Ngorongoro hali mbaya: Maulid Kitenge ataka hatua za dharura zichukuliwe kuwanusuru Wamasai

Ngorongoro hali mbaya: Maulid Kitenge ataka hatua za dharura zichukuliwe kuwanusuru Wamasai

Wao wanasema wamefika, na wanapigana wasiondoke,hata sie watanzania wenzako tuko nao bega KWa bega ,Kitenge anawashwawashwa nini?masai tribe SIO watu wa anasa hata walioko mjini huwezi jua wanalalaga wapi...
Hujui unachkiongea,baadhi ya hoja zinataka Proffesionals.

Bora saa ingine usome na kupita tu.
 
Wao wanasema wamefika, na wanapigana wasiondoke,hata sie watanzania wenzako tuko nao bega KWa bega ,Kitenge anawashwawashwa nini?masai tribe SIO watu wa anasa hata walioko mjini huwezi jua wanalalaga wapi...
Utalii na mapato yatokanayo mnayapeleka hazina bila kuwafaidisha watunza mazingira asilia na kuwaendeleza.Masai pia anapenda maisha bora kama Mtanzania au binadamu mwingine yeyote.

Hawa wenzetu hawaruhusiwi kulima,kujenga nyumba au kufanya biashara zingine isipokuwa ufugaji.Tija ya mfugaji wa Kiafrika inatokana na wingi wa mifugo,sasa mnashangaa nini?Serikali imewarudishia nini wananchi wa Ngorongoro ili wasiongeze mifugo?

Hata ile posho ya chakula kilichokuwa kinatolewa na serikali sidhani kama bado ipo!

Mliruhusu ujasiriamali wa mahoteli kuwepo ndani ya mamlaka ambapo mazingira yanaharibiwa bila udhibiti kwa hiyo wanyama lazima watoweke.

Lazima Watanzania tukubali kuwa hatupo vizuri kwenye mambo mengi. Mungu katupatia raslimali nyingi lakini tumeshindwa kuzigeuza kuwa fursa.

Nawaza tu!
 
Kupanga ni kuchagua kwa kipato utaliii Ina bidi Wananchi na mifugo wapishe wapishe kwa resettlement plan ya haki, wapewe eneo la pembezoni lenye ecolojia similar lenye mipaka. Wakati wa vijiji 1974 Mwl. Nyerere aliwapeleka baadhi wakazi Kilimanjaro Tanga na Morogoro kuwagawia mashamba. Maamuzi sahihi yafanyike haraka.
You have to weigh the concequences,there shall never be Ngorongoro without Maasais' there.
 
Makamu mwenyekiti wa kituo hicho mwanahabari mkongwe Maulid Kitenge ameyasema hayo kwa niaba MECIRA muda mfupi baada ya kamati tendaji ya taasisi hiyo kutembelea hifadhi hiyo kujionea utalii na maisha ya wananchi husika kuzingatia ukweli kuwa hifadhi ya Ngorongoro ndio hifadhi pekee nchini inayohusisha maisha ya binaadamu, mifugo na wanyama
Huyu si tuliambiwa ni DC? aliitumiaje nafai yake serikalini kushauri hayo anayoyasema nje ya mfumo?
 
Kupanga ni kuchagua kwa kipato utaliii Ina bidi Wananchi na mifugo wapishe wapishe kwa resettlement plan ya haki, wapewe eneo la pembezoni lenye ecolojia similar lenye mipaka. Wakati wa vijiji 1974 Mwl. Nyerere aliwapeleka baadhi wakazi Kilimanjaro Tanga na Morogoro kuwagawia mashamba. Maamuzi sahihi yafanyike haraka.
Naunga mkono hoja.Kwa mwendo huu ndani ya miaka 50 kutakuwa na mbuzi tu hapo mbugani
 
Hasihamishiwe Serengeti...Wahamishiwe mahala salama penye msitu ambapo wataishi na kuboresha maisha yao
Acheni siasa za kipuuzi, za kufifisha UTU wa mwanadamu kwa tamaa zenu za pesa.

