Ni aibu gani uliipata kwenye Interview yako ya Kwanza? Mimi yangu hii

Da nimecheka sana [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Aibu ambayo mimi nimeipata katika interview ni suala la kuabudu....

Picha linaanza kuna mtu kanipa connection ya kufundisha shule fulani ya Dini, nikapeleka CV zangu pale mimi huyo nikapotea kurudi zangu Mkoa baada ya kuona miezi inapita siitwi kwenye Interview ,

Hatimaye miezi kadhaa mbele nikaitwa nikafunga safari hadi jiji la Dar,
nikapewa ile Written Interview then nikapiga ile Oral,

Kimbembe kilianza pale muda wa kuabudu umefika na watu wote ambao walikuwapo pale wakatawanyika wamekwenda kujiaanda kwa ajili ya ibada,
mimi nimekaa mtaani kipindi hicho takribani miaka mitatu baada ya kutoka chuo so mazingira ya mtaani nimeadopt ile mbaya hadi kuabudu imekuwa shida,
Baada ya ibada msaili mmoja akaniuliza mbona haujafanya ibada? Nikajikaza kwa kumwambia niko vibaya naumwa,
Aisee nilijiona dhaifu na aibu kubwa juu yangu hatimaye sikuchaguliwa nikahisi hili la kuabudu limechangia...Basi nilikaa mjini takribani wiki 1 nikarudi zangu Kijijini,

Now Employed.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kitendo cha kukaa kimya unadondosha marks so jibu kwa kujiamini hata kama ni pumba
Aisee, Mwaka huu wote nime u dedicate katika kutafuta Ajira maana ni fresh Graduate (Accounts) Napitia nyuzi za Interview kupata Kauzoefu kidogo. Najiuliza sana maswali endapo nitaulizwa jambo geni na endapo sina idea kabisa itakuaje. Kama wanauliza kupima uelewa aisee Hawatanisahau maana Niko Vzr sana, Ila kama wanauliza Terms ngumu ngumu nahisi naweza nikateleza sehemu
 
Be honest waambie kitu kama hukijui kuwa sijui but nitakifuatilia na kujifunza.
Kuna maswali huwa yanaulizwa wakijua huna majibu kukupima how trustful your are wala
nia sia kulipata swali.
 
Hivi Kwenye Interview kama hujui Swali inakuaje? I mean Kama huna idea kabisa, Unawaambia hujui au Unawaambia waulize jingine?
Huwezi kukosa idea labda kama hujaelewa hamna swali unaweza usitambue labda kamaanisha nn yaani msamiati hujui kwa kingereza ila ukiwa na ukiactivate moody kwamba niko kwenye interview kila swali utajibu kama umeelewa tu utapiga mule mule

Except kwa maswali ambayo yako strictly na majibu yako constant mfano kama hujasoma job duties and responsibilities kama zilivyo kweny tangazo la ajira kutunga utapata tabu sana
 
Mi nakumbuka nafanya interview nilikuta watu wana summary za kusomea na ni oral nimeenda rafu wanaonijua walikuwa wengi wakawa wanacheka tu mi nikajitenga walikuwa wanaitoa kwenye mood kichwani ninajua job duties and respobilities tu hapo sijui hata nikiambiwa tell is about yourself ntasemaje, mambo kibao sijui what are the interest facts about you

Tukaambiwa tukale kwanza baada ya kutambulishwa kwenye panel list kimekaa na watu wanafanya rehearsal kabisa hapo pembeni wanaulizna niliona wanaboa chai sijamliza nikaondoka watu wanapractise mpaka jinsi ya kutembea Dah

Nikapewa namba nilikuwa wa 6 nilipoingia tu nilijibu yote mzee natak kutoka nikaambia tell us eaxctly what you are going to do once you employed in the corporation as you area specialization" nikasema hapa ndio naongezea sauti ndo zile job duties and responsibilities wakasema five things nikataja mpaka tatu nikaambiwa gud nikatoka
 
Ulifanikiwa kupata kazi hapo?
 
Huko kuwa uko vizuri au hauko vizuri utakujua baada ya kuwa kwenye interview room 🤣 🤣
 
Ulikua 2019 niliitwa kwenye usaili wa ualimu. Tulipiga written fresh, ikaja practical nikaingia kupiga pindi. Ile shule ni private na wanafunzi wanaumri mkubwa kidogo na wanavaa sare nyeusi chini juu nyeupe.

Miongoni mwa waliokuwepo darasani kumbe alikuwemo mkuu wa shule sikujua maana umri wake Kama wanafunzi tu. Sasa wakati napigisha pindi na msaili anasimamia nikampoint mkuu ajibu swali.

Wanafunzi wakawa wanashangaa,jamaa akajibu swali wakampigia makofi nikahitimisha pindi. Yaliyojiri sinahaja ya kusimulia wote mnajua.
 
Be honest waambie kitu kama hukijui kuwa sijui but nitakifuatilia na kujifunza.
Kuna maswali huwa yanaulizwa wakijua huna majibu kukupima how trustful your are wala
nia sia kulipata swali.
Hapa nimekupata Mkuu, Umeelezea Vizuri sana, Naimani ntajibu kadri ya uwezo na Uwelewa wangu
 
Huko kuwa uko vizuri au hauko vizuri utakujua baada ya kuwa kwenye interview room [emoji1787] [emoji1787]
[emoji23][emoji23] Mkuu ww ulishawahi kuingia kwenye chumba Cha Interview? Hebu tupe Experience yako
 
Hapo sawa mkuu nimekupata Vyema, Na vipi kuhusu Lugha unachagua au wanakuchagulia? Na Je ni Lugha ipi inafaa kutumia kati ya kiswahili au Kiingereza? Maana tunajua Kiswahili Huwa kina Maneno magumu sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…