Nguvu ya mitandao: Nimeokota handbag yenye pesa kabla vibaka hawajaiwahi na kumrudishia aliyeidondosha kupitia Instagram

Nguvu ya mitandao: Nimeokota handbag yenye pesa kabla vibaka hawajaiwahi na kumrudishia aliyeidondosha kupitia Instagram

Leo hii wakati nimeamka kufanya mazoezi asubuhi, nilikikuta kipochi cha mkononi (hand bag) kwenye njia ambayo huwa nafanya jogging, Nilichunguza mazingira vizuri na nikakifungua, nilikuta noti 132 za elf 10 pamoja na noti nyingine chache, flash, na kitambulisho...
Hongera sana kwa kudumisha utu.

Nishaokota simu ya mtu, nikamrudishia.

Nishapoteza wallet yenye pesa na cards, nikarudishiwa.

Nishaokota wallet ya mtu, nikamrudishia.
 
Kuna siku utapewa kesi ya mauaji au ubakaji ndio utajua hujui,huyo mtu angekuwa kauawa sasa hivi ungekuwa segerea,usirudie ujinga huo
wanaangalia na aina ya mtu mkuu.

Mimi mtumishi wa umma, ninapokea mshahara wangu, nina biashara yangu nimeajiri mtu, n.k siwezi kuwa suspected kirahisi namna hio kwamba nianze kukaba watu ?

Ingekuwa sina ajira, sina shughuli maalum, n.k nisingejisumbua huko kote maana naijua vizuri hii system
 
wanaangalia na aina ya mtu mkuu.

Mimi mtumishi wa umma, ninapokea mshahara wangu, nina biashara yangu nimeajiri mtu, n.k siwezi kuwa suspected kirahisi namna hio kwamba nianze kukaba watu ?

Ingekuwa sina ajira, sina shughuli maalum, n.k nisingejisumbua huko kote maana naijua vizuri hii system
Watunishi wa umma kibao ni matapeli tu,sabaya hakuwa mtumishi wa umma,?maaskari wangapi wanakesi za mauaji kisa mapenzi na kulipa kisasi,uuaji na ubakaji havina cha utumishi wa umma
 
√√•Wema ni akiba, hongera sana kwa moyo huo aice. Mimi nakumbuka mwaka 2014 niliibiwa begi stand ya nyegez na ndani likiwa na vyet vyote kuanzia darasa LA 7 had shahada(llb) nilitafta zaid ya miez 6 bila kupata ikabid nianze process za kutangaza kwenye gazet ndo niende baraza ili nipate vingne.

Nikiwa kwenye hilo zoezi ndo nikapigiwa simu vyet vimeokotwa mkoani mwanza ikumbukwe kwenye ile bahasha ilikuwemo CV ya kuombea kazi kwahyo mmoja kati ya wadhamini wangu ndo alipigiwa simu, ajabu nikuwa walikuwa wanataka million 1 kama fidia wakadai hawakuzipata nguo bali bahasha tu, aiceee kwa ufupi ilibid nitumie tu mtego wa poris kupata vyet vyangu binadam tumebadilika sana roho yan nawatangazia dau LA laki 5 lakin hawataki.

#Hongera sana kwa ubinadamu wako mkuu.
 
√√•Wema ni akiba, hongera sana kwa moyo huo aice. Mimi nakumbuka mwaka 2014 niliibiwa begi stand ya nyegez na ndani likiwa na vyet vyote kuanzia darasa LA 7 had shahada(llb) nilitafta zaid ya miez 6 bila kupata ikabid nianze process za kutangaza kwenye gazet ndo niende baraza ili nipate vingne...
Aseeh!yaani hao hawana utu hata kidogo!

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Leo hii wakati nimeamka kufanya mazoezi asubuhi, nilikikuta kipochi cha mkononi (hand bag) kwenye njia ambayo huwa nafanya jogging, Nilichunguza mazingira vizuri na nikakifungua, nilikuta noti 132 za elf 10 pamoja na noti nyingine chache, flash, na kitambulisho...
Baada ya kumrudishia hiyo wallet alikuelezea mazingira ya hizo wallet kupotea?
 
