Ni kipi humfanya mtu kupata GPA ndogo chuoni? Kati ya mwenye GPA ndogo na kubwa ni yupi ana uwezo mkubwa?

Ni kipi humfanya mtu kupata GPA ndogo chuoni? Kati ya mwenye GPA ndogo na kubwa ni yupi ana uwezo mkubwa?

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7,899
Reaction score
10,415
Kuna watu hapa wana GPA chini ya 3.5 na wengine chini ya 3.8.

Jambo hili linawafanya wengi wao kukosa baadhi ya nafasi za kazi.

Sasa je ni kipi husababisha mtu kupata GPA ndogo.

Na je kati ya mwenye GPA ndogo na kubwa ni yupi anauwezo mkubwa?
 
GPA haimfanyi mtu kupata kazi gpa huwa wanaitumia tu kufanya mchujo wa awali wapate watu wachache watakaowafanyia written na kisha oral interview.

Nina jamaa yangu amepata kazi kampuni kubwa ya kiserikali na alikuwa na gpa chini ya 3.5 kumbuka walipotangaza nafasi ta kazi kigezo kilikuwa gpa ya 4.0 kwenda juu.
 
GPA haimfanyi mtu kupata kazi gpa huwa wanaitumia tu kufanya mchujo wa awali wapate watu wachache watakaowafanyia written na kisha oral interview .

Nina jamaa yangu amepata kazi kampuni kubwa ya kiserikali na alikuwa na gpa chini ya 3.5 kumbuka walipotangaza nafasi ta kazi kigezo kilikuwa gpa ya 4.0 kwenda juu.
Sasa mbona aliingizwa wakati hakua na qualifications za hiyo kazi?
 
Sasa mbona aliingizwa wakati hakua na qualifications za hiyo kazi?
Gpa ilitumika kuwafanyia early vetting mzee ( kuwaogopesha tu mambo yasiwe mengi ) watu wasio wengi yeye akafanya ku apply basi tu ila sasa akaitwa akapiga written na oral hapo ana compete na walio na 4.0 + gpa na akapata .

Kikubwa ukiona kazi kigezo ni gpa nabhauna kigezo cha gpa we apply tu maana mara nyingi huwa hawaiangalii hiyo gpa kazini wanataka ujuzi wako na uwepesi wako wa kujifunza mambo mengi.
 
Course work. Hizi ndo chanzo kikubwa cha wengi kupata matokeo gpa ndongo. Mfano mtu maxs za quiz haupo, attendance haupo, group work tia tia maji wote mnategea. Individual assignment una copy google mwisho wa siku unapata Course ya 19 kati ya 40. Final exam maswali 5 unahuakika wa maswali mawili tena maswali yenyewe ni yale ya kupunguza sup mwisho wa siku lzm tu gpa itakua ndongo
 
Kuna watu hapa wana GPA chini ya 3.5 na wengine chini ya 3.8.

Jambo hili linawafanya wengi wao kukosa baadhi ya nafasi za kazi.

Sasa je ni kipi husababisha mtu kupata GPA ndogo.

Na je kati ya mwenye GPA ndogo na kubwa ni yupi anauwezo mkubwa?
Uwezo wa nini?
Kuwa na GPA kubwa inaweza kuonyesha uwezo ki taaluma,kama GPA hizo zimepatikana bila magumashi,ila kama imepatikana ki magumashi,sio chochote,
Wakati Bado nimeajiliwa tulikuwa na ma "engineer"kutoka vyuoni wenye shahada za mechanical engineering,lakini walikuwa hawana uwezo wa kufungua engine ya gari na kufanya matengenezo!kazi zilikuwa zinafanywa na kijana wa VETA Tena std 7!!
Kwa sasa hv GPA kubwa ,ndogo,sio uthibitisho kama unajua kitu!!
Elimu ni performance,unaweza kufanya nini?kama ulichosomea huwezi kujifanya,sasa hizo GPA za kujibia mitiani,hazina maana
 
Kuto ku concentrate na shule, na kutokuwa makini ndo kunasababisha watu kupata GPA ndogo. Vijana wengi wakifika chuo wanaacha kilicho wapeleka na kuanza mambo mengine kama ujasiriamali, kazi, ubishoo, mapenzi n.k. mambo haya huwafanya washindwe ku concentrate na shule hivyo kujikuta hawaingii darasani kusikiliza walimu, au hata wakiwa darasani hawa concentrate kusikiliza mwalimu.

Hushindwa kufanya assignment kwa wakati na hivyo kujikuta wanalipua assignment na kupata course work ndogo.

Wengine wanajikuta wakikosa msukumo wa kusoma kwa bidii kutokana labda na hali za kiuchumi na kukata tamaa.