Ni wajinga wachache sana wasiojua nini kinafanyika nyuma ya the so called 'uharibifu wa mazingira' unaoripotiwa na huyo Kibaraka Maulid!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binaadamu wana hali mbaya sana kuliko wanyama....wanaotakiwa Kuokolewa sasa ni wamasai si wanyama

Jenga Hoja
Una hoja nzuri, lakini badilisha 'angle' unayotumia.
Usiseme wanaotakiwa kuokolewa ni Wamasai, badala yake sema wanaotakiwa kuokolewa ni Binadamu na mifugo yao.
Ngorongoro ni ya Watanzania wote, siyo ya Wamasai pekee.
Kuidumisha Ngorongoro, kinachotakiwa ni 'Ecological Balance'.
Ngorongoro ni 'unique' duniani, kwa maana ya Binadamu kuishi na Wanyamapori.
Hoja hapa ni kuiokoa Ngorongoro na siyo kuokoa Binadamu.
Hoja ni kuiboresha Ngorongoro ili Binadamu na Wanyamapori waendelee kuishi pamoja.
Viongozi wa MECIRA, Maulidi Kitenge na Oscar Oscar wamefanya kazi nzuri sana ya kutuhabarisha Watanzania ili tupaze sauti zetu kwa lengo la kuitunza Ngorongoro.
Uwekezaji wa Wageni usikubaliwe, lakini pia uwekezaji wa Wakazi wa Ngorongoro udhibitiwe.
Kama ujenzi katika maeneo yaliyopimwa Mijini yanahitaji kupata Kibali cha Ujenzi cha Halmashauri husika, vivyo hivyo, Ujenzi katika Hifadhi ya Ngorongoro unatakiwa udhibitiwe kwa Vibali vya Mamlaka husika.
Ngorongoro ni World Heritage na Watanzania tunalo jukumu kuitunza.
 
Hivi lini mmesikia wamasi wanasema Wana Hali mbaya, Kama kweli Wana Hali mbaya why hawataki kuondoka,

Ni mafisadi yanayotaka jimilikisha mbuga Ili kufanya ujangili, ndo wanakuja na propaganda mfu pitia KWa wamasai ,Ili wakatekeleze ushetan wao
Watanzania wafugaji wana hali mbaya kutokana na kuharibika maeneo ya malisho.
Maeneo ya malisho yanapomalizika, Wafugaji huhamia sehemu nyingine.
Matokeo yake tunasikia migogoro ya Wakulima na Wafugaji.
Kama Wafugaji wasingekuwa na hali mbaya, wasingehamia maeneo mengine.
Kwa hiyo, hoja hapa ni kuboresha Mazingira, ili wasihame.
Ngorongoro ni eneo la kipekee duniani, ambalo haliongezeki ukubwa.
Binadamu wanaongezeka.
Mifugo ya Wafugaji inaongezeka.
Wanyamapori wanaongezeka.
Asiyeona hili kama ni 'time bomb' ni yule asiye na upendo kwa watu na wanyama.
Uanaharakati hautakiwi Ngorongoro.
Kinachotakiwa na mipango thabiti ya kuiokoa Ngorongoro.
Izungumzwe waziwazi ili Watanzania wote tuwe na msimamo mmoja.
Wa kuidumisha Ngorongoro.
 
Hujui unachkiongea,baadhi ya hoja zinataka Proffesionals.

Bora saa ingine usome na kupita tu.
Hizo professionals zenu zinakuja leo 2022, WAKATI mnawaamishia pale professional zilikua mfukon au , professional zenu uchwara ndo zinaalibu Sana taifa
 
Wanataka kuiuza na ngorongoro kama Loliondo? Mbona propaganda za kuwaondoa wamasai zimepamba moto? Naona wanashindwa kufanya ujangili na wamasai wakiwepo wameona waje na propaganda nyepesi. Bahati mbaya project imeshafeli mapema Sana wabuni nyingine.
Kaifelisha nani?
 
You have to weigh the concequences,there shall never be Ngorongoro without Maasais' there.
Sifa ya Ngorongoro ni mchanganyiko wa wanyama na binadamu hiyo ndio brand yake.

Sasa kama wanataka kuiua branda wawaondoe wamasai ili ngoro ngoro iwe mbuga sawa na nyingine.

The good things would have been to put the proper ways of how to conserve the area and not to permanently barn Maasai population in the area.
 
Back
Top Bottom