Ni kwanini amri ya kuiabudu siku ya sabato tangu enzi za Musa hadi sasa ni jumamosi lakini makanisa mengine huabudu jumapili?

Ni kwanini amri ya kuiabudu siku ya sabato tangu enzi za Musa hadi sasa ni jumamosi lakini makanisa mengine huabudu jumapili?

Ndiye

Musa aliepewa amri 10 kutuletea, akiwa huko patakatifu, alielekezwa sabato iwe jumamosi na ikawa hivyo
Yesu aliulizwa na mafarisayo hilo swali,akajibu akasema "Yeye ndiye Bwana wa sabato".
Nikipata mstari naleta hapa.
Ukielewa hii sentensi umepata jibu .
 
Hata Yesu aliikuta siku maalum ya sabato, aliiabudu, kuisifia na kuitetea (marko 2) na miaka nenda eudi mpaka leo hii utaratibu ni huo ilikoanzia Israel, ni kipi cha kubadili ?
Yesu aliivunja sabato, akasema je ni yupi Kati yenu mwenye ng'ombe ambaye akitumbukia shimoni atamuacha mpaka sabato iishe? 😀😀😀Wayahudi walisema wanafunzi wake wanakula siku ya sabato
 
Yesu aliivunja sabato, akasema je ni yupi Kati yenu mwenye ng'ombe ambaye akitumbukia shimoni atamuacha mpaka sabato iishe? 😀😀😀Wayahudi walisema wanafunzi wake wanakula siku ya sabato
Aliiweka sawa sabato, Mafarisayo walijianzishia sheria zao za ziada kwamba hata ukiona mtoto wako ama mfugo wako unazama hutakiwi kuuokoa kwa kisingizio kwamba ni kushughulisha mwili, Sabato inahusu kuweka kando shughuli zako unazofanya lakini sio kukwepa kujishughulisha kabisa kiasi cha kushindwa kuokoa hata maisha ya mwanadamu ama mnyama.

Soma Marko 2, Yesu aliitambua, aliiabudu, aliisifia na kuitetea Sabato
 
Je unaishika kulingana na torati?
Kuna baadhi ya Mazingira ni tofauti na agano la kale

Mfano kitabu cha Kutoka wayahudi walipewa mtihani, wanatoka makwao wanaenda sehemu kuokota mikate bure kabisa na siku ya sita wanapewa mara mbili, kwa kuwa wanapewa bure wakapewa mtihani siku ya sabato wasitoke kwenda hio sehemu lakini wapo waliotoka kwenda huko (tamaa), pia sharti la ziada la kupewa bure chakula waliambiwa wapashe mikate mapema siku ya sita hakuna sababu ya kuwasha moto wa kupika siku ya sabato sababu mikate ilikuwa haiharibiki wala kunuka lakini wapo waliokaidi.

Sasa tukija kwenye uhalisia wa sasa mtu anajitafutia chakula kabanwa na kazi na chakula anachokula kinaharibika, kuna tatizo gani kupika jumamosi ?
 
Moja ya amri kumi ni kuabudu siku ya sabato, Siku takatifu iliyotengwa na Mungu kuturuhusu KUPUMZIKA kwa kuziweka kando shughuli zetu na tunashukuru kwa kujumuika pamoja kwenye shughuli za kuabudu ikiwa ni ishara ya shukran kisha tunarudi makwetu kupumzika, Kila siku ni siku ya Mungu lakini sio kila siku ni sabato kwasababu si kila siku ya kuacha shughuli zako kupumzika.

Mfumo wa kutambua siku upo tangu zamani lakini hakukuwa na majina ya kisasa ya siku kama jumamosi na jumapili ndio maana huwezi yakuta hayo majina kwenye biblia, Musa alipopewa amri kumi ikiwemo ya siku ya sabato alishaelekezwa siku rasmi ya kuanza kuiabudu Sabato ambayo kwa mfumo wa sasa imeangukia Ijumaa dakika chache kabla jua halijazama mpaka jumamosi lisaa baada ya jua kuzama, kisha baada ya hapo zinahesabiwa upya siku sita na ikifika ya saba inakuwa Sabato.

Hata Yesu aliikuta siku ya Sabato, aliiabudu, aliisifia na kuitetea (Marko 2), miaka nenda rudi hado sasa ukienda Israel wanaendeleza huu utaratibu, siku ya jumamosi maduka hufungwa na shughuli nyinginezo husimama.

