Ni kisa au mkasa gani uliwahi kufanyiwa na ndugu au mtu wako wa karibu?

Ni kisa au mkasa gani uliwahi kufanyiwa na ndugu au mtu wako wa karibu?

Watu tukiwaambia kuna wazee aidha wanabagua au hawawapendi watoto wao, hawaelewi.

Huwa nikikaa nikifuatilia mambo yanayotokea nahisi mzee wangu hakutaka niwe na nafasi fulani, Mungu alivyo fundi sasa kati ya watoto wake wote mimi ndio nina kiajira japo uchwara.
wewe ni mimi kabisa. ila nshamsamehe
 
Sitosahau mwaka 2021 nikiwa Arusha kwa ndugu nilifukuzwa Usiku wa saa tatu kisa sijaosha vyombo vya ndani aisee niliumia sanaa kama nisingekuwa najuana na majirani siku hiyo ningelala kwenye mitalo, nilienda kwa jirani nikapokelewa next day nikakata ticket ya kurud nyumban.

Secondly 2018 nikiwa form two nilikua naishi kwa ndugu yangu but alinipa chumba na akanambia nijitegemee Yani niwe najipikia nk na chumba alicho nipa nilikua nakilipia mwisho wa mwezi lakin funguo alikua anazimiliki yeye maana chumba kilikua ndani ya nyumba ambayo alikua akiish,, basi ikaja likizo ya mda mfupi nikarudi home vtu vyangu pamoja na vyomb nikaviacha, baada ya likizo nikarudi nikakuta chumba hakina vitu vyangu kina vitu vingne, kumbe yule mama kachukua vyombo vyangu pamoja Vitabu vyangu akaenda kutupa kwenye Banda la mbwa na kilicho niuma zaidi sufuria ambazo nilikua natumia akawa ndo anatumia yeye kurishia mbwa wake, aisee niliumia mno nikataman niache shule kabisa ila namshukuru Mungu alinisaidia alinipa moyo wa uvumilivu.

Kiufupi kuish kwa Ndugu changamoto sana labda upate ndugu mwenye moyo mzuri

Safari yangu ya Maisha Bado sana ndo kwanza naanza Mungu azidi kunitetea na kunipa moyo wa Uvumilivu.
 
Tukio kubwa nalokumbuka ndugu kugoma kunilipia ada baada ya baba kufariki pamoja na kuwa waliuza nyumba yetu hatukuambulia hata mia
Nakumbuka nilimpigia simu babamdogo kumuomba ada akasema hatoi pesa had aende kijijini ndo waamue ikawa mara ya mwisho kuongea nae nikanusurika kuacha shule nikiwa kidato Cha pili, ikabidi nisomeshwe na wasamaria wema kama yatima na wakat sikuzaliwa kwenye familia ya kichovu ila Mungu ni mwema
Walinifundisha maisha nilikuwa strong nikiwa mdogo sana..🙏
Iam deeply sorry, y'al😐
 
Nilishawahi kuajiriwa na muhindi mmoja kama project manager. Ali apply tender iliyohusisha kuweka signage (mabango) nchi nzima kutoka kampuni moja maarufu ya Makaburu (South Africans). Kipindi hicho ilikuwa project yenye thamani ya kama $100,000.

Kabla ya kupata tender kulikuwa na bidding ambapo moja ya sharti ilikuwa ni kuwakilisha installation plan (proposal) iliyohusisha uchambuzi wa matumizi ya budget, utekelazaji wa kazi mpaka kukamilika kwake.

Nilifanya kazi ya kuandaa plan wiki 2 nzima usiku na mchana maana ilikuwa inahitajika haraka. Ilipotimia na kuwakilishwa muhindi akashinda tender.

Ilipoidhinishwa tu kuwa kashinda jamaa akaniambia kuna muhindi mwenzie toka India (expatriate) atasimamia hiyo project (kutumia plan yangu), moja ya makubaliano yetu ya awali ilikuwa nitaisimamia mimi hiyo project yote endapo proposal yangu itapita.

Aliposema mambo ya expatriate tu nikatoa notice yangu ya mwezi mmoja ya kuacha kazi.

Kipindi nataarisha plan ya hiyo project nilifanya research ya kutosha nikijua nitasimamia mimi mwenyewe hivyo niliweza kuhalalisha baadhi ya matumizi ya budget nikijua nitafanikisha vipi baada ya research yangu.

