Ni ipi sababu ya Rais Samia kuwa karibu sana na kuipa uzito Nchi ya Oman?

Ni ipi sababu ya Rais Samia kuwa karibu sana na kuipa uzito Nchi ya Oman?

Hawa waZenj wamepumbazwa sana na vijizawadi wanavyopewa kutoka kwa watawala wa Oman ambao ni ndugu wa Sultan aliyepinduliwa 1964!!

Sijui kwanini wanadhani hawa waliopinduliwa na sasa wako Oman hawataki kurudisha kile ambacho wanaamini walinyang'anywa? Mimi naona wanawakula timing tu siku moja mtakuja kukuta manowali iko nje ya Bandari wanayojenga na hapo ndiyo mtakapojua kunyoa au kusuka?

Mafundisho haya uliyapata kwa Mchungaji wako Tito?
 
Nimekuwa nikiona Rais wetu akiipa uzito hii nchi ya kuitwa Oman.

Hadi sasa ninachojua tu ni kwamba Zanzibar ilikuwa koloni la Oman na masultani wake walikuwa na asili ya Oman.

Ila leo pia nimeona hii nchi nayo ipo mbioni katika kinyanganyiro cha kujenga Bandari ya Bagamoyo.

Kwa anaejua japo hata kidogo ningependa kujua nini hasa kipo nyuma ya pazia.
Soma vizuri historia yako, nionavyo mimi Oman ndiyo ilikuwa koloni la Zanzibar.
 
mashariki

Jamaa smart sana, Ana Ana tuzo nyingi kote mashariki na Magharibi UK, Italy, Portugal mpaka Ottoman, anafaa hata kwenye mitaala mashuleni afundishwe kuondoa mentality za kitumwa mashuleni.
Hujasema hao weusi wametokea wapi, naona hili swali ni gumu kwako.
Hiyo Oman inawezekana ikawa kama Liberia? Waarabu walipoona hawataki kujihusisha na watu weusi wakawaundia nchi yao, Oman?
 
Hujasema hao weusi wametokea wapi, naona hili swali ni gumu kwako.
Hiyo Oman inawezekana ikawa kama Liberia? Waarabu walipoona hawataki kujihusisha na watu weusi wakawaundia nchi yao, Oman?
Conspiracy theory with no basis!
 
Conspiracy theory with no basis!
"Conspiracy theory".

Hiyo itakuwaje 'conspiracy theory', labda uwe hujui maana ya msemo huo.

Msaidie basi mwenzio kujibu swali nililouliza. Hao weusi wa Oman walitokea wapi. Asili yao ni wapi hasa? Au ni wa hapo hapo Oman zama na zama! Kama walivyo wale weusi wa New Guinea kule Mashariki ya mbali!

Sema hao weusi walitokea tokeaje wakawa hapo, na kuwa watawala wa sehemu hiyo.
 
Unapataje Uhuru kama hujatawaliwa?
Aisee!
Naona kama suala la Uhuru wa Znz limetawaliwa na propaganda nyingi..
Hii maana'ake nini?
👇👇
Disemba 10 mwaka 1963, Zanzibar ilipata uhuru kutoka kwa Uingereza, lakini ya vyama vya ZNP na ZPPP iliyoingia madarakani iliondolewa katika mapinduzi ya tarehe 12 Januari 1964. Ni tarehe hiyo ya mapinduzi inayotambuliwa kama siku ya uhuru wa visiwa hivyo...

Nadhani Uhalisia ni kuwa, Znz ilipopata Uhuru kutoka kwa Uingereza mnamo 10/12/1963, Uhuru huo uliangukia mikononi mwa wakoloni wengine - Waarabu, ndipo sasa mapinduzi yakafanyika kufurusha hao wakoloni wapya😊
 
Hujasema hao weusi wametokea wapi, naona hili swali ni gumu kwako.
Likely, itakuwa ni kutokana na ile 'biashara' ya akina Tiputipu - ukusanyaji wa binadamu toka huko Kigoma, Tabora, Dodoma, nk..
 
Mimi ninachojua tu tuna vyombo vya usalama imara zaidi Africa na ni watu makini mno. Watafuatilia kila move watakayoona itatuletea matatizo huko mbele, iwe kwa waarabu au wachina. Hii no nchi huru, sio koloni.
 
Inawezekana pia kukawa na ndugu zake huko, kama wajomba hivi!

Pia ni kawaida sana kwa wanasiasa wetu kuwa karibu zaidi na watawala wetu (wakoloni). Kambona alipokimbia nchi hakwenda Oman, hivyo hivyo, Samia naye anaweza kukimbilia Oman kuliko kukimbilia Uingereza.
Jf kumbe kuna mabwege sana!
 
Shida inaanzia kwenye shule za kata zinazalisha vijana wenye uelewa mdogo sana mambo though sio wote, vijana wa leo hawafikilii kingine zaidi ya ushabiki na mihemko ya mambo, pia mizizi ya umaskini na kutoka kwenye familia za kichawi inachangia kuwa na vijana ambao upeo wao umeegemea kwenye chuki, husda na wivu.

