Ni heri kubariki ndoa kuliko kufunga harusi

Ni heri kubariki ndoa kuliko kufunga harusi

Nadate n a kitoto kinakaribia kulingana na first born wangu kina 17 yrs old kinaniambia eti kina miaka minne toka kimeanza mapenzi sasa huyu akishafikisha 25 si balaa, na hapo alishaachana si chini ya mara sita
 
Naelewa concept yako Ndugu Mtakatifu.Lakini naona kuna mchanganyiko katika maelezo yako.

Tukio la kubariki ndoa, si Toba. Bali ni tukio la kutaka kuishi katika utaratibu sahihi wa Mungu kati ya mke na mume.

Toba ni tukio la kujutia ile dhambi yako,kuikiri na kuiacha, na katika mada hii, dhambi ni uzinzi.

Unaweza kubariki ndoa, lakini ukawa hujatubu dhambi yako ya uzinzi wala hujajutia, na hiyo dhambi ikawa na wewe ndani ya hiyo ndoa.

Ushauri ni kwamba, kabla ya kubariki ndoa,kwanza tubu dhambi yako na kuiacha huku ukiwa unaendelea na mchakato wa kubariki.

Neno KUBARIKI ndoa ni kuita baraka za Mungu ambazo hazikuwepo wakati mmeshaanza kuishi tu bila utaratibu wake Mungu.

Hivyo KUBARIKI ndoa SI TOBA japo unaweza fikia TOBA wakati unaelekea mchakato wa Kubariki ndoa.Ili ile laana ya uzinzi itoke na uanze kuridhiwa kutembea na baraka za Mungu.
 
Nimechukua miaka miwili kuchunguza hili Jambo, kwanini ndoa za siku hizi hazidumu na zimesongwa na milima mingi na mabonde kuliko tambarare. Kila mara watu wanatumia nguvu nyingi kuendesha mahusiano yaliyokufa ndani ya nafsi japo Yana heshima kubwa mbele ya macho ya watu.

Baada ya uchunguzi nimegundua ndoa nyingi zinazofungwa makanisani na misikitini zilitakiwa zibarikiwe tu na sio kufungwa Kama ndoa takatifu maana ndoa hizo zilishafungwa tayari na wapendanao.

Athari za kufunga ndoa iliyotakiwa kubarikiwa

1) Ulinzi, baraka na ahadi za Mungu juu ya ndoa hupotea na kamwe hautakuepo mpaka mtubu dhambi ya uzinzi juu yenu.

2) Kufa kwa ndoa husika maana mshahara wa dhambi ni mauti na Mungu kamwe hadhihakiwi.

HITIMISHO
Usiende mbele za Mungu kuoa au kuolewa na mpenzi ulieshiriki nae tendo la ndoa kabla ya ndoa Bali mbariki hiyo ndoa kwa kuomba toba ya msamaha ili Mungu afanye Jambo jipya ya kale yatapita na tazama yatakuwa mapya.
Baada ya uchunguzi nimegundua ndoa nyingi zinazofungwa makanisani na misikitini zilitakiwa zibarikiwe tu na sio kufungwa Kama ndoa takatifu maana ndoa hizo zilishafungwa tayari na wapendanao.[emoji1545]
 
Kubaliki ndoa kuliko kwenda kumkana Na mumdanganya Mungu mbele ya madhabau takatifu ......kuapa uongo mbele za Mungu ni kitu hatari Cha kuogopwa na kutisha magumu wanayopitia waliofanya hivyo kamwe usikae kuwashauri laana zinavyo watafuna
Kiapo chenyewe kimeandikwa kama script. Maneno ya kukiri unapangiwa badala ya kujipangia mwenyewe. Na mbaya zaidi kaandika mtu lakini unaapa kwa Mungu. Watu tunadanganyana kwa mengi sana.
 
Kwan ukifunga ndoa kuna mahali mnaulizwa km mlishawah kufanya tendo???
 
Naelewa concept yako Ndugu Mtakatifu.Lakini naona kuna mchanganyiko katika maelezo yako.

Tukio la kubariki ndoa, si Toba. Bali ni tukio la kutaka kuishi katika utaratibu sahihi wa Mungu kati ya mke na mume.

Toba ni tukio la kujutia ile dhambi yako,kuikiri na kuiacha, na katika mada hii, dhambi ni uzinzi.

Unaweza kubariki ndoa, lakini ukawa hujatubu dhambi yako ya uzinzi wala hujajutia, na hiyo dhambi ikawa na wewe ndani ya hiyo ndoa.

Ushauri ni kwamba, kabla ya kubariki ndoa,kwanza tubu dhambi yako na kuiacha huku ukiwa unaendelea na mchakato wa kubariki.

Neno KUBARIKI ndoa ni kuita baraka za Mungu ambazo hazikuwepo wakati mmeshaanza kuishi tu bila utaratibu wake Mungu.

Hivyo KUBARIKI ndoa SI TOBA japo unaweza fikia TOBA wakati unaelekea mchakato wa Kubariki ndoa.Ili ile laana ya uzinzi itoke na uanze kuridhiwa kutembea na baraka za Mungu.
Mkuu upo sahihi sana....ila kwenye process za kubariki ndoa huwa tunakamilishaga na toba pia japo hata kugundua umekosea na kutaka kubariki ni ishara ya kutubu kwa mtu.
 
Back
Top Bottom