Phase ya kwanza ya project ilianzia mikoa ya Tanga, Arusha na Moshi. Muhindi alipopewa mzigo installation ianze akachemka baada ya kumaliza Tanga tu. Pesa ilikata na kazi hata robo haijaisha.
Kila sehemu ilikuwa na time limit kama ilivyoanishwa kwenye proposal plan, muhindi alichemka phase ya kwanza tu huku ikiwa keshachukuwa advance ya Mkaburu.

Nilifanya presentation mimi mwenyewe kwenye bidding kwa niaba ya muhindi, hivyo sharti aliliopewa na makaburu ni kuwa aliendaa na kufanya presentation ya proposal ndio asimamie project la sivyo atanyang'anywa kazi.

Ilibidi muhindi anitafute tukae chini tena akiahidi offer kubwa kulinganisha na ya awali. Nilimkatalia na wakati huo huo nili apply kivyangu kwa makaburu wanipe project mimi kama mimi.

SIkuwa na kampuni yangu hivyo ile project ikahamishiwa kuwa in house project kumaanisha walianzisha kitengo maalum cha signage ndani ya kampuni yao kuanzia production mpaka installation na mimi nikapewa hicho kitengo kukisimamia. Hivyo badala ya Project Manager nikawa Division Manager.

Kwa ile phase ya kwanza ilimlazimu muhindi kumaliza na ilibidi areport kwangu moja kwa moja kwa niaba ya kaburu, karma is real.

Sehemu ya kazi iliyobaki iliisha kwa wakati na mpaka sasa kupitia hiyo project kitengo cha signage kwenye kampuni ya kaburu kimekuwa one of the leading signage companies kwa Tanzania.

Katika maisha chochote kinachopaswa kuwa chako kitakuwa chako tu haijalishi kitachelewa kwa kiasi gani.

Ila Sijui wahindi wanashida gani,

Kuna skin Product na import kutoka India, week kadhaa zilizopita nikapata ujio wa muhindi ofisini kwangu, akidai namuharibia soko kwa kuingiza bidhaa aliyokua anaingiza yeye.

Hivyo nikimaliza mzigo ni lazima nichukue kwake la sivyo atanipeleka polisi.

Ajabu ni kwamba Bei anayoniuzia kwa 500pcs ni Bei nnayouza kwa mteja wa less than 6pcs

Sasa nimekataa ananifata anaomba tufanye Kazi pamoja..
Kwa kweli nimekataa kata kata.
 
Sitosahau mwaka 2021 nikiwa Arusha kwa ndugu nilifukuzwa Usiku wa saa tatu kisa sijaosha vyombo vya ndani aisee niliumia sanaa kama nisingekuwa najuana na majirani siku hiyo ningelala kwenye mitalo, nilienda kwa jirani nikapokelewa next day nikakata ticket ya kurud nyumban.

Secondly 2018 nikiwa form two nilikua naishi kwa ndugu yangu but alinipa chumba na akanambia nijitegemee Yani niwe najipikia nk na chumba alicho nipa nilikua nakilipia mwisho wa mwezi lakin funguo alikua anazimiliki yeye maana chumba kilikua ndani ya nyumba ambayo alikua akiish,, basi ikaja likizo ya mda mfupi nikarudi home vtu vyangu pamoja na vyomb nikaviacha, baada ya likizo nikarudi nikakuta chumba hakina vitu vyangu kina vitu vingne, kumbe yule mama kachukua vyombo vyangu pamoja Vitabu vyangu akaenda kutupa kwenye Banda la mbwa na kilicho niuma zaidi sufuria ambazo nilikua natumia akawa ndo anatumia yeye kurishia mbwa wake, aisee niliumia mno nikataman niache shule kabisa ila namshukuru Mungu alinisaidia alinipa moyo wa uvumilivu.

Kiufupi kuish kwa Ndugu changamoto sana labda upate ndugu mwenye moyo mzuri

Safari yangu ya Maisha Bado sana ndo kwanza naanza Mungu azidi kunitetea na kunipa moyo wa Uvumilivu.
KAZA WEWEEEE!
 
