Ni gari gani huwezi kununua Wala kumshauri mwingine anunue?

Ni gari gani huwezi kununua Wala kumshauri mwingine anunue?

Mkuu, hiyo Subaru yako ina matatizo makubwa tu... Subaru hata iwe imechoka vipi, lita 1 inaenda sio chini ya kilometa 10 iwe Impreza au Forester...
Hamjanielewa nimesema subaru inanyonya mafuta halafu kwa siku unaweza tumia elfu 90 .
 
Hamjanielewa nimesema subaru inanyonya mafuta halafu kwa siku unaweza tumia elfu 90 .
Ndio ila hapo kuna tatizo kubwa sana ktk hio Subaru yako... Mafuta ya elfu90 ni lita 25 ambapo inatakiwa utembee kilometa 250... ambapo Subaru zote kwa kawaida inatakiwa itembee sio chini ya Km10 kwa lita 1. Nenda garage nzuri wataalam wa Subaru... Nimetumia Subaru Impreza na Forester kwa miaka 5, sijawah kutana na utumiaji mkubwa kias hiko
 
Wana Jf salaam,

Ikiwa ni weekend tulivu kabisa.
Kama tujuavyo, kumiliki gari sasa hivi ni miongoni mwa vitu vya muhimu sana.

Wamiliki wapya wanaongezeka kila kukicha, na kwa bahati mbaya wengi hujikuta wanamiliki magari ambayo baadae yanakuja kuwapa changamoto na kujutia kabisa.

Leo embu tuambiane ukweli, pengine kupitia uzi huu utakua msaada kwa mtu au watu kabla ya kufanya maamuzi ya kuingia kwenye dunia ya umiliki wa gari.

Ni gari gani ambayo hauwezi kumshauri mtu kununua na ni kwanini?
Gari zote Za kijerumani isipokuwa benz, gari zote Za UK, Nissan xtra, Nissan Mach, hino, vits new model,
 
Kiujumla magari mengi ya ulaya hassa uingereza na ujerumani karibu yoote yanakuwa over Engineared ! Wanazingatia saana usalama na comfort ya gari, vile vile yanakuwa yametembea saana kilometa nyiingi, likiisha warranty wanauza.
Kwa namna hiyo kununua yaliyotumika used, kuwa na changa moto nyiingi saana na kati ya gari kumi saba hazifiki miaka mitatu Bongo, ununue iliyo kuwa bado ina upya itakupa muda kiasi, nimemiliki nyiingi tu kweli likiwa used na model chini ya miaka 13 hazifai. Bora kuanzia 2015 ambazo ni za gjhali saana. Sishauri mtu mwenye kipato chochote kununua gari ya zamani mno za Europe ni pasua kichwa.
Kwa mjapan Nissan nyiingi zinafanana spare parts zake tabu na bei juu mfano. Namiliki Nissan Patrol y62 ya 2017 - gari V8 ina nafasi ina nguvu nilinunua mpya sasa inasoma laki km kwenye Dash board ilipofika kM 92,000 ilisumbua sana senser, ignition coils,plugs,rejeta, fuel pump n.k. nilisimamisha miezi mitatu nakusanya nguvu kuagiza spare na ufundi wa uhakika limegharinu zaidi ya milioni 27. Kwa sasa lipo saafi illa sishauri kuwa mtu awe nalo labda uwe na uwezo wa pesa, natumia kwa safari sasa sana na lipo saafi na lina bugia wese balaa gari ya starehe na nguvu.
Nimenunua gari mbili hilux 2017 used na harrier 2008 used yaani na enjoy hamna shida natumia killa siku na masafa mafupi mambo safi na wife nimemchukukia Crown Athletic 2010 ( alikuwa na Bmw x5 ilitushinda) ana enjoy na kwa sasa hata pesa zinabaki na mjengo wetu unaelekea kwisha bado kidogo.
Nimemiliki namshukuru mungu gari nyiingi aina nyiingi , Gari ni Toyota kwa Africs.
Nissan naitangaza hakuna mteja na mpango wa kuliuza lipo safi sasa hata offer niliyopeea ya Mill 100 bora kuliko likianza matatizo.
Nimeagiza Toyota Prado Diesel litafika mwishoni mwa mwaka kwa njia ya finance la mwaka 2021 ni mara dufu bora.
Kuna jamaa yangu analo la 2016 hadi leo KM 278,780 hamna shida ni Breki na service tu.
Kwa uchache Bongo ni Toyota hata ukiwa na pesa vipi zingine ni majanga tu.
Umeeleza vizuri..
Samahani lakini, we ni Muhaya..??
 
