Nilishawahi kuajiriwa na muhindi mmoja kama project manager. Ali apply tender iliyohusisha kuweka signage (mabango) nchi nzima kutoka kampuni moja maarufu ya Makaburu (South Africans). Kipindi hicho ilikuwa project yenye thamani ya kama $100,000.
Kabla ya kupata tender kulikuwa na bidding ambapo moja ya sharti ilikuwa ni kuwakilisha installation plan (proposal) iliyohusisha uchambuzi wa matumizi ya budget, utekelazaji wa kazi mpaka kukamilika kwake.
Nilifanya kazi ya kuandaa plan wiki 2 nzima usiku na mchana maana ilikuwa inahitajika haraka. Ilipotimia na kuwakilishwa muhindi akashinda tender.
Ilipoidhinishwa tu kuwa kashinda jamaa akaniambia kuna muhindi mwenzie toka India (expatriate) atasimamia hiyo project (kutumia plan yangu), moja ya makubaliano yetu ya awali ilikuwa nitaisimamia mimi hiyo project yote endapo proposal yangu itapita.
Aliposema mambo ya expatriate tu nikatoa notice yangu ya mwezi mmoja ya kuacha kazi.
Kipindi nataarisha plan ya hiyo project nilifanya research ya kutosha nikijua nitasimamia mimi mwenyewe hivyo niliweza kuhalalisha baadhi ya matumizi ya budget nikijua nitafanikisha vipi baada ya research yangu.
Phase ya kwanza ya project ilianzia mikoa ya Tanga, Arusha na Moshi. Muhindi alipopewa mzigo installation ianze akachemka baada ya kumaliza Tanga tu. Pesa ilikata na kazi hata robo haijaisha.
Kila sehemu ilikuwa na time limit kama ilivyoanishwa kwenye proposal plan, muhindi alichemka phase ya kwanza tu huku ikiwa keshachukuwa advance ya Mkaburu.
Nilifanya presentation mimi mwenyewe kwenye bidding kwa niaba ya muhindi, hivyo sharti aliliopewa na makaburu ni kuwa aliendaa na kufanya presentation ya proposal ndio asimamie project la sivyo atanyang'anywa kazi.
Ilibidi muhindi anitafute tukae chini tena akiahidi offer kubwa kulinganisha na ya awali. Nilimkatalia na wakati huo huo nili apply kivyangu kwa makaburu wanipe project mimi kama mimi.
SIkuwa na kampuni yangu hivyo ile project ikahamishiwa kuwa in house project kumaanisha walianzisha kitengo maalum cha signage ndani ya kampuni yao kuanzia production mpaka installation na mimi nikapewa hicho kitengo kukisimamia. Hivyo badala ya Project Manager nikawa Division Manager.
Kwa ile phase ya kwanza ilimlazimu muhindi kumaliza na ilibidi areport kwangu moja kwa moja kwa niaba ya kaburu, karma is real.
Sehemu ya kazi iliyobaki iliisha kwa wakati na mpaka sasa kupitia hiyo project kitengo cha signage kwenye kampuni ya kaburu kimekuwa one of the leading signage companies kwa Tanzania.
Katika maisha chochote kinachopaswa kuwa chako kitakuwa chako tu haijalishi kitachelewa kwa kiasi gani.