Ni halali CCM kufanyia vikao Ikulu?

Ni halali CCM kufanyia vikao Ikulu?

Naomba kufahamishwa na wale wenye kufahamu zaidi, hivi ni sawa vikao vya CCM kufanyika Ikulu? Ninavyotambua Ikulu huwasikilisha serikali ikiwa ni pamoja na jamii nzima ya Tanzania.

Hivi CUF, TLP au Chadema wanaweza kufanyia mikutano yao Ikulu au katika sehemu zingine kama hizo?
CCM miaka ya hivi karibuni (hususani chini ya awamu hii) inafanya mambo yake kama vile mtu anayetaka kujinoma kamwisho-mwisho kabla utamu haujaondolewa.

[HASHTAG]#2020mtuchali[/HASHTAG]
 
Mkuu, naomba nikiwa nikufahamishe kuwa sina personal issue na mtu yeyote, na uandishi wangu hautawaliwi na hizo. Kama umesoma vizuri nimeuliza swali la kimsingi kuhusu kufanyia vikao vya chama tawala ikulu. Nakumbuka kuanzia enzi za TANU (ndiyo, nakumbuka vizuri sana) vikao vya chama vilifanyika katika ofisi za chama, hata wakati wa Chama kiliposhika hatamu, ndio kwanza makao makuu ya CCM Lumumba street, yakapata hadhi zaidi. Je kumekuwa na mabadiliko rasmi mapya yaliyotokea ambapo chama tawala kimeshika hatamu tena
Mkuu sio kweli kwamba tokea zamani vilikuwa vinafanyika kwenye makao ya ccm,Kuanzia wakati wa Mwalimu Nyerere,Wakati wa Mwinyi,Wakati wa Mkapa,Wakati wa Kikwete mpaka utawala huu wa awamu ya tano,wote wamefanyia vikao,vya chama kinachotawala ikulu.
Hata kwa rais Magufuli hii si mara ya kwanza,Mwaka 2016 My 05,ccm walifanya kikao cha kamati kuu ya halmashauri kuu,Ikulu ya Chamwino,lakini hukuuliza kwa nini,au ilikuwa ni sahihi kufanya vile.13-december,2016 kamati kuu ya ccm walifanyia kikao,pale ikulu ya magogoni,hukuona.
Tarehe,02-03-2015,ccm central committee walifanyia kikao cha ikulu,chini ya rais Kikwete,hukuona wala hukuoji,
Tarehe 28-02-2015 ccm central committe walifanya kikao ikulu ya magogoni,lakini hukuona
Tarehe 22-05-2010 ccm central committee walifanya kikao ikulu ya magogoni.
Chama tawala kwa kawaida kiongozi wake wakati mwingine huitisha kikao kama hicho ikulu,ili aweze kufanya majukumu yake kama rais au mwenyeketi.
Rejea mwezi April au May,wakati rais Trump alipotakakubadilisha sheria ya Obamacare,aliwaita senetors wote wa republican ikulu ya white house,kwenda kuweka mikakati ya pamoja kuweza ku-repeal Obamacare.
 
Naomba kufahamishwa na wale wenye kufahamu zaidi, hivi ni sawa vikao vya CCM kufanyika Ikulu? Ninavyotambua Ikulu huwasikilisha serikali ikiwa ni pamoja na jamii nzima ya Tanzania.

Hivi CUF, TLP au Chadema wanaweza kufanyia mikutano yao Ikulu au katika sehemu zingine kama hizo?

Ni halali kwa yafuatayo
1) chama tawala
2) katiba yenu inaruhusu
3) bado nchi ina wajinga wengi 89% kwa utafiti wangu bado wana matope kichwani
 
Hii Tabia Rais Maguful anayotaka kuiotesha mizizi ya kufanya vikao vya Chama Ikulu bila hata ya kuwa na aibu, Inatia najisi siasa na serikali ya Tanzania.

Maraisi waliotoka hawakuwahi kufanya huu ufisadi sababu hawakuwa wajinga. Na si kuwa hawakuwa na ubavu wa kufanya ivyo. Ni kuwa walitumia busara zaidi kuliko kiburi na jeuri. Walijitambua kuwa katiba imewapa mamlaka makubwa sana kiasi kuwa hata hawakupaswa kuhojiwa kwa kosa lolote ambalo walifanya.

Matumizi ya Ikulu kwa biashara binafsi Ni ufisadi sababu ni matumizi mabaya ya Mali za umma.

Kodi zetu ndizo zinalipa billi ya maji ya ikulu.

kodi zetu ndizo zinanunua chakula cha ikulu.

kodi zetu ndizo zinalipa mishahara kwa wahudumu na walinzi wote wa ikulu.

kodi zetu ndizo zinalipia billi ya umeme wa ikulu.

Na kodi zetu ndizo zilijenga ukulu.

Leo ikulu ndiyo inatumiwa Na Raisi kufanya biashara zake binafsi. Vikao vya chama ni biashara yake BINAFSI. Sisi ndyo tunagharamikia hii biashara yake binafsi.

Ni katiba yetu mbuvu tu ndyo inambeba Raisi. Angekuwa kwenye nchi zilizoendelea hapa Rais alikuwa anastep down na kuhukumiwa kwa kosa la kuhujumu mali ya umma.

Kama leo Ikulu inatumika kufanya kazi za kichama kweupe kabisa. Vipi kuhusu kodi zetu. Maana hii inatupa picha kuwa inawezekana ndizo hizi kodi zetu zinatumika pia hata kwenye majukumu mengine ya kichama.