1. nissan extrail, hii imeshachangiwa na members wengine humu tayari, cha kuongezea tu ni kwamba hizo nissan wenyewe walitoaga tamko kwama walibugi kwenye hizo gari, kuchemsha hilo gari ni ugonjwa mkubwa, labda ubadilishe rejeta uweke kubwa_modification

2. European cars ambazo hazijathibitshwa na wenyewe, kwamba umenunua kwa third part owners kama sbt, kwa mtu, befoward etc..yaani iwe bmw, volvo, honda etc kama umenunua used kwa mtu basi jua asilimia ya kuwajua mafundi wote hapa mjini ni mkubwa sana, nunua hata ikiwa used iwe imethibitishwa iko okay na authourised European car agent wa hayo magari..itakupa garantii kwamba sensor hazijawa bypassed etc etc engine haijawahi chezewa ili kukunusuru otherwise buy 0 km car.
ukitaka kuthibitisha hili nenda kuna mtaa mmoja hapo mwenge kule karibu na mapambano yamejaa mabmw, nenda kinondoni hananasif mtaa wote umejaa rangerover..au tembelea mitaa ya mbezi beach, makumbusho uone bmw na rangerover zimekuwa mapagale..

3. Daihatsu Terrios/ camry...automatic gear box zake mbovu

4. mazda tribute, hyundai , isuzu trooper, bighon, honda oddesy..hamna spare utachina na hela unayo, litaishia kupaki uwani liwe jumba la panya..spare mpaka nairobi au japan
5. Nissan kwa ujumla: ie terrano, navara.. hazikopeshi hizi gari, hazivumilii watu maskini, ihudumie ikuhudumie, ikose maji tu au oil mlimani inakukaangia engine dakika 0 tu..iwekee shock up og ukiweka za 80k wiki tu unayaingia mashimo mazima mazima.

Pendekezo.
Toyota ndo magari yako made for us, yanavumilia, hata ukiyawekea oil ya boda boda yatakuvumilia..nenda milimani mahenge uko utakua toyota corolla ya mwaka 89 inakilometa laki 6 na inapiga kazi mzee.
Mzee umeua.mim toka mdogo pale mwenge karibu na polisi kwa nyuma ule mtaa ma bmw na mabenz mazur mazur ila mabov hatar
 
Ufafanuzi tafadhali
Natumaini wazima nyote humu.
Nimeona nitolee mchango wangu hapa kwenye Nissan March.
Nimemiliki Nissan March (Old), yafuatayo ni Mazuri yake:
  1. Very economy kwenye Mafuta.
  2. Ni kizuri kwa matumizi ya kila siku, wale wa mishemishe za kubebea vitu vyepesi hapa na pale, kinawafaa.
  3. Engine yake ni Ngumu Ukiijali Service kwa wakati, rejeta itaitaji modification kidogo kwa kureplace zile Plastic top covers kwa steel top covers ili kuzuia kuchemsha.
Changamoto zake:
  1. Spear Mpya dukani hamnaga, nishasota sana maduka yote makubwa ya Nissan, wanakwambia hamna demand ya spear parts kwa hizi gari maana ni zakitambo. Spear parts utapata kwenye Used tu mfano ilala, Tandale kwa Dar.
  2. Spear parts ni Ghali mno so unatakiwa ujimudu.
  3. Spear parts kwakua ni used, zinakua na maisha mafupi mno, so kujikuta unabalidilisha spear moja mara 2 mpaka 3 kwa mwaka ni kawaida mno.(mfano Hub bearings, shock-ups..)
  4. Kiujumla maintainance ya hichi kigari iko juu sana compared na wenzake kina VITS, IST, DUET, SUZUKI K nakadhalika.
  5. Ukimiliki Mjini tu, ukienda chaka huko utaki telekeza.
 
