kwa kocha Didier Deschamps na kumpa tabasamu kama kawaida yake kisha akamuambia nimecheleweshwa na treni.

Didier Deschamps hakuwa mkali kwake. 'Anajua tu huyu ni Ngolo Kante na hawezi kuchelewa nje ya taratibu kwasababu za kihuni'.

Didier Deschamps alimpa tabasamu na kumuambia, "Lakini Ngolo Kante upo fasta kuliko treni kwanini hukuiacha kisha ukaja mwenyewe??" [emoji1783]. Walicheka wote kisha kesi iliishia hapo.

NGOLO KANTE ALISAMEHEWA KWASABABU NI NGOLO KANTE.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Kante ni burudani ya kimyakimya kwenye soka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom