Ni aibu kwa taifa letu kumuona Prof Abdulrazak Gurnah kama shujaa wa taifa letu, wakati huko nyuma hajawahi kutambuliwa kwa kazi alizofanya

Naunga mkono hoja.

Nilipomsikia nikadhani ni yule rapper accomplice wa Lil baby anaeitwa Gunna.

Completely dishonest with this writer hajawahi kutumia hela ya bodi ya mikopo, hazina wala hakuna aliyemsomesha lakini leo watu wanataka credit. Oddafrica.
 
Hayo yote ni madhara ya kuendelea kuwa na katiba iliyopitwa na wakati.

Tukudai katiba mpya muwe mnatuelewa basi kabla ya kutuona kuwa sisi ni wapinzani.
Mkuu tatizo sio kuwa na katiba mpya sasa, tatizo ni hao wanaoaminiwa kusimamia matakwa ya katiba. Wengi ni wanafiki na wabinfsi tu.

Kama hawawezi kutekeleza kikamilifu yaliyomo kwenye katiba hii ya sasa hata ikiandikwa mpya kwa wino wa dhahabu bado haitasaidia kitu.
 
Ukweli mtupu.
 
Kwani Ni jukumu la Nani kum aknowlegde mchango wake...hata wewe ungeweza kum aknowlegde inaruhusiwa
Tena ukizingatia watanzania wengi hatupendi kusoma vitabu ilikuwa ni ngumu sana kumjua kirahisi kama ilivyo kwa diamond platnumz[emoji1787][emoji23] yeye aliyekuwa anamjua angeanza mapema sana kumtambulishi kwenye jamii yake.
 
Kwani umesahau kwamba tuna kwaya yetu ya praise and worship
 
Kama umezaliwa Tz na asili yako ni taifa lingine huthaminiwi kama mzawa bali eti mhamiaji

Hii ni kwa ajili ya mfumo wetu na raia tunafuata mkumbo wa serikali
Mataifa mengine serikali zao zinawavutia wote waliozaliwa haijalishi ana asili ya wapi na wanaingia mpaka sehemu nyeti bila tatizo

Serikali ibadilike
 
Tunahitaji katiba mpya hayo maelezo ni muendelezo wa watawala wanao ogopa katiba mpya.
 
Sio kweli kwamba alienda kama mkimbizi. Huyu aliondoka Zanzibar 1960 - kwa mujibu wa DW. Wakati huo hakukuwa na sababu ya ukimbizi.
Aliondoka late 1960's! Jana nilihoji ikiwa by the late 1960's, kulikuwa na security risk kwa kijana mdogo ambae hakuwa mwanasiasa. I know by that time, vijana wengine kama akina SAS walikuwa kwenye hiyo risk na ndo maana Mwalimu akamtupa ubalozini!

Conclusion yangu, Mwamba alitumia janja ile ile ya Watanzania na kwingineko Afrika... kwamba unazamia mbele kwa gia ya ukimbizi na Wazanzibari wanatumia sana hii mbinu,!!

Mwaka juz Makonda alipoanza ku-deal na mashoga, nilipata issue za Wazanzibari wawili walioingia Marekani kwa hoja kwamba maisha yao yapo hatarini kwa sababu ya wao kuwa mashoga. Na hapa ninapoongea, jamaa wote wawili wanakula pesa ya Joe Biden Unyamwezini!

All in all, hadi kesho, pamoja na kuchimba sana lakini sijaona popote ambapo Abdulrazak Gurnah kutajwa kama Mwingereza. Sources zote zinamtaja kama Mtanzania au Zanzibar-born based in UK!

Na lingine ambalo watu hawalifahamu ni kwamba, sio kwamba jamaa baada ya kutoka ZNZ hakuwahi kurudi tena bali back 1984, ndipo kwa mara ya kwanza alirudi ZNZ tangu alipoondoka!!

Tukija kwa mleta mada.... hili jambo linakuzwa sana! Hivi hao akina Samia hata wakisema "alisoma kwa kodi zetu" kwani Wabongo mnapungikiwa nini? Mbona tunapend kujihangaisha na mambo madogo madogo sana?!!

Lakini kwa upande mwingine, asikudanganye... Nobel Prize ni tuzo inayoheshimika sana duniani na ndo maana media kubwa karibu zote duniani, zimeruka na hii issue zaidi ya mara moja!!

]Kwahiyo sioni tatizo lolote akina SSH wakiteleza na ganda la ndizi... that's how the world work! Au mnataka Wakenya waanze kusema jamaa ni Mzaliwa wa Lamu, na alienda mbele akitokea Mombasa? You know they're good at it....
 
Hii
Hii nimeiona na ya DW nimeiona. Kwa mujibu wa sheria ya uraia ya Tanzania 1995 mtu yeyote aliyekuwa raia wa Tanganyika au Zanzibar kabla au siku ya tarehe 26 April 1964 huyo ni Mtanzania ikiwa uraia wake haujapotea kwa mujibu wa sheria. Ikiwa Gurnah hajaukana Utanzania au ukawa umeondoka kisheria basi yeye Bado ni Mtanzania.
 
Hili nimelisema sana kwamba kwa mujibu wa sheria ya uraia ya Tanzania 1995 Gurnah ni Mtanzania maadam uraia huo haujaondoka kisheria.
 
Ishu iliopo hapo ni Raia wa Tanzania au hana asili ya Tanzania visiwani .
Then katiba yetu hairuusu uraia pacha
 
Sio kweli kwamba alienda kama mkimbizi. Huyu aliondoka Zanzibar 1960 - kwa mujibu wa DW. Wakati huo hakukuwa na sababu ya ukimbizi.
Soma historia yake vizuri, ni kati ya waliokimbia wakati wa mapinduzi. Alikuwa upande sultani.
 
Tunahitaji katiba mpya hayo maelezo ni muendelezo wa watawala wanao ogopa katiba mpya.
Ajabu... Sasa hiyo katiba utaipata kwa lazima kama watawala wa sasa hawaoni umuhimu?.😳
 
Soma historia yake vizuri, ni kati ya waliokimbia wakati wa mapinduzi. Alikuwa upande sultani.
Kwa usahihi ni 1968 ndio aliondoka ila wana generalise kwa kuandika 1960s
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…