Ndugu yangu wa mbali kaja mjini kakaa kwangu miezi 2. Cha ajabu alivyoondoka kaenda kunianika kijijini kuwa tunakula wali maharage Kila siku jioni....na Dagaa kabichi mchana na kwamba wife atakua mchoyo!
Ndugu wa hovyo wapo kila ukoo
 
Ila Sijui wahindi wanashida gani,

Kuna skin Product na import kutoka India, week kadhaa zilizopita nikapata ujio wa muhindi ofisini kwangu, akidai namuharibia soko kwa kuingiza bidhaa aliyokua anaingiza yeye.

Hivyo nikimaliza mzigo ni lazima nichukue kwake la sivyo atanipeleka polisi.

Ajabu ni kwamba Bei anayoniuzia kwa 500pcs ni Bei nnayouza kwa mteja wa less than 6pcs

Sasa nimekataa ananifata anaomba tufanye Kazi pamoja..
Kwa kweli nimekataa kata kata.
Tatizo kubwa la wahindi ni kudharau uwezo wa kiakili wa watu weusi. Siku zote wanaamini mtu mweusi ni wa kuburuzwa. Hata ikitokea akakubali ufanisi wako atahakikisha anamuweka muhindi mwenzie karibu ili achukue ujuzi wako na mwisho wa siku akutimue pale anapokosa haja na wewe.
 
Sometimes watu wakiishi wenyewe wanaitwa wabinafsi. Ila inakuepusha na mengi kwa kweli. Ila yaliyonipata kwa so called ndugu na watu wa karibu hakika mengine nitaenda nayo kaburini. Naamini nafsi yangu itapona hata kama ni uzeeni [emoji119]
 
Habari za muda huu wapendwa

Bila shaka kwenye safari ya maisha kila mmoja wetu amewahi kukumbana na visa na mikasa mbali mbali kwenye purukushani za maisha

Mikasa ambayo imekuwa ikitupa mafunzo na mafundisho maishani mwetu na wakati huo huo kubadilisha kabisa mitazamo ya maisha yetu juu ya watu.

Watu wetu wa karibu ni watu tunaowategemea kwenye maisha yetu Kwa mambo mbali mbali lakini pia watu hao hugeuka na kutuletea vilio vya kudumu vyenye machungu maishani mwetu.

Je umewahi kufanyiwa mkasa, kisa au tukio Gani baya na ndugu au mtu wako wa karibu?

Mimi niliwahi kuchomewa utambi kazini na mtu wangu wa karibu...ambaye nilikuwa na share mambo yangu kibao na hata niliwahi kumpa mtaji wa biashara, lakini kumbe alikuwa anachukia mafanikio yangu tangia hapo nikabadilisha kabisa mtazamo wangu juu ya marafiki na watu wangu wa karibu. Kwa kifupi nikawa na chujio mdomoni mwangu na kichwani mwangu.
Kuna jamaaa mmoja alifukuzwa geto sekondari na wenzake hakua na msosi Wala Kodi ya nyumban mm niko kidato Cha pili yeye Cha tatu, nikamulea Hadi akamaliza shulen vizuri, siku ya mwisho nikamuomba aniachie vitabu akaomba hela, nikawa Sina, akapata kazi baadae Mambo mazuri nikwa na mm namishe kidogo nikamwambia nipo hapa Arusha vipi nikuone ndugu tusalimiane hajkujibu chochote. Akabadilishwa kituo Cha Kaz akaja mkoa nilipo akaletwa anatafuta nyumban ya kupanga kabla ya salamu akaniomba msamaha.
 
Kuna jamaaa mmoja alifukuzwa geto sekondari na wenzake hakua na msosi Wala Kodi ya nyumban mm niko kidato Cha pili yeye Cha tatu, nikamulea Hadi akamaliza shulen vizuri, siku ya mwisho nikamuomba aniachie vitabu akaomba hela, nikawa Sina, akapata kazi baadae Mambo mazuri nikwa na mm namishe kidogo nikamwambia nipo hapa Arusha vipi nikuone ndugu tusalimiane hajkujibu chochote. Akabadilishwa kituo Cha Kaz akaja mkoa nilipo akaletwa anatafuta nyumban ya kupanga kabla ya salamu akaniomba msamaha.

Msela mafiii huyo na mbinafsi
 
Back
Top Bottom