Angalizo, hivi sasa kuna plotting conspiracy nyingi sana ambavo zinaonekana wazi kumchonganisha Rais as an individual na wananchi wake hivyo vijana tuingalie Tanzania yetu ya kesho, tujitambue na tujue wajibu wetu kwa ajili ya taifa letu
Kiongozi umemaliza. Ubarikiwe sana
 
Mimi ninachojua tu tuna vyombo vya usalama imara zaidi Africa na ni watu makini mno. Watafuatilia kila move watakayoona itatuletea matatizo huko mbele, iwe kwa waarabu au wachina. Hii no nchi huru, sio koloni.
Hahahaa..
Kwamba hao wanausalama wanaweza kutoa maelekezo ya kiweledi kwa mhimili uliojichimbia chini zaidi?!
 
Nimekuwa nikiona Rais wetu akiipa uzito hii nchi ya kuitwa Oman.

Hadi sasa ninachojua tu ni kwamba Zanzibar ilikuwa koloni la Oman na masultani wake walikuwa na asili ya Oman.

Ila leo pia nimeona hii nchi nayo ipo mbioni katika kinyanganyiro cha kujenga Bandari ya Bagamoyo.

Kwa anaejua japo hata kidogo ningependa kujua nini hasa kipo nyuma ya pazia.
Sioni tatizo
 
Unapataje Uhuru kama hujatawaliwa?
Uhuru ni mamlaka na si kutawaliwa,kutawaliwa kupo hadi leo,CCM inatawala Tanzania.
Zanzibar ilipata Uhuru kwa maana ya kupewa mamlaka ya kuongoza kuiendesha nchi yao ,leo Zanzibar haina mamlaka kamili na koti linazidi kuwabana. Koti Made in Tanganyika.
 
kwani historia inasemaje?? hao waarabu wa Oman si ndio walikuwa wanamiliki watumwa Zanzibar na kuwalimisha mashamba?? Ni ndugu yako gani ambae anakugeuza mtumwa na kukuuza arabuni akiwa kakuhasi? Japo Muingereza nae alikuwa na mabaya yake lakini bora alivyokomesha utumwa vinginevyo mpaka 1964 wengi wangekuwa manamba huko visiwani.

Historia ipo tusijifanye hatuijui, hizo ngozi nyeupe hatuna undugu nao walikuja kimaslahi tu.
USA Kuna wamarekani weusi na shida wanazozipitia, vipi kuhusu waarabu weusi Oman wapo? Akili za kuambiwa changanya na za kwako...

Waarabu ni makatili hasa wala siwatetei lakini penye ukweli hatuwezi kupindisha.... Oman haina ubavu wa kututawala ABADANI ....
 
USA Kuna wamarekani weusi na shida wanazozipitia, vipi kuhusu waarabu weusi Oman wapo? Akili za kuambiwa changanya na za kwako...

Waarabu ni makatili hasa wala siwatetei lakini penye ukweli hatuwezi kupindisha.... Oman haina ubavu wa kututawala ABADANI ....
nachosisitiza yaliyopita si ndwele tugange yajayo, kwa vyovyote vile tutachofanya akili iwe kumkichwa hakuna taifa ambalo litakuja tu bila kuangalia maslahi yake, wengi wanaangalia faida watakayopata na ndio maana ni busara kuwabana ili nasi tufaidike, hivyo tuwe makini na mikataba ambayo tutakayoingia nayo ili nchi ifaidike kwanza bila kujali walikuwa ndugu zetu wa damu au wakoloni wetu.

changamoto ni kuwa baadhi ya viongozi wetu wapo kimaslahi zaidi, badala ya kuangalia nchi itafaidika nini wao wanazingatia binafsi watapata nini, sasa hapa tutawalaumu watu weupe mpaka kesho ilhali sisi wenyewe ndio tuna makosa.
 
Kwanini iwe ni kila muomani alihusika na biashara ya utumwa?!!!

Kwani ni kila mmarekani alihusika kuwachukua watumwa Afrika ya magharibi?!!!

Kwani ni kila muingereza alihusika na ukoloni kwa nchi za afrika?!!!

Huko Omani hakukuwa na wananchi wa kawaida wasiohusika na hiyo biashara?!!!

Kama sivyo ,je unawahukumuje waomani wote na biashara hiyo?!!!

Ikiwa utumwa ungalipo huko Oman basi biashara hiyo haijakoma ulimwenguni kote kwani nchi za ulaya ya mashariki na magharibi nao wanaongoza kwa "HUMAN TRAFFICKING...."

N.B Hata waafrika tulichukuana utumwa....isome historia vyema

#Siempre JMT[emoji120]
nachosisitiza ni huu undugu wa damu mnaolazimisha ilhali hakuna ndugu yako wa damu ambae anakufanyia madhila kama yale, vivyo hivyo kwa mzungu n.k wote walikuja kwa faida yao na si kingine. Hivyo kwa chochote tutachofanya tuangalie maslahi ya taifa kwanza, mambo ya undugu tupa kule maana tukichanganya urafiki na biashara tutapata hasara.
 
Hujasema hao weusi wametokea wapi, naona hili swali ni gumu kwako.
Hiyo Oman inawezekana ikawa kama Liberia? Waarabu walipoona hawataki kujihusisha na watu weusi wakawaundia nchi yao, Oman?
Hapana Oman ni Taifa kongwe, source ya watu weusi wa oman ni Ukanda wa pwani ya Afrika mashariki Kuanzia Ethiopia hadi huku kwetu. Kumbuka kuna Kipindi makao makuu ya Oman yalikuwa ni Zanzibar kabla ya kugawanyika kuwa mataifa mawili tofauti.
 
Back
Top Bottom