Ni kheri ufiwe na mzazi kuliko kufiwa na mume/mke

Oh so sad, pole sana kaka.
 
Pole sana mkuu.
Naamin alikuwa rafiki na mshkaji wako sana ndo maana haya yanatokea.
Kikubwa n kumwombea kwa Mwenyezi Mungu ampumzishe salama
Pia jitahid sana kulea hao watoto
 
Nakuelewa sana na ndio maana kwenye comment niliyoweka kwa mtoa post niliweka kigezo cha kama maisha yake ya shule yalikuwa ya boarding school lazima awe na mtazamo huo kwa kuwa mimi pia nimekuwa na maisha hayo kwa kiasi fulani. Hivyo naelewa bond kati ya mtoto na mzazi hufa
 
Umarioo tu unakusumbua. Kwamba mzazi Hana thamani kiasi hicho? Pumbavu kabisa.
Kuna rafiki yangu Fulani tulisoma pamoja O level kitambo alifiwa na mke wake, taarifa nilizipata kwa wakati nikaenda msibani kuzika, yule mwamba alikuwa analia kama mtoto kiasi kwamba nilimsalimia tu na kumuacha hakuwa normal.

Tulivyotoka makaburini kwa sababu kuna watu nawajuwa wa mitaa ile ndio nikafanya udadisi ndio nikapewa mkanda mzima kwamba mwanamke ndio alikuwa kila kitu, amembeba sana mshkaji na mtaani watu wakiwa na shida ya pesa huwa wanakopa kwa huyo Shemeji yangu marehemu, na nikaambiwa Jana jamaa alipelekwa hospitali akawekwa mapumziko na dripu juu, sukari na pleasure vilipanda.

Kwahiyo nakubaliana na hoja yako ukiwa marioo msiba lazima utakusumbuwa kupitia kiasi.

Kuna mwamba mwingine huyo ni wa mtaani kwangu kabisa mke wake alipofariki wote tulijuwa ni lazima amefurahia kifo hicho, maana gwaride alilokuwa anapelekeshwa na mwanamke siyo la dunia hii, halafu mke anajuwa kabisa jamaa ana financial harassment lakini mwanamke haelewi ni gubu hatari.
 
Huna akili
 
Mimi niko tofauti sana na wewe

Heri upoteze wife utaoa mwingne na siyo MAMA
Ni afadhali ukae kimya kuliko kuongea hivi, je watoto wako waisikie kauli kama hii ndugu utawatafuta
 
Upo sahihi chifu. Haiwezekani mwanaume mwenye akili timamu akawaza kwa namna mleta mada alivyowaza. Kama hachezi na akili zetu humu lazima ni paka wa kufugwa ndani huyu.
 
Si uoe mwanamke mwingine umpende kama huyo aliyetangulia.
Mzazi si wa kufananishwa na mtu tu alikuja kwenye maisha yako baada ya kujua$&&) Acha ujinga
 
Ujamuelewa jamaa ajasema Bora kuf nani yaani anazungumzia maumivu baada ya kifo kwamba ukilinganisha Ni Bora maumivu ya mzazi kuliko mke ila sio kwamba wakiwa hai alikuwa ana wish Bora afe mzazi nooh

So hata huyo mwanamke unasema anaona Bora afiwe na mume huenda akifiwa na huyo mume machungu yake ataona Bora maumivu ya kufa mzazi
 
Jambo usilolijua au kulifahamu asilimia kubwa ya wanawake wapo tayari kumpoteza Mume na sio mtoto au mzazi wazazi wake.
Comment Bora ya mwaka 2023, hii iwekwe kwenye Frame kabisa hii hiifadhiwe pasipoweza kufikika kabisa hii na mchangiaji aangaliwe kwa Jicho la pekee
 

Mkuu najua umeandika kwa hisia, kwenye heading kuhusu wazazi umeteleza kidogo, rekebisha…pole sana
 
Soma hapa mkuu

Ni kheri ufiwe na mzazi kuliko kufiwa na mume/mke

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…