Ukiongea na vijana wengi ni kama wanataka cheti tu. Utasikia wakijiaifu mimi ninachotaka ni cheti tu. Baada ya kumaliza ndo hugundua kuwa walifanya kosa sana kutokuwa makini na shule na hatimaye kupata GPA ndogo.

Ila wengine ni uwezo wao mdogo. Akili ina levels..kuna watu wanafanya vizuri shule ya msingi na kufanikiwa kwenda secondary..ila wakifika sekondari wanajikuta wana changamoto kubwa ya kuelewa..hata kama wakisoma na kukesha.

so kuna wale levels zao zinaishia kidato cha sita, ingawa hupata nafasi ya kwenda chuo lakini hawezi kufanya vizuri.
 
Tambua hili mfano mwenzio ana GPA ya 2.7 wewe una 4.2 ukienda pale utumishi kama sio zile kazi za kuwa mkufunzi ,hizi za gombania goli tambua kufanya vizuri interview kutakupa nafasi .

Tambua interview nyingi ni kama zali unaweza ukawa na GPA kuwa ila sio smart ukafeli mtihani mdogo hata oral usifike...Hapa kweny kufeli Kuna mengi sana unaweza usimalize mtihani basi ushalost mwenzio kapasua, mwisho wa siku yuko kazini ndo anaanza kushika pesa ndefu wewe bado unazunguka tu kitaa.

Unaweza kuwa na GPA kubwa ila uwezo wa kujieleza kweny interview ni chenga , kiujumla hauna confidence ukapitwa ..Wapo Wanajua kuandika wako fresh ila kuongea kingereza ni chenga..

Mimi nimesoma na mkenya alipata form ila alikuwa yuko mbele kweny debate zote tangu form one yaani kuongea ni mjanja, akaenda diploma mambo ya afya...Jamaa yuko NGO'S moja walikuja fanyiwa interview akapita na mpaka nakuambia ana masters alijiendeleza degree mpaka masters kitambo sana..Tatizo lake kubwa hesabu hapatani nazo kabisa alikula F😂😂😂
 
Tambua hili mfano mwenzio ana GPA ya 2.7 wewe una 4.2 ukienda pale utumishi kama sio zile kazi za kuwa mkufunzi ,hizi za gombania goli tambua kufanya vizuri interview kutakupa nafasi .

Tambua interview nyingi ni kama zali unaweza ukawa na GPA kuwa ila sio smart ukafeli mtihani mdogo hata oral usifike...Hapa kweny kufeli Kuna mengi sana unaweza usimalize mtihani basi ushalost mwenzio kapasua, mwisho wa siku yuko kazini ndo anaanza kushika pesa ndefu wewe bado unazunguka tu kitaa.

Unaweza kuwa na GPA kubwa ila uwezo wa kujieleza kweny interview ni chenga , kiujumla hauna confidence ukapitwa ..Wapo Wanajua kuandika wako fresh ila kuongea kingereza ni chenga..

Mimi nimesoma na mkenya alipata form ila alikuwa yuko mbele kweny debate zote tangu form one yaani kuongea ni mjanja, akaenda diploma mambo ya afya...Jamaa yuko NGO'S moja walikuja fanyiwa interview akapita na mpaka nakuambia ana masters alijiendeleza degree mpaka masters kitambo sana..Tatizo lake kubwa hesabu hapatani nazo kabisa alikula F😂😂😂
Nimefanyia watu interview nyingi mno na nimefanya kazi na watu wengi. Sijawahi kupata GPA ya 4 ikaniangusha kwenye kazi. In most cases 99% GPA kubwa ina maanisha mtu ana uwezo mkubwa..katika theory na kazi. Ana analytical and thinking capacity kubwa kitu ambacho ni adimu sana kwa vijana wa kitanzania
 
Nimefanyia watu interview nyingi mno na nimefanya kazi na watu wengi. Sijawahi kupata GPA ya 4 ikaniangusha kwenye kazi. In most cases 99% GPA kubwa ina maanisha mtu ana uwezo mkubwa..katika theory na kazi. Ana analytical and thinking capacity kubwa kitu ambacho ni adimu sana kwa vijana wa kitanzania
Kwa asilimia kubwa hata pale utumishi vile vimtihani wanapiga fresh ..Ishu ni ile unakuta siku umeenda kombo mambo sio fresh ..

Licha ya elimu yetu kuwa na mapungufu ila kwa aliyefaulu vizuri anakuwa ni smart hata kiakili kwa asilimia kubwa nimeona.

