Ni changamoto zipi umewahi kupitia ukiwa katika hali ya umasikini?

Ni changamoto zipi umewahi kupitia ukiwa katika hali ya umasikini?

Kumbe Dar ikakushinda ukarudi kwenu Mbeya au Dodoma.

Umeona umasikini ulivyo mbaya?
Dar sio tuu nimeishi Bali nimesoma hapo Mlimani naijua vizuri..

Watu wanashindia mihogo na vile vimahindi mnapaka pilipili na mnalia chumvi 😆😆😆😆

Ukigeuka huku shombo ,mbele madimbwi Kila sehemu kiufupi ni hovyo , majority wanashindia biashara uchwara za kuuza maji,wanakoishi Sasa afadhali nguruwe 😃😃

Niliwahi mtembelea Jamaa yangu alikuwa anakaa ubungo,asiee mtu anachota maji ya msimbazi huo umejaa mataka eti ndio anatumia khaa !!
 
Dar sio tuu nimeishi Bali nimesoma hapo Mlimani naijua vizuri..

Watu wanashindia mihogo na vile vimahindi mnapaka pilipili na mnalia chumvi [emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]

Ukigeuka huku shombo ,mbele madimbwi Kila sehemu kiufupi ni hovyo , majority wanashindia biashara uchwara za kuuza maji,wanakoishi Sasa afadhali nguruwe [emoji2][emoji2]

Niliwahi mtembelea Jamaa yangu alikuwa anakaa ubungo,asiee mtu anachota maji ya msimbazi huo umejaa mataka eti ndio anatumia khaa !!
Sasa huoni ni sababu ya umasikini wao?

Tatizo we naye unaandamana na masikini, tafuta marafiki ambao wanaweza kukusaidia na sio kulala stooo
 
Sasa huoni ni sababu ya umasikini wao?

Tatizo we naye unaandamana na masikini, tafuta marafiki ambao wanaweza kukusaidia na sio kulala stooo
Utokee familia ya chini uje kupata rafiki Tajiri never labda ni bahati ikutokee Sasa utakutana nao wapi? Saizi ndio ninao Sasa ila ningesndelea kubakia Dar ningekufa maskini 😁😁
 
Basi watakiwa ukimuona mtu anaishi Dar umsalimu maana si kazi rahisi kabisa kuishi Dsm
75% ya watu wanaoishi Dar ni maskini wa kutupwa 😆😆 na kama unataka kuwa maskini Hadi unazikwa endelea kuishi huko huko..

Kwanza wakati narudi Mkoani kilomouma maana niliacha mademu zangu kibao huko 🤣🤣

Ila uzuri kufika Mkoani nilisoyea miezi kama 6 ila msoto wa nafuu maana Niko mazingira ya home home..

Baada ya mda nikapata kazi Kwa yule mama wa PMM aliyetaka kununua mtaa huko.Buguruni ,from hero to zero ndio nikapatiaga upenyo..

Sina hamu na Dar 😂😂
 
Ili kuimarika kuna mapitio mengine ni muhimu kuyapitia ili yawe ukumbusho wa kukosa pale ukipata.

Ila kiukweli kabisa hakuna faraja kwenye ufukara.

Nakumbuka kuna kipindi nilipigika ikawa natembelea washkaji mida ya misosi kiasi cha kujua ratiba ya mlo wa masela wote.

Kuna msela wangu (Mungu amlaze mahala pema) ilikuwa ikifika jioni ananipigia simu kuniita tukapige story, kumbe alishajua hali yangu na ule wito ulikuwa ni msaada indirectly maana alihakikisha nakula ndio naondoka.

Na kila nikiondoka mkewe ananipa kikontena cha msosi ananiambia shem naona chakula cha leo umekipenda beba na hiki utakula baadae.

Hawakujua jinsi gani walikuwa wakinisevu.
Mkuu familiya ya msela ambaye alihakikisha unakula nyumbani kwake na mkewe kukufungia kingine ambaye ameshatangulia mbele ya haki, huwa unapata muda kuitembelea?.
 
Wimbo wa Kamandaaa wa Duz nundaz enzi hizo wakina Feruz Daz baba wanashinda kwenye vimbweta vya pale Azania wakiishusha mistari
Daaah umenikumbusha mbali sana..Enzi hizo mchwa mpaka kapunguza ukali,Daaah kweli maisha yanasonga ni mda sasa almost 20yrs
 
75% ya watu wanaoishi Dar ni maskini wa kutupwa 😆😆 na kama unataka kuwa maskini Hadi unazikwa endelea kuishi huko huko..

Kwanza wakati narudi Mkoani kilomouma maana niliacha mademu zangu kibao huko 🤣🤣

Ila uzuri kufika Mkoani nilisoyea miezi kama 6 ila msoto wa nafuu maana Niko mazingira ya home home..

