naona hizi takataka zimejaa huko ulikodhihifadhi, na unaamua kuzileta hapa jukwaani.
Kalamu,
Nina maktaba kubwa sana ya picha zangu binafsi kuanzia niko mtoto wa miaka 2 hadi hivi sasa mzee wa miaka 71.
Picha nilizopiga katika safari zangu katika nchi nyingi nilizotembelea duniani.
Nina picha pia za harakati za uhuru ambazo nimekusanya kutoka sehemu mbalimbali za Tanganyika.
Nashukuru kuwa baada ya kufahamika siku hizi naletewa picha na wasomaji wangu hapa JF.
Picha hizi zote ni "catalogued."
Ford Foundation walihusika katika uasisi wa Nyerere Foundation na mtu wao aliyekuja Tanzania kusaidia kuundwa kwa NF aliniomba niipatie NF picha nilizokuwanazo.
Nilifanya hivyo.
Ninazo pia picha kutoka Bailey Collection Johannesburg.
Hizi alinipa Jim Bailey mwenyewe wakati nikihariri kitabu chake cha picha kuhusu Julius Nyerere.
Nina picha kutoka Maktaba ya Mohamed Shebe mpiga picha wa kwanza wa TANU na Julius Nyerere.
Mohamed Shebe alinipiga mimi picha yangu ya kwanza 1953.
Studio yake ilikuwa Mtaa wa Livingstone na Kipata mkabala na nyumba aliyokuwa akiishi mama yangu mkubwa.
Mzee Shebe akiniita mimi rafiki yake.
Ni kisa kirefu na nimekiandika.
Baadhi ya wasomaji hapa wameziona picha za Mzee Shebe alizopiga katika mikutano ya kwanza ya TANU 1954.
Nitaziweka hapa In Shaa Allah kwa faida ya historia ya nchi yetu.