Nguvu kubwa imetumika kuwapiga Houth na hakuna kilichobdilika. Vita enzi hizi ni ngumu kushinda

Nguvu kubwa imetumika kuwapiga Houth na hakuna kilichobdilika. Vita enzi hizi ni ngumu kushinda

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Siku ya mwanzo Marekani na Uiengereza walipoanza kushambulia Houth kule Yemen maeneo karibu 85 ya Houth tuliambiwa yamepigwa na picha za moshi ukifuka tukarushiwa.

Kuna watu walijua Houth imeisha lakini siku iliyofuata Yahya Sarea akatoa tangazo kulenga meli nyengine na watu hawakuamini.

Baada ya hapo Marekani kipekee na wakati mwengine Uiengereza anajiunga wameshambulia mara nyingi sana.Rada zote za Houth tuliambiwa zimevunjwa vunjwa.Zaidi ya hivyo droni na makombora ya Houth tukaambiwaa sasa yanawindwa na kuwahiwa kuangamizwa kabla hata hayajarushwa hewani.

Meli na majahazi yanayopeleka silaha kwa Houth kutoka Iran mara kadhaa zimeshikwa na meli hizo kuzamishwa na shehena zake japo mara moja askari wawili wa US walisukumwa majini.

Yote hayo yaliyotokea kumbe si chochote.Houth kila siku wanarusha makombora kwa meli zenye mafungamano na Israel,Marekani na Uiengereza.Matangazo ya Houth hayabaki kuwa ni kampeni na propaganda tu bali yamekuwa yakithibitishwa na mataifa hayo bila kutaja hasara wanazozipata.

Hapo juzi na jana mfululizo meli za Uiengereza za mizigo ya nafaka na mafuta zimerushiwa makombora na kukoswa koswa.Hali hiyo haiyapi mashirika ya meli furaha na uhuru wa kutumia bahari ya red sea.

Mashirika makubwa ya usafirishaji mizigo baharini kama Maersk wamesalimu amri na kusema hawawezi kubahatisha kupita maeneo hayo ya Houth kwa kuamini ulinzi wa Marekani na Uiengereza ambao meli zao zenyewe zikiwemo za kivita haziko salama.

Defiant Houthis claim fresh Red Sea attacks on US, UK ships

 
Ngoja wanyoshwe kidogo...


Cc: Mahondaw

Ugomvi wao wa mwanzo ulikuwa ni Saudia, vita vyao vilkuwa purely vya kidini, dhehebu la Zaydyyah la Kishia, kuuondoa utawala wa kiongozi wa Yemen wakati huo.

Ni ubavu wa pesa ya Iran ndio unaowafanya wapumue, uchumi, wa Yemen ni uko chini mno, ugomvi huu hauwapeleki popote pale, sana sana kuifanya Yemen kuwa duni tu!
 
Ugomvi wao wa mwanzo ulikuwa ni Saudia, vita vyao vilkuwa purely vya kidini, dhehebu la Zaydyyah la Kishia, kuuondoa utawala wa kiongozi wa Yemen wakati huo.

Ni ubavu wa pesa ya Iran ndio unaowafanya wapumue, uchumi, wa Yemen ni uko chini mno, ugomvi huu hauwapeleki popote pale, sana sana kuifanya Yemen kuwa duni tu!
1708160117447.png


Ubavu wa kurusha Maroketi....angalia wananchi wake...80% wanaishi kwa msaada.....Akili za Mwarabu ngumu mno kuzielewa....Sijui ni lipi linalowasukuma.
 
View attachment 2906675

Ubavu wa kurusha Maroketi....angalia wananchi wake...80% wanaishi kwa msaada.....Akili za Mwarabu ngumu mno kuzielewa....Sijui ni lipi linalowasukuma.

In photos: 17 million on the brink of starvation in Yemen​


In recent years, Yemen has become one of the world’s worst humanitarian crises.

Over half of all Yemenis — 17.4 million people — are food insecure, and the number of people facing famine-like levels of hunger is likely to jump to 161,000 by the end of the year.

Food insecurity is most severe in areas of active conflict or in surrounding areas, where humanitarian access is limited by the security situation.
The rate of child malnutrition is one of the highest in the world: 75 per cent of Yemeni children are suffering from acute malnutrition. WFP is supporting 3.3 million children and mothers with nutrition supplements and provides 1.55 million children with daily snacks in school — a vital nutrition boost that also helps them keep studying.

Source: United Nation Sustainable Development Group.
 
Ugomvi wao wa mwanzo ulikuwa ni Saudia, vita vyao vilkuwa purely vya kidini, dhehebu la Zaydyyah la Kishia, kuuondoa utawala wa kiongozi wa Yemen wakati huo.

Ni ubavu wa pesa ya Iran ndio unaowafanya wapumue, uchumi, wa Yemen ni uko chini mno, ugomvi huu hauwapeleki popote pale, sana sana kuifanya Yemen kuwa duni tu!
Yemen ina mafuta na vyanzo vingi vya uchumi.Wakiachwa huru kutumia rasilimali zao hawatakuwa na haja ya kuomba msaada popote.
 
Mkuu Alwaz: Ni aina gani ya vita unapigana......Hilo lazima uliangalie......Kuna aina nyingi ya Vita Mkuu!.
Nimeangalia vita vyote vilivyopiganwa na US katika kipindi cha miaka 60 iliyopita.
Wametumia nguvu kubwa na hawajashinda hata sehemu moja.
Walishindwa Vietnam
Wakashindwa Afghanistan kwa aibu ya kukimbizwa na kuacha silaha nyuma
Wameshindwa Iraq,wameondoka na makambi makubwa ya kijeshi waliyojenga ni mali ya Iraq na huku wale waliobaki wanaporomoshewa maroketi
Wameshindwa kumuondoa Bashar Al asad.Maraisi kadhaa wa Marekani wameondoka yeye bado yupo anadunda
Wameshindwa kubadili chochote Venezuela.Hata mafuta Iran imeweza kufufua visima vya Venezueala na nchi iko kimya.Na kadhalika
Sasa ni zamu ya kushindwa Yemen.
 
Yemen ina mafuta na vyanzo vingi vya uchumi.Wakiachwa huru kutumia rasilimali zao hawatakuwa na haja ya kuomba msaada popote.

Miaka na miaka Yemen ni maskini......Mbona Saudia.....Kuwait haizuliliwi.....au umeijua Yemen leo! Kama kuna mtu au taifa limamzuia hilo ndilo lenye nguvu....! Bila Saudia kuzuiwa ingewamaliza......ona nguvu zo, kama sio upumbuvu...

1708167201411.png
 
so unataka wapigwe kama gaza ndio moyo wako ufurahi? vita sio kitu ya kuletea ushabiki ile ni maisha ya watu sio movie kwamba behind the scene no animal wa killed during the process
 
Back
Top Bottom