Tar 30 September nilikuwa na safar ya kia adventure kutoka mafinga hadi mufindi ndani huko. Nimefika misistu ya sao hill upande wa mtili (kwa wenyeji wanapajua) basi nikaona kisimu fulani kidogo cha batani pembeni ya barabara kimekwanguka kidogo kwa juu ila kiko on na missed call kadhaa basi nikajua ya kuwa kuna mtu kaangusha. Huyo nikakicheki hakina pasword na inaonesha ni cha mtu fulani mzito zito huyo nikakiweka mfukoni nikaendelea kupiga peda.

Lengo langu lilikuwa ni kuwa makini na sura za watu naopishana nao njiani ili ninga'amue lbda watakuwa wanatafuta simu ili niwahoji na kuwapatia.

Nikafika home salama mara nakuta mtu anapiga kwa ile kisimu nikapokea haraka nikajitambulisha kwamba niliyepokea si mimi ndiye mmiliki ila nakuomba kama unajuana na watu wengine wa karibu na mmiliki wa hii simu basi wampe taarifa mwnye nayo ili tuwasiliane.

Si muda mrefu nikaona katika ile simu jina la 'my wife' ndio linapiga basi nikajua hii simu ni ya mwanaume mtu mzima akanambia oh mume wangu alikuwa anatoka mafinga na pikipiki kaangusha simu. Nikasema naomba niongee naye.

Nikampanga na kumhoji vzr nikajihakikishakia. Akanambia yuko sawala ila anakuja na pikipiki hadi kijiji nilipofikia. Kweli baada ya kufika akanipigia kwa ile ile simu niliyoiokota tukakutana kibao cha shule ya msingi. Kumbe kaja na mkewe.

Awali nilipanga nimpe simu afu niishie nisiwe na mastory mengi lkn mkewe akawa anataka anipe hela nikagoma katakata.

Jamaa akaikagua baada ya kuambia ya kuwa acheki kama kila kitu kiko sawa. Akasema kiko sawa. Huyoo nikawapa kisogo.
 
Aseeh!yaani hao hawana utu hata kidogo!

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
#reymage..ilibidi niludi mwanza nikawaambia waje bar moja IPO buzuruga waje na hivyo vyeti niwape hiyo pesa, walikuwa bint mmoja na msera mmoja nikawaambia waagize vinywaji, wakaagiza bas wakanipa hiyo bahasha nikakagua nikakuta vyeti vyote vimo, basi yule askar alivaa kiraia akawaambia wao ndo watakuwa na begi pia LA nguo aiceee waliondoka bila kumalizia vinywaj ikabid nimwambie aachane nao tu yamkin nmepata vyet bas nguo ntatafta zingne. Wala pesa sikuwapa
 
Umejenga msingi mzuri wa kuwaliza watu jf pindi utakapokuja na biashara ya tuma nikutumie mzigo.
Watu mnaona mbaaali saaana

Eti mi mtumishi, siyapo matumishi majambazi tuu?

Eti una biashara, siwapo majizi tui

Mshahara si kigezo mkuu

Hongera yake
 
#reymage..ilibidi niludi mwanza nikawaambia waje bar moja IPO buzuruga waje na hivyo vyeti niwape hiyo pesa, walikuwa bint mmoja na msera mmoja nikawaambia waagize vinywaji, wakaagiza bas wakanipa hiyo bahasha nikakagua nikakuta vyeti vyote vimo, basi yule askar alivaa kiraia akawaambia wao ndo watakuwa na begi pia LA nguo aiceee waliondoka bila kumalizia vinywaj ikabid nimwambie aachane nao tu yamkin nmepata vyet bas nguo ntatafta zingne. Wala pesa sikuwapa
Yaani walikosa utu kabisaa...walishindwa kufanya wema kabisaa mpk kwa malipo!daahh!bora uliwakomesha hvyo maana walileta tamaa

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom