Ni baraka kwa introvert kujifahamu kuwa ni introvert na kuamua kuutumia uintrovert wake kwa manufaa!

Ni baraka kwa introvert kujifahamu kuwa ni introvert na kuamua kuutumia uintrovert wake kwa manufaa!

Uwe na kifua cha kuvumilia neno "ubinafsi" .Introvert ina tafsiri ya ubinafsi, sana kama upo kwenye Community (sio kweny society)
Sidhani kama introverts ni wabinafsi. Mimi watu wengi wananiambia nina sifa za introverts na nimekuwa nikitoa sehemu ya resources zangu kwa wengine hasa wahitaji including muda. Hii pia imekuwa ni kitu ambacho nakifurahia
 
Magonjwa ya kizungu hayo
Magonjwa ya Kizungu? Basi Wazungu wana bahati sana!

~ Wakati magonjwa ya Kiafrika kama kipindupindu yakihatarisha uhai wa Waafrika, magonjwa yao yaitwayo INTROVERT yanawafikirisha na kuibuka na chanjo kwa ajili ya watu wao.

~ Wakati magonjwa ya Kiafrika kama Malaria yakiwarudisha Waafrika nyuma kimaendeleo, magonjwa ya Wazungu yaitwayo INTROVERT yanawasaidia kusonga mbele kupitia ubunifu wa Kisayansi na Kiteknolojia.

Wazungu wana bahati sana! Ugonjwa wao wa introvert umewazalia watu ambao wamekuwa na manufaa makubwa kwa Mataifa yao: Barack Obama, Vladmir Putin, Thomas Edison, Abraham Lincoln, Warren Buffett, Hillary Clinton, Elon Musk, n.k.
 
Introvert wa JF mpoo! Unafahamu thamani ya uintrovert wako?

Kuwa introvert si ugonjwa. Nibaraka, lakini ukijitambua na kujikubali. Vinginevyo, unaweza ukawa sawa na mtu anayetaka kubadilishana kilo kumi za dhahabu kwa kuku kumi wa mayai! Hasara iliyoje!

Jamii yetu, kwa kutokufahamu, wamekuwa wakiwalaumu introvert kwa kutokuwa extrovert. Kuna wanaofikiria wana viburi,, wengine wanafikiri ni waoga, wengine wanawaona kama ni watu wanaojisikia, n.k. Hawajui kuwa wao ndiyo "wajinga", kwa kushindwa kujua utofauti wa maintrovert an extrovert.

Mungu, kwa nia njema kabisa, kaona vyema watu wawe na "personality" tofauti. Wewe unafikiri ingekuwaje kama dunia nzima ingekuwa ni ya maextrovert pekee? Au unafikiri ingekuwaje kama watu wote wangekuwa ni maintrovert?

Kama ambavyo Mungu kaamua kututofautisha, tuzikubali hizo tofauti na tuzitumie kwa manufaa. Wazazi wenye watoto maintrovert waache kuwalazamisha kuwa extrovert, badala yake wawasaidie kuvuna manufaa ya kuwa introvert.

Kwa wasiofahamu, kuwa introvert si ugonjwa. Ni namna ubongo unavyochakata taarifa zinazotumwa kwake. Kwamba, kiwango cha "dopamine" na muundo wa "dopamine receptors" kwenye ubongo ndiyo humtofautisha Introvert na Extrovert.

Tafiti za Kisayansi zinaonesha kuwa mtu anaweza kubainika kama ni introvert au extrovert akiwa na umri wa kuanzia miezi minne.

Kwa wasiojua, hizi ni baadhi ya tabia za Introverts:

~ Wakiamya

~ Wanapenda mazingira ya kuwa peke yao - hawafurahii mazingira ya mchanganyikeni

~ Wanapenda mazingira ya ukimya

~ Hufikiri kabla ya kuongea

~ Wana kawaida ya kuwa na marafiki wachache

~ Ni wasiri sana, n.k. (wengine wataongezea).

Baadhi ya watu maarufu ambao ni Introverts:
1. Warren Buffett
2. Mark Zuckerberg
3. Bill Gates
4. Steve Wozniak
5. Larry Page
6. Michael Jordan
7. Elon Musk
8. Charles Darwin
9. Mahtma Gandhi
10. Al Gore
11. Sir Isaac Newton
12. Rosa Parks
13. Eleanor Roosevelt
14. Abraham Lincoln
15. Barack Obama
16. Marissa Mayer
17. Guy Kuwasaki
18. Hilary Clinton
19.Michael Jackson
20. Brenda Barnes, e.t.c.

