Nguruwe ni mojawapo kati ya wanyama HAYAWANI?

Nguruwe ni mojawapo kati ya wanyama HAYAWANI?

Mwenyezi Mungu ameahidi kutoa kipigo heavy kwa wala nguruwe ,Tena hasa Hawa wamataifa ,


Isaya 65

1 Watu wasionitaka wanauliza habari zangu; nimeonekana na hao wasionitafuta; naliliambia taifa lisiloitwa kwa jina langu,
2 Nitazameni, nitazameni. Mchana kutwa nimewanyoshea mikono yangu watu walioasi, watu waendao katika njia isiyo njema, wakifuata mawazo yao wenyewe;
3 watu wanikasirishao mbele za uso wangu daima, wakitoa dhabihu katika bustani zao, na kufukiza uvumba juu ya matofali;
4 waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao;
5 watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe; watu hao ni moshi puani mwangu, moto uwakao mchana kutwa.
6 Tazama, neno hili limeandikwa mbele zangu. Sitanyamaza, lakini nitalipa, naam, mimi nitawalipa ujira wao vifuani mwao;
Agano la kale hilo mkuu
 
muhim hakikudhuru we kula tu mkuu,, kwan hujafka china😌
Kule njaa na scarcity ya vyakula imewatoa ufahamu japo Si wote wenye kula u hafu huo.
 
AGANO la kale halikuondolewa ndugu,

Liliboreshwa tu,

Ujasiri wa kula mbwa au panya WANADAMU wanatoa wapi?
Agano la kale ni kama katiba kwenye katiba Kuna vifungu huwa vinabadilishwa lakini katiba inabaki kuwa vile vile kuja kwa Yesu alikuja kubadilisha vifungu vinavyoleta shida kipindi kile watu walikuwa wakitembea umbali mrefu kwenda kuhubiri neno njiani wakawa wanakutana na hao nguruwe lakini ni changamoto kula hao viumbe Mungu akaona ni vyema kuruhusu pia nguruwe kuliwa.
 
Agano la kale ni kama katiba kwenye katiba Kuna vifungu huwa vinabadilishwa lakini katiba inabaki kuwa vile vile kuja kwa Yesu alikuja kubadilisha vifungu vinavyoleta shida kipindi kile watu walikuwa wakitembea umbali mrefu kwenda kuhubiri neno njiani wakawa wanakutana na hao nguruwe lakini ni changamoto kula hao viumbe Mungu akaona ni vyema kuruhusu pia nguruwe kuliwa.
Nguruwe pori?šŸ˜€
 
Salaam, shalom!!

Utafiti mdogo niliofanya unasema, mnyama huyu nguruwe, akizaa watoto, ukichelewa kuwaondoa, aweza kuwala wote pasi huruma,

Kuna wanyama na ndege walioumbwa wakiwa na utindio, aina Fulani ya ukichaa, mbuni akiwa Mmoja wapo,

Ikiwa mnyama huyu KWELI anaangukia kundi la wanyama wasio timamu , ni sahihi kuwatumia Kwa chakula?

Na Kuna uadui Gani kati ya nguruwe na mapepo?

Maana (Luke 8:30-32) nguruwe akaona kuliko kukaliwa na mapepo, akaona Bora ajitose Baharini afe kuliko kumilikiwa na mapepo,

Karibuni šŸ™
Mkuu Rabbon,

Mimi babu yangu ni mchungaji na tangu udogo wangu nilikuwa namuuliza maswali mengi sana ikanifanya nipoteze kabisa kuamini haya masuala.

Nilishawahi ongea nae kuhusu hii kitu, akaniambia unajua mara nyingi shetani huwa anashambulia kitu ambacho una kithamini sana. Akaanza kwa kusema katika mji wa wagerasi ufugaji wa nguruwe ulikuwa ni kwa sehemu kubwa, hivyo watu wa mji ule walithamini nguruwe kuliko mtu yule aliyeishi pangoni akiteswa na mapepo.

Akaniambia hivi sababu shetani alifahamu kwamba watu wa mji huu wanathamini nguruwe kuliko mtu yule anayeteseka hivyo akamuomba Yesu amruhusu kuwaingia nguruwe wale. Akifahamu kwamba moja, nguruwe hawawezi kuogelea hivyo kwa namna yoyoye watazama ziwani.

Mbili, nguruwe watakapozama watu wa mji ule watachukizwa kwa kupoteza kitu ambacho wanakithamini, hivyo watu wa mji wa wagerasi watamfukuza Yesu asiendelee na kazi yake kwa kusababisha uharibifu wa Mali zao.

Na ndicho kilichotokea,
Nikamuuliza kwahiyo unataka kusema shetani alikuwa smart kumshinda yesu kufahamu tricky yake?

Akanijibu shetani alikuwa nyuma na tricky yake ilikuwa ya hovyo. Akasema mtu yule alipotaka kuongozana na yesu akamwambia wewe baki ushuhudie aliyokutendea Mungu, hivyo kupitia mtu yule wengi wangepata kuamini.

Btw, huwa nikiendaga kanisani sikuhiz naenda kumuangalia mwanangu anavyopiga KINANDA.

Kula nguruwe hana madhara yoyote
 
According to TANZANIA IN FIGURES.

Hii ni biashara ambayo soko lake lipo tu na linaongezeka. Kama unataka kufuga fuga, kama unataka kula kula sana.
 

Attachments

  • FDBE26E9-AD1C-4D73-8198-AFBDABA3B896.jpeg
    FDBE26E9-AD1C-4D73-8198-AFBDABA3B896.jpeg
    79.4 KB · Views: 6
Weeeeeeh ngoja nikuibie SIRI binadamu vibonge wote unaowaona wenye matumbo makubwa na mavichwa kama ng'ombe wakifa roho zao zinarudi kama nguruwe!

Inshort kadiri siku zinavyozidi kusonga na ndivyo navyozidi kuamini, kwamba yule mdudu ni binadamu!
Macho ya binadamu
Damu ya binadamu
Figo ya binadamu
Ini la binadamu
Roho ya binadamu mlafi.
 
Back
Top Bottom