Baada ya mda nikapata kazi Kwa yule mama wa PMM aliyetaka kununua mtaa huko.Buguruni ,from hero to zero ndio nikapatiaga upenyo..

Sina hamu na Dar 😂😂
Mkuu mjini mipango ila mkoani kuna fursa pia
 
Mkuu familiya ya msela ambaye alihakikisha unakula nyumbani kwake na mkewe kukufungia kingine ambaye ameshatangulia mbele ya haki, huwa unapata muda kuitembelea?.
Wamekuwa sehemu ya familia yangu kwa sasa. Watoto wake aliowaacha wadogo kama kuja kujua kuwa sikuwa ndugu wa damu wa baba yao nadhani itakuwa ni hivi karibuni tu sababu wamekuwa wakubwa kuweza kuelewa mambo. Na hilo halijaathiri upendo na heshima kubwa baina yetu.

Harusi ya binti yake nilisimama kama baba wa binti (nahisi unaweza kuhisi ukaribu wetu ni wa kiasi gani)

Msaada wake kwangu haukushia kwenye chakula tu. Alinipa connections ambazo zimenifikisha nilipo leo (sio tajiri lakini hakika namshukuru Mungu sio maskini pia), kupitia hizo connection kulifanya ukaribu wetu uwe zaidi kabla ya mauti yake sababu ya muingiliano wa moja kwa moja wa kibiashara kiasi cha familia zetu kuwa mithili ya ndugu mpaka leo hii.
 
Nilikuwa naishi na bibi yangu, kwakuwa hatukuwa na chakula ndani ikabidi aniache pekeyangu aende kwa baba zangu wadogo kuomba pesa ya matumizi.

Safari yake ilikuwa ya siku mbili kama sijakosea. Aisee nilishikwa na njaa nikachemsha yale mamchicha mekundu nikala baadae nikaenda kwa jirani nikakuta wanatoa vichwa kwenye samaki wadogo kanda ya ziwa tunawaita Furu.

Ikabidi niwaombe vile vichwa, nakumbuka nilidanganya naenda kumpa bata wangu. Nilichemsha vile vichwa nikala nikanywa na supu angalau nikawa vizuri.

Tulipokuwa tunapitia hali ngumu Bibi alijua ninaumia japo nilikuwa sisemi chochote alinitia moyo huku akilengwa na machozi "IPO SIKU UTAKULA VIZURI NA UTAKULA UNACHOKITAKA"
Mungu alivyo wa ajabu, ukipata fedha unaugua kisukari! Daktari anakukataza kula vinono
 
Huu ujumbe unatia moyo Sana.
Hii inaweza kuwasaidia

Kwa hustler yeyote ukiingia kwenye mji au nchi yoyote ambao ww ni mgeni huna pa kufikia wala hujui utapata wapi kibarua, cha kufanya uliza mwenyeji yeyote akuelekeze mahali Soko kubwa la mji lilipo.

Amini nakwambia hutolala njaa pindi ukifika sokoni na hutakosa kazi ya kufanya hata kubeba mzigo utabeba na pesa utapata.

Why Sokoni na si mahala pengine? Sokoni ndio sehemu ambapo kuna mzunguko mkubwa wa pesa katika mji au kitongoji husika. Baada ya hapo sasa utaweza kuangalia ufanyaje ili utoke kimaisha.

Sehemu nyingine ambayo inaweza kukuokoa ni Migahawani au Hotelini. Hii sehemu inaweza kukuokoa usilale na njaa na pia unaweza kupata ujira mdogo. Ukifika maeneo hayo omba kazi ya kufanya usafi na hata kuosha vyombo. Hii itakusaidia sana kupata ujira mdogo na chakula pia.

Mwisho kabisa ni nyumba za ibada iwe msikitini au kanisani. Huku kunaweza kukupa fursa ya kukutana na watu wenye hofu na kumjua Mungu hivyo ni mara chache sana kwa wewe mgeni kukosa hifadhi au chakula, na ukiwa nao vizuri unaweza ukapatiwa connection ya kazi.

Kikubwa ukifika sehemu yoyote jiepushe sana kuomba Fedha bali omba kibarua /kazi ,hii itakuwezesha upate pesa ya kujikimu na vilevile kukuepusha dhidi ya fedheha na udhalili wa kuombaomba. Kumbuka mwanadamu hapendi kuombwa pesa.

Katika kutafuta pesa epuka kitu kinachoitwa kuona aibu, watu watakuchukuliaje nk. Mwanaume hachagui kazi as long as kazi hiyo ni ya halali na haimuondolei utu wake.
 
Back
Top Bottom