Nafikiri, na hawa Watanzania nao ni introvert: Dr. Mohammed Gharib Bilal, Dr. Ally Mohammed Shein, Dr. Philip Mpango, n.k.

Introvert, umebarikiwa kuwa introvert! Usitamani kuwa extrovert!

Extrovert, hakuna hasara kuwa Extrovert! Usiigize kuwa introvert!

Kila mmoja akae kwenye nafasi yake!!!
Elon hpn kwa Kweli tajiri yule anaropoka ropoka snaa kila dkika 5 anatwit no siyo
 
Introvet raha sana. Unapiga zako gambe unatulia. Pia unapata muda wa kuwazua mambo, siku hizi nimejifunza kitu nikiwa na jambo gumu nalipa muda nakaa ata siku tatu silifikirii.

Kumbe akili inaliwazua bila mimi kujua mwisho wa siku nashangaa nakuja na solution ya ajabu sana kila mtu anabaki mdomo wazi.

Napenda usiri japo siku hizi nimeiba tabia za extrovet najichanganya na kusalimia kila mtu maeneo ya kazi but baada ya hapo napotea kujichimbia kwa computer. Kuna muda nahisi siko introvet 100%. Sababu pia naweza kudanganya sana ila kwa kutumia akili, natabia ya wasiwasi sipendi kuacha alama kwenye harakati zangu.

Napenda kutumia majina bandia sitaki mtu ajue jina langu halisi na hii ni tokea nikiwa sekondari mpaka sasa wanaojua jina langu halisi ni wachache. Miaka ya hivi karibuni ndio nimeanza tena kutumia jina langu halisi baada ya kuhama mazingira. Inshort kila mtaa niliokaa nilitumia jina tofauti.....NB: SIJAWAHI KUTAPELI WALA KUIBA CHA MTU ILIKUWA NASIKIA FURAHA TU KUWA MTU BANDIA

Nakipaji cha kuandika na kuchakata maneno, naweza kusoma matamshi ya sauti ya mtu na kujua hatua itakayofuata. Naweza kuonana na mtu kwa dakika chache nikaandika historia yake kwa usahihi 70% na kuweza kubashiri kesho yake kwa 60%.
Naona uanttauta watu wake pm Kwamba wee Ni mtabiri
 
Hebu zitaje baadhi, hasa zile zinazokukera. Huenda kuna mtu atakushauri cha kufanya ili kuzigeuza kuwa "mtaji"

Chochote ambacho hakifahamiki sababu ya uwepo wake, kinaweza kutumiwa ndivyo sivyo.

Ndivyo ilivyo kwa introvert wasiojijua, wanateswa na ambacho kilipaswa kuwasaidia.
Mtu wa hivi hata kwenye Misiba au Harusi au Shughuli tu za wanaomuhusu kama ndugu au marafiki utakuta anakwepa. Atachanga vizuri tu kama ni harusi lakin ikija kadi anagawa.
 
Mtu wa hivi hata kwenye Misiba au Harusi au Shughuli tu za wanaomuhusu kama ndugu au marafiki utakuta anakwepa. Atachanga vizuri tu kama ni harusi lakin ikija kadi anagawa.
Na ukiona amekuja kwenye sherehe yako, ujue ni kwa sababu amekuheshimu tu. Hana "time" na sherehe yako. Ungemwomba akuchangie tu lakini asihudhurie, angeweza kukuongezea na hela ya ziada ya "asante" kwa kutokumsumbua.
 
V
Vitu vingine tuwaachie wazungu, asili yetu ni kujichanganya hao wanaoiga uzungu wanajipa stress bure tu.
Chura anaweza kuishi majini na nchi kavu, lakini kuna mazingira anayoyapendelea zaidi kati ya hayo mawili.

Mamba anaweza kupambana hata akiwa nchi kavu, lakini akiwa majini anakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kushinda.

Ndivyo ilivyo kwa introvert. Yeye si anti - social, bali anafurahia zaidi mazingira fulani yaliyo kinyume na yale ya extrovert.

Kama ni mazungumzo ya kupiga tu stori, anapenda kufanya na mtu aliyezoeana naye, tuseme, rafiki yake wa karibu.