Mi nina mazda cx 5 yangu mwaka wa nne sasa japo ilipata ajali imesharudi barabarani tayari iko fresh kabisa..... Napata heshima gari ni maamuzi tu na uelewa kuna gari zinahitaji u smart kichwan sio kichwa I mweupe halafu unataka umiliki lazima tu utaanza kumtukuza mjapan hasa Toyota but always mm nasema bongo hasa Tz hatuyapendi magari tupo poor why kenya European zinafanya vizuri sana
 
Mkuu, hiyo Subaru yako ina matatizo makubwa tu... Subaru hata iwe imechoka vipi, lita 1 inaenda sio chini ya kilometa 10 iwe Impreza au Forester...
Vipi kuhusu mnyama legency kila kukicha watu wana jitahidi kuziuza tena bei ya kawaida Forester xT habari nyingine inapuuliza wese asikwambie mtu
 
Vipi kuhusu mnyama legency kila kukicha watu wana jitahidi kuziuza tena bei ya kawaida Forester xT habari nyingine inapuuliza wese asikwambie mtu
Legacy zinauzwa cheap kwasabab zimepoteza mvuto na muonekano wake kama tax za kizaman alafu ndani space ndogo😅, ila si kwamba ni mbovu au zina shida... Subaru XT tena uikute ni Turbo inavuta wese sana wenyew wanasema Turbo ili isile mafuta inataka speed ukiwa high way ndio utainjoi ila ukiwa na trip za mjini tu wese linaenda, japo sio sana kias cha kutisha ni 9km per lita...
 
Kiujumla magari mengi ya ulaya hassa uingereza na ujerumani karibu yoote yanakuwa over Engineared ! Wanazingatia saana usalama na comfort ya gari, vile vile yanakuwa yametembea saana kilometa nyiingi, likiisha warranty wanauza.
Kwa namna hiyo kununua yaliyotumika used, kuwa na changa moto nyiingi saana na kati ya gari kumi saba hazifiki miaka mitatu Bongo, ununue iliyo kuwa bado ina upya itakupa muda kiasi, nimemiliki nyiingi tu kweli likiwa used na model chini ya miaka 13 hazifai. Bora kuanzia 2015 ambazo ni za gjhali saana. Sishauri mtu mwenye kipato chochote kununua gari ya zamani mno za Europe ni pasua kichwa.
Kwa mjapan Nissan nyiingi zinafanana spare parts zake tabu na bei juu mfano. Namiliki Nissan Patrol y62 ya 2017 - gari V8 ina nafasi ina nguvu nilinunua mpya sasa inasoma laki km kwenye Dash board ilipofika kM 92,000 ili
.
.
.APO USIKUTE BANDO LA KUINGIA JF UMEMUIBIA SHEMEJI YAKO CHENCH ALIVYO KUTUMA KARANGA
 
Imprezza ina tofaut gani na IST? Kwa cc?

Mkuu usijidanganye na cc 1490 za subaru ukadhani ziko sawa na za IST.

Cc za gari zinaweza kutumika ku determine power na ulaji mafuta wa gari, ila sio kigezo pekee cha ku determine hizo.

Kuna vitu vingi sana vina determine na inabidi uwe unalijua gari moja moja na mifuno yake ndipo utaweza kujua ipi unakula zaidi.

Factors ni kama hizi
  • type ya engine
  • mwaka wa gari
  • aina ya mafuta inayotumia
  • technology iliotumika

Mfano mdogo tu, kuna gari inaitwa Mazda rx 8, hii gari ina cc1300 tu, ila ndugu ya tu usijidanganye ukaifukuzia ikakukalisha wewe na cc2500 za brevis yako. Na inabugia mafuta kuliko hata toyota za Cc2500. Why? Sababu inatumia rotary engine tofauti na za toyota.

Turudi katika ulinganisho wako, Subaru wanatumia boxer engine, ni powerful na zinabwia mafuta ukilinganisha na cc za engine za toyota.

Yaani ukiweka subaru ya cc1490, 1990 zinabwia wese na powerful zaidi ya toyota za same engine size

Mfano mimi natumia Volkswagen polo ina cc 1380 tu, ila kanakunywa mafuta vizuri na kanakimbia kuliko hata IST ya 1490, na hata baadhi ya magari ya cc2000+ nawakalisha vizuri tu

I hope umenipata hapo
 
Legacy zinauzwa cheap kwasabab zimepoteza mvuto na muonekano wake kama tax za kizaman alafu ndani space ndogo[emoji28], ila si kwamba ni mbovu au zina shida... Subaru XT tena uikute ni Turbo inavuta wese sana wenyew wanasema Turbo ili isile mafuta inataka speed ukiwa high way ndio utainjoi ila ukiwa na trip za mjini tu wese linaenda, japo sio sana kias cha kutisha ni 9km per lita...

Unajua lkn turbo ina-operate vipi?Yaani turbo 'ifunguke' kweli kweli halafu Muda huo eti consumption ndio iwe ndogo?Aiseee
 
Back
Top Bottom