Ni kisa au mkasa gani uliwahi kufanyiwa na ndugu au mtu wako wa karibu?

Ndugu yangu wa mbali kaja mjini kakaa kwangu miezi 2. Cha ajabu alivyoondoka kaenda kunianika kijijini kuwa tunakula wali maharage Kila siku jioni....na Dagaa kabichi mchana na kwamba wife atakua mchoyo!
Wamekupa likes za bure lakini huyo ndugu yako ni mtu mzuri sana. Ni mkweli. Ulitaka aseme unakula kuku na ngombe kila siku wakati siyo kweli? Huoni angekuchongea kwa ndugu zako na wangetaka ''uwapunguzie'' raha zako? Au siku akija ndugu mwingine na akute unakula maharage na kabeji kila siku na huku huyu alisema vingine, angedhani umeamua kumkomoa?
 
Looooh[emoji23]
 
Inategemea ntu na ntu,

Binafsi nimeishi na watu ndugu/sio ndugu fresh tu,

Na home tumeishi na watu hasa vijana na wana maisha yao sasa MashaaAllah,na mama ni kama mama yao sasa,

Unajua nini??? Chakula,chakula,chakula.shida inaanzia hapa.
 
Duh pole nyie,watu km hao ndo wanasababisha tusipate connections
 
Hahaha hajasema uwongo of course. Ila ni kama ananinanga fulani. Pia lile pilau la Kila jumapili ambalo sio la maharage hajalisema.
 
Nimekosa double like...hongera sana champ
 
Mi nililogwa na mtu niliyekuwa namstahi na kumfadhili kwenye mambo mbalimbali ilikuwa kidogo nilale mavumbini ila Mungu mwema alinipigania na kunitoa kwenye kamba za Mauti.
Adui zetu hawatoki mbali
 
Mpeleke yeye Polisi kwa kukutishia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…