Yesu ni Pumziko letu kiroho hata tunapofanya kazi nzito tukiwa hoi taaban lakini siku ya sabato tunaweka kando shughuli hizo tunapumzisha na miili
Ukiona mtu anakazania sabato na kukaza misuli ya shingo na kiuno ujue bado hajui Yesu Kristo alikuja duniani kufanya nini kama Bwana wa Sabato.
 
Hata Yesu aliikuta siku maalum ya sabato, aliiabudu, kuisifia na kuitetea (marko 2) na miaka nenda eudi mpaka leo hii utaratibu ni huo ilikoanzia Israel, ni kipi cha kubadili ?
Hakuna cha kubadili isipokua mnajipa haki sana kwamba Sabato ya kweli ni jumamosi. Ilihali hata wanaosali jumapili nayo ni sabato
 
Kuna baadhi ya Mazingira ni tofauti na agano la kale

Mfano kitabu cha Kutoka wayahudi walipewa mtihani, wanatoka makwao wanaenda sehemu kuokota mikate bure kabisa na siku ya sita wanapewa mara mbili, kwa kuwa wanapewa bure wakapewa mtihani siku ya sabato wasitoke kwenda hio sehemu lakini wapo waliotoka kwenda huko (tamaa), pia sharti la ziada la kupewa bure chakula waliambiwa wapashe mikate mapema siku ya sita hakuna sababu ya kuwasha moto wa kupika siku ya sabato sababu mikate ilikuwa haiharibiki wala kunuka lakini wapo waliokaidi.

Sasa tukija kwenye uhalisia wa sasa mtu anajitafutia chakula kabanwa na kazi na chakula anachokula kinaharibika, kuna tatizo gani kupika jumamosi ?
Kwa hiyo mazingira yanabadili amri ya Mungu?
 
Moja ya amri kumi ni kuabudu siku ya sabato, Siku takatifu iliyotengwa na Mungu kuturuhusu KUPUMZIKA kwa kuziweka kando shughuli zetu na tunashukuru kwa kujumuika pamoja kwenye shughuli za kuabudu ikiwa ni ishara ya shukran kisha tunarudi makwetu kupumzika, Kila siku ni siku ya Mungu lakini sio kila siku ni sabato kwasababu si kila siku ya kuacha shughuli zako KUPUMZIKA.

Mfumo wa kutambua siku upo tangu zamani lakini hakukuwa na majina ya kisasa ya siku kama jumamosi na jumapili ndio maana huwezi yakuta hayo majina kwenye biblia, Musa alipopewa amri kumi ikiwemo ya siku ya sabato alishaelekezwa siku rasmi ya kuanza kuiabudu Sabato ambayo kwa mfumo wa sasa imeangukia Ijumaa dakika chache kabla jua halijazama mpaka jumamosi lisaa baada ya jua kuzama, kisha baada ya hapo zinahesabiwa upya siku sita na ikifika ya saba inakuwa Sabato.

Hata Yesu aliikuta siku ya Sabato, aliiabudu, aliisifia na kuitetea (Marko 2), miaka nenda rudi hado sasa ukienda Israel wanaendeleza huu utaratibu, siku ya jumamosi maduka hufungwa na shughuli nyinginezo husimama.

Yesu ni Pumziko letu kiroho hata tunapofanya kazi nzito tukiwa hoi taaban lakini siku ya sabato tunaweka kando shughuli hizo tunapumzisha na miili
Kuna Ibrahimu baba wa imani, na kuna Musa mleta Torati. Unamfuata yupi kati ya hao wawili?
 
Moja ya amri kumi ni kuabudu siku ya sabato, Siku takatifu iliyotengwa na Mungu kuturuhusu KUPUMZIKA kwa kuziweka kando shughuli zetu na tunashukuru kwa kujumuika pamoja kwenye shughuli za kuabudu ikiwa ni ishara ya shukran kisha tunarudi makwetu kupumzika, Kila siku ni siku ya Mungu lakini sio kila siku ni sabato kwasababu si kila siku ya kuacha shughuli zako KUPUMZIKA.

Mfumo wa kutambua siku upo tangu zamani lakini hakukuwa na majina ya kisasa ya siku kama jumamosi na jumapili ndio maana huwezi yakuta hayo majina kwenye biblia, Musa alipopewa amri kumi ikiwemo ya siku ya sabato alishaelekezwa siku rasmi ya kuanza kuiabudu Sