Nguvu za kioo na miujiza yake: Wale wenye imani zenu njooni hapa

Ukitaka kujua nguvu ya kioo na maajabu yake mpe mtoto ambaye hajamaliza hata mwaka mmoja

Na haitatokea kamwe ukayajua yote ya Dunia hadi unaingia kaburini. Dunia Ina mambo mengi yenye kuonekana na yasiyoonekana kwa macho. Endelea kujifunza.
Kweli nilimpoteza mwanangu kwa hili.
Alikuwa akiona mengi sana.
 
Soma Dr From Lhasa,chapter 6 Clairvoyance.
 
Kwenye nyumba zenye msiba mara nyingi vioo vinafunikwa na nguo? Hii ni kwa sababu gani? Au nyumba ambazo hazikaliwi na kuna furniture ndani yake vioo pia hufunikwa.

Kuna duaa ya kujiangalia kwenye kioo katika uislam (Ewe Mola kama ulivyoyapendezesha maumbile yangu-kuwa mzuri...basi Vipendezeshe na vitendo vyangu pia)
 
I second you mkuu. Huu upuuzi wa mambo ya kufikirika unafanya wazungu watutukane waafrika na kuona tuna ulemavu wa kufikiri.

Wakati wenzetu wanachanja mbuga kwenye teknolojia na artificial intelligence sisi tunawaza kioo. Yaani babu zetu waliporwa dhahabu kwa kubadilishana na kioo na sisi tulivyo wajinga tunajadili upumbavu mpaka leo.

Ndio maana wajasiriamali wa imani za uponyaji na miujiza ya mafanikio bila kufanya kazi wanawapiga mbumbumbu kwa akili hizi.
 
Sikuwahi kujua juu ya kioo ila mimi huwa kuna roho inaniambia usiku nifunike vioo popote napokuwa kabla sijalala nikiona kioo kimefunuliwa mi najikuta tu nimeshafunika sielewi huwa ni kitu gani kinanisukuma kufanya hivyo
 
Sikuwahi kujua juu ya kioo ila mimi huwa kuna roho inaniambia usiku nifunike vioo popote napokuwa kabla sijalala nikiona kioo kimefunuliwa mi najikuta tu nimeshafunika sielewi huwa ni kitu gani kinanisukuma kufanya hivyo
Vile vya kubandikwa ukutani unavifanyeje mkuu?
 
Nimekuelewa mkuu Hongera[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Mm nlipata demu mneithaland pale nairobi demu ukitaka mdanganya anakwambia kaangalie kioo ukithubutu anakwambia kama uko home au uko baa au unachepuka .nkasema cha kufia nn nkapiga chini
 
sijaelewa hapa.
aliyeelewa anieleweshe
 
Unaambiwa kioo ikikiweka kwenye beseni lenye maji ukajitazama unaweza kugundua kama unaumwa ama la.

Unaambiwa ukitaka ndoa yako idumu, mara baada ya kufunga mkajiangalie kwenye kioo kwa maana nafsi zetu zitabaki kuwa milele, ndoa itadumu milele.

Wakati mwingine tunaota manyoka nyoka tukiwa tumelala ni kwasababu tunamakabati yenye vioo chumbani mwetu. Tukilala nafsi zinatoka, zinaenda kutalii, sasa ikitoka inakutana na kioo. Ni shida.

Miaka mingi iliyopita mtu aliuwawa pasipo haki, kwa dhuluma, kabla ya mazishi vioo vitawekwa kila mahali kwenye chumba chake ndani ya siku tatu..baada ya hapo atazikwa. Ile roho yake itabaki kwenye kioo italipa kisasi kwa wabaya wake wote.

Nasikia pia eti hata mtu alikataa roho kama kuna kioo kipo karibu basi kitavunjika.

Shaloom

COPY N PASTE..
 
Hapa sijui kama Dr Mshana alipita
 
Ukitaka kujua nguvu ya kioo na maajabu yake mpe mtoto ambaye hajamaliza hata mwaka mmoja

Na haitatokea kamwe ukayajua yote ya Dunia hadi unaingia kaburini. Dunia Ina mambo mengi yenye kuonekana na yasiyoonekana kwa macho. Endelea kujifunza.
Kuna vindege huwa vikijiona kwenye kioo cha dirisha au gari huwa vinapambana kweli ili vimfikie yule reflects wake. Kanagonga dirisha balaa
 
Thomaso kama thomaso apa bado cjaamini kitu kwaiyo vioo vya makabati itakuaje
 
Wewe unazungumza kuhusu claivoyance. Kioo kinachongumziwa siyo kioo cha bafuni. Kioo cha clairvoyance ni CURVED mirror,kama kifuniko cha taa ya gari au taa ya pikipiki.
Kioo hiki unakipaka rangi cheusi upande mmoja,halafu unakitazama ndani.
Kioo hiki kinaitwa Black Mirror.
Pia juzi nilikwenda Mererani. Kuna kitu kule kinaitwa crystal,neno ambalo linatajwatajwa sana watu wanapoongea kuhusu claivoyance.
Bado najitahidi kuipata hii crystal.
 
Duh!!,Dunia haiishi ya kujifunza.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…