Ukija kweny utendaji wa kazi hamna maajabu kawaida sana ...Ndo maana hata wapiga kazi wengi ofisini ni level ya diploma wanakuwa active na uchapaji kazi
 
Gpa ilitumika kuwafanyia early vetting mzee ( kuwaogopesha tu mambo yasiwe mengi ) watu wasio wengi yeye akafanya ku apply basi tu ila sasa akaitwa akapiga written na oral hapo ana compete na walio na 4.0 + gpa na akapata .

Kikubwa ukiona kazi kigezo ni gpa nabhauna kigezo cha gpa we apply tu maana mara nyingi huwa hawaiangalii hiyo gpa kazini wanataka ujuzi wako na uwepesi wako wa kujifunza mambo mengi.
Uko sawa kabisa mie nakumbuka nilipohitimu kidato cha sita nilibahatika kupata ajira Mgodini kampuni kubwa tu hapa Tanzania, niliingia kama mine trainees ( Mchimbaji mwanafunzi) nilikaa kwenye hiyo kazi mda tu huku najipanga kurudi shule siku moja nikaona tangazo la kazi humo ndani ya kampuni vigezo wanahitaji mtu aliyesomea Mine engineer, duh mie nikaona isiwe shida acha niombe tu wakiniita nitajaribu maana kigezo kingine uwe mzuri kwa hisabati na mie kwawakati huo nilikua sijambo kweli kwenye hisabati na ukizingatia bado shule haijaisha kichwani kipindi hiko Mungu si abdallah kikaitwa kufanya usahili tukiwa watu Hamsini na nafasi taraji ni sita tu ajabu nilipambana nikawashinda mpaka waliokuwa na vigezo zaidi yangu kumbe mie ndio nilijibu maswali yote kwaufasaha zaidi, Unajua ukikuta usahili anafanyisha mtu kutoka nje ya nchi unaweza kufurahia sana hakuna longolongo kama Watanzania wenzetu, Hivyo kijana jiamini tu unapoona nafasi ya kazi na sifa angalau unaendana nazo jaribu mengine makaratasi tu wala yasije kukutisha.
 
Uko sawa kabisa mie nakumbuka nilipohitimu kidato cha sita nilibahatika kupata ajira Mgodini kampuni kubwa tu hapa Tanzania, niliingia kama mine trainees ( Mchimbaji mwanafunzi) nilikaa kwenye hiyo kazi mda tu huku najipanga kurudi shule siku moja nikaona tangazo la kazi humo ndani ya kampuni vigezo wanahitaji mtu aliyesomea Mine engineer, duh mie nikaona isiwe shida acha niombe tu wakiniita nitajaribu maana kigezo kingine uwe mzuri kwa hisabati na miraba kwawakati huo nilikua sijambo kweli kwenye hisabati na ukizingatia bado shule haijaisha kichwani kipindi hiko Mungu si abdallah kikaitwa kufanya usahili tukiwa watu Hamsini na nafasi taraji ni sita tu ajabu nilipambana nikawashinda mpaka waliokuwa na vigezo zaidi yangu kumbe mie ndio nilijibu maswali yote kwaufasaha zaidi, Unajua ukikuta usahili anafanyisha mtu kutoka nje ya nchi unaweza kufurahia sana hakuna longolongo kama Watanzania wenzetu, Hivyo kijana jiamini tu unapoona nafasi ya kazi na sifa angalau unaendana nazo jaribu mengine makaratasi tu wala yasije kukutisha.
Ajira ni mpango wa Mungu kijana wala usijisifu. Ila mwenye A na GPA zake ndio mwenye uwezo kukuzidi. Wote wanaokuongoza katika taifa hili fuatilia ufaulu wao, hakuna mbumbu wote wamekula vitabu na wana GPA kubwa. Ni mmoja mmoja wasio na good education track record.
 
Ajira ni mpango wa Mungu kijana wala usijisifu. Ila mwenye A na GPA zake ndio mwenye uwezo kukuzidi. Wote wanaokuongoza katika taifa hili fuatilia ufaulu wao, hakuna mbumbu wote wamekula vitabu na wana GPA kubwa. Ni mmoja mmoja wasio na good education track record.
Duh! pole sana hivi unajua hata hii elimu tunayoisoma walioleta hawakuwa na hii mambo unayoona ya maana? Watu walioleta hii elimu hawakusoma pahala popote mbali walikua na akili tu hivyo kumbuka ndugu kuna tofauti kati ya kusoma na akili, maana mtu anaweza kuwa kasoma sana tu lakini akakosa akili japo kuna ufungamani kidogo kati ya akili na elimu, akili mtu huzaliwa nayo na hauwezi kuihuisha kwa mwingine isipokuwa elimu ndio hufanywa hivyo na si akili
 
Back
Top Bottom