Iko hivi! "Chaji" ya introvert inakuwa ipo full muda wote, wakati extrovert inakuwa na nafasi inayohitaji kujazwa na "makelele", n.k.

Hiyo ndiyo inayomfanya extrovert apende "kuzurura"! Anapokutana na watu na mazingira ya kelele kunalisaidia "tenki" lake kujaa.
 
Hata mm kwa huyo nimeshangaa jamaa ana maneno mengi sana huyo kila leo na tweet zake za utata utata
Kwanza, ninakiri kuwa simfahamu Elon Mask, zaidi ya kumsoma google, n.k.

Mitandao yangu pendwa ni JAMII FORUM na QUORA. Twitter, Facebook n.k. simo, kwa hiyo sijui anachopost Musk.

Lakini kwa mujibu wa wanaoifahamu, yeye mwenyewe akiwemo, wanasema ni INTROVERT!

Kuna wakati alishawahi kusema kati ya mambo ambayo huwa anafanya tu kwa kuwa inamlazimu, ni kuongea mbele za watu. Hayupo comfortable katika hilo.

Suala la yeye kupost twitter hakumuondolei uintrovert. Labda tu ujue kuwa kati ya eneo ambalo maintrovert wanalimudu sana ni kuwasiliana kwa njia ya maandishi. Hata vitabu vingi vinavyouzwa sana waandishi wake wengi ni Introvert.

Introvert ni hodari wa kuandika, lakini hapendi kuongea sana.
 
Hata mm kwa huyo nimeshangaa jamaa ana maneno mengi sana huyo kila leo na tweet zake za utata utata
Kwanza, ninakiri kuwa simfahamu Elon Mask, zaidi ya kumsoma google, n.k.

Mitandao yangu pendwa ni JAMII FORUM na QUORA. Twitter, Facebook n.k. simo, kwa hiyo sijui anachopost Musk.

Lakini kwa mujibu wa wanaomfahamu, yeye mwenyewe akiwemo, wanasema ni INTROVERT!

Kuna wakati alishawahi kusema kati ya mambo ambayo huwa anafanya tu kwa kuwa inamlazimu, ni kuongea mbele za watu. Hayupo comfortable katika hilo.

Suala la yeye kupost twitter hakumuondolei uintrovert. Labda tu ujue kuwa kati ya eneo ambalo maintrovert wanalimudu sana ni kuwasiliana kwa njia ya maandishi. Hata vitabu vingi vinavyouzwa sana waandishi wake wengi ni Introvert.
 
Kwanza, ninakiri kuwa simfahamu Elon Mask, zaidi ya kumsoma google, n.k.

Mitandao yangu pendwa ni JAMII FORUM na QUORA. Twitter, Facebook n.k. simo, kwa hiyo sijui anachopost Musk.

Lakini kwa mujibu wa wanaoifahamu, yeye mwenyewe akiwemo, wanasema ni INTROVERT!

Kuna wakati alishawahi kusema kati ya mambo ambayo huwa anafanya tu kwa kuwa inamlazimu, ni kuongea mbele za watu. Hayupo comfortable katika hilo.

Suala la yeye kupost twitter hakumuondolei uintrovert. Labda tu ujue kuwa kati ya eneo ambalo maintrovert wanalimudu sana ni kuwasiliana kwa njia ya maandishi. Hata vitabu vingi vinavyouzwa sana waandishi wake wengi ni Introvert.
Unaweza kukuta ile account zake za mitandaoni anaendesha mtu mwingne on behalf. Yeye yuko zake busy huko kwingne hana habari.
 
Mimi ni introvert mixture ya melancholy na phlegmatic, kuna introverts ambao ni waongeaji wakiwa tu na watu waliowazoea na huwa wakimya sana wakiwa na watu wasiowazoea, na huyo ni mimi

Mimi kuna ndugu na jamaa zangu ambao sijawazoea wanajua mimi mkimya sana, ukiwaambia ni muongeaji wanakataa katakata, wakati kuna marafiki zangu niliowazoea wanajua mimi muongeaji sana

Hata shuleni ulikuwa ukiwauliza classmates mimi ni mtu wa aina gani, wanakuambia mimi mkimya sana ila wakati huo huo ulikuwa ukiwauliza roommates, wanakuambia mimi muongeaji sana
 
Back
Top Bottom