Ni biashara Gani ulianza na pesa kidogo na inakulipia bills zote,saidia na wengine 🤔🙏❤

Ni biashara Gani ulianza na pesa kidogo na inakulipia bills zote,saidia na wengine 🤔🙏❤

Nikiwa chuo mwaka wa Kwanza
Nilijichanga changa nikafungua
Vijiwe viwili vya kuuza pweza

Kimoja mitaa ya mwenge
Kingine buguruni

Nikawapata madogo wawili wakutoka lindi wakawa wananiuzia

Nilianza na capital ya laki moja na themanini (180k) kwa kila kitu

Yaani
Meza 2 za kishkaji
Themosi, vikombe, vijiko, bakuli
Majiko ya mkaa
Mkaa kidogo
Viazi vya kachori
Mafuta
Pweza nilianza na kilo 5
Nauli za madogo
Nk


Baada ya miezi minne nilifungua
Vijiwe vingine vitatu
Gongolamboto
Mbagala kwa Aziz ally
Ubungo riverside njia panda ya makoka

Na ilikuwa inanipa pesa nzuri kwa wakati ule

Changamoto ilikuwa ni kupitia na kuzunguka vijiwe vyote kukagua nini kinaendelea

Nilichofanya nilikuwa nachukua faida buku 2 kila kijiwe kila siku, na hiyo pesa naikusanya jumamosi

Kila jumamosi nilikuwa nachukua elf 70
Na mara chache ilikuwa inapungua kulingana na changamoto

Nashukuru wale vijana walikuwa waaminifu, sikuwa nawalipa mshahara, yaani niliwaachia mtaji mi nachukua buku 2 kilichobaki chao, ila nazingatia mtaji anaulinda
 
Nikiwa chuo mwaka wa Kwanza
Nilijichanga changa nikafungua
Vijiwe viwili vya kuuza pweza

Kimoja mitaa ya mwenge
Kingine buguruni

Nikawapata madogo wawili wakutoka lindi wakawa wananiuzia

Nilianza na capital ya laki moja na themanini (180k) kwa kila kitu

Yaani
Meza 2 za kishkaji
Themosi, vikombe, vijiko, bakuli
Majiko ya mkaa
Mkaa kidogo
Viazi vya kachori
Mafuta
Pweza nilianza na kilo 5
Nauli za madogo
Nk


Baada ya miezi minne nilifungua
Vijiwe vingine vitatu
Gongolamboto
Mbagala kwa Aziz ally
Ubungo riverside njia panda ya makoka

Na ilikuwa inanipa pesa nzuri kwa wakati ule

Changamoto ilikuwa ni kupitia na kuzunguka vijiwe vyote kukagua nini kinaendelea

Nilichofanya nilikuwa nachukua faida buku 2 kila kijiwe kila siku, na hiyo pesa naikusanya jumamosi

Kila jumamosi nilikuwa nachukua elf 70
Na mara chache ilikuwa inapungua kulingana na changamoto

Nashukuru wale vijana walikuwa waaminifu, sikuwa nawalipa mshahara, yaani niliwaachia mtaji mi nachukua buku 2 kilichobaki chao, ila nazingatia mtaji anaulinda
Bado uko nayo hiyo biashara?
 
Asikuambie mtu biashara ya duka la rejereja limenitoa mavumbini wakuu na nilianza na laki saba tu nilionunulia bidhaa cha msingi :
Sehemu yenye mzunguko mzuri
Uvumilivu manake itakuchukua muda kutengeneza wateja wako
Kauli nzuri kwa wateja
Kutotoa mikopo ya hovyo au usikopeshe kabisa
Usikae na hela always ukishauza jion ukifunga hesabu hela yote kanunulie bidhaa zingine
 
Back
Top Bottom