Mzee Mohamed ungekuwa na uwezo ungetaka iandikwe kwamba Sykes ndo alipambania uhuru kuliko hata Nyerere. Siku moja kubali tu kuwa Nyerere alikuwa mbali sana kifikra kuliko Sykes na wazee wengine wa Kariakoo. Hatumdharau Sykes ila ndo uwezo wake ulipokuwa umefikia kina Mwalimu Nyerere wakaanzia pale alipoishia yeye.
Mama...
Mimi nitakuwa mjinga sana kama nitapuuza uwezo wa Mwalimu Nyerere.
Kwanza fikiria uwezo watu hawa ambao ndiyo walikuwa ndani ya TAA Political Subcommittee mwaka wa 1950: Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Steven Mhando na John Rupia.
Mshauri wa hii kamati akiwa Earle Seaton.
Sijui kama wewe unajua uwezo waliokuwanao watu hawa.
Hawa ndiyo walikuwa wanapanga mipango ya kuikomboa Tanganyika na hawa ndiyo waliomtia Nyerere katika uongozi wa juu wa TAA.
Kwa kipande hiki cha historia kinaonyesha uwezo mkubwa wa Mwalimu Nyerere.
Swali langu kwako ni hili.
Wewe ulikuwa unawajua hawa niliokutajia kuwa walipigania uhuru wa Tanganyika?
Mimi nimenyanyua kalamu kusahihisha historia iliyokuwa inamtaja Nyerere peke yake na kueleza historia ya TANU kama ilivyotakiwa kuandikwa.
Kubwa na hili ndilo wengi hapa linawaumiza ni kutaja mchango wa Waislam na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika kupigania uhuru.
Mufti Sheikh Hassan bin Ameir akiuza kadi za TANU misikitini na aliwaongoza Waislam kumuunga mkono Julius Nyerere.
Je, wewe hupendi haya yakaelezwa katika historia ya uhuru?
Hakuna mahali unaweza kusema hawa wazalendo waliishia hapa katika kudai uhuru na Nyerere akaanzia hapa.
Hawa na wazalendo wengine walikuwapo na Nyerere toka walipompokea 1952 hadi uhuru unapatikana 1961.
Nyerere angekuwa mbali sana angeunda TANU nje ya watu hawa na labda angeunda chama chake.
Lakini Nyerere kamkuta Abdul na wenzake katika harakati za uhuru katika African Association (1929) na Al Jamiatul Islamiyya (1933) iliyoundwa na baba yake.
Iweje historia hii ifutwe?
Unaweza vipi kuwafuta wazalendo hawa katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ukambakisha Nyerere peke yake?
Sikuandika kitabu kumdogosha Nyerere.
Nimeandika kitabu kusahihisha historia iliyojaa makosa mengi sana.
Hii ndiyo sababu Prof. Haroub Othman alimshauri Mwalimu akubali iandikwe historia ya maisha yake ipatikane nafasi ya kufanya marekebisho ya historia iliyokuwapo ambayo kitabu cha Abdul Sykes iliibomoa.
Unasema ningekuwa na uwezo?
Uwezo ninao na umetambulika.
Kleist Sykes ametiwa katika Dictionary of African Biography (DAB) Oxford University Press, New York 2011.
Kitabu nilichoandika "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968)," Minerva Press London 1998 kimechapwa matoleo manne tunakwenda la tano na kipo kwa Kiswahili pia Phoenix Publishers, Nairobi 2002.
Niko hapa JF sasa mwaka wa 11 nafundisha historia hii.
Kimeandikwa kitabu cha Nyerere (2020) nimeshirikishwa na nimenukuliwa sana ndani ya kitabu hicho.
Mahojiano na TBC kuhusu Nyerere Biography