Tunahitaji wachunguzi waje wafanye auditing vizuri ya vyanzo vya pesa vya CCM na wacompare na matumizi yao.
Siwezi kuprove kuwa CCM wanatufisadi bila auditing, ila ninaimani 50% ya matumiz yao ni kodi zetu.
 
Hii Tabia Rais Maguful anayotaka kuiotesha mizizi ya kufanya vikao vya Chama Ikulu bila hata ya kuwa na aibu, Inatia najisi siasa na serikali ya Tanzania.

Maraisi waliotoka hawakuwahi kufanya huu ufisadi sababu hawakuwa wajinga. Na si kuwa hawakuwa na ubavu wa kufanya ivyo. Ni kuwa walitumia busara zaidi kuliko kiburi na jeuri. Walijitambua kuwa katiba imewapa mamlaka makubwa sana kiasi kuwa hata hawakupaswa kuhojiwa kwa kosa lolote ambalo walifanya.

Matumizi ya Ikulu kwa biashara binafsi Ni ufisadi sababu ni matumizi mabaya ya Mali za umma.

Kodi zetu ndizo zinalipa billi ya maji ya ikulu.

kodi zetu ndizo zinanunua chakula cha ikulu.

kodi zetu ndizo zinalipa mishahara kwa wahudumu na walinzi wote wa ikulu.

kodi zetu ndizo zinalipia billi ya umeme wa ikulu.

Na kodi zetu ndizo zilijenga ukulu.

Leo ikulu ndiyo inatumiwa Na Raisi kufanya biashara zake binafsi. Vikao vya chama ni biashara yake BINAFSI. Sisi ndyo tunagharamikia hii biashara yake binafsi.

Ni katiba yetu mbuvu tu ndyo inambeba Raisi. Angekuwa kwenye nchi zilizoendelea hapa Rais alikuwa anastep down na kuhukumiwa kwa kosa la kuhujumu mali ya umma.

Kama leo Ikulu inatumika kufanya kazi za kichama kweupe kabisa. Vipi kuhusu kodi zetu. Maana hii inatupa picha kuwa inawezekana ndizo hizi kodi zetu zinatumika pia hata kwenye majukumu mengine ya kichama.

Tunahitaji wachunguzi waje wafanye auditing vizuri ya vyanzo vya pesa vya CCM na wacompare na matumizi yao.
Siwezi kuprove kuwa CCM wanatufisadi bila auditing, ila ninaimani 50% ya matumiz yao ni kodi zetu.
 
Moja kati ya mambo yanayonishangaza ikulu kutumiwa kwa shughuli za chama.
 
Nchi yetu ni mali ya watanzania na muongozo wake ni katiba tuliyonayo.

Jana kwa hofu tena na aibu juu kamati kuu ya CCM imekutana usiku ikulu katika kujadiri mambo ya chama.

Suala hili ni kinyume cha sheria kutumia ofisi ya umma kufanyia mkutano wa chama cha siasa.

CCM mna ofisi Lumumba, Dodoma mna majengo mawili pale JK Convertion centre pamoja na lile jengo lenu la bendera ya chuma Nendeni huko hata mkalale kabisa hakuna atakayewahoji lakini kutumia mali ya umma kufanyia kikao chenu ni big NO.

Mnatuudhi.
 
Kufanyika mara nyingi hakuhalalishi jambo.

Watu wakiuua mara nyingi, does it make murder legal?
Kwa hili la Vikao vya CCM ni halali kwasababu ni utaratibu uliokuwepo. Na kila kiongozi wa CCM anauenzi utaratibu hata kama Kuna wavimba macho wachache wanaoupinga. Hayo ya kuua muulize Gaidi Mbowe!
 
Jpm alipigiwa kelele lakini wala haikusaidia kitu kuhusu hilo suala, labda Katiba haitoi katazo lolote
 
Nchi yetu ni mali ya watanzania na muongozo wake ni katiba tuliyonayo.

Jana kwa hofu tena na aibu juu kamati kuu ya CCM imekutana usiku ikulu katika kujadiri mambo ya chama. Suala hili ni kinyume cha sheria kutumia ofisi ya umma kufanyia mkutano wa chama cha siasa.

CCM mna ofisi Lumumba, Dodoma mna majengo mawili pale JK Convertion centre pamoja na lile jengo lenu la bendera ya chuma Nendeni huko hata mkalale kabisa hakuna atakayewahoji lakini kutumia mali ya umma kufanyia kikao chenu ni big NO.

Mnatuudhi.
MIMI NA MAGUFULI KITU KIMOJA.... Jiwe alikuwa anafanya upuuzi huo huo kwenye ofisi ya umma kwa chama chake, against the rules and regulation of doing political party affairs
 
Wizi wa kura na kununua wapinzani huwa unaratibiwa na upinzani?
 
Nchi yetu ni mali ya watanzania na muongozo wake ni katiba tuliyonayo.

Jana kwa hofu tena na aibu juu kamati kuu ya CCM imekutana usiku ikulu katika kujadiri mambo ya chama. Suala hili ni kinyume cha sheria kutumia ofisi ya umma kufanyia mkutano wa chama cha siasa.

CCM mna ofisi Lumumba, Dodoma mna majengo mawili pale JK Convertion centre pamoja na lile jengo lenu la bendera ya chuma Nendeni huko hata mkalale kabisa hakuna atakayewahoji lakini kutumia mali ya umma kufanyia kikao chenu ni big NO.

Mnatuudhi.
Aliposema yeye na Magufuli ni kitu kimoja wengi hatukumwelewa
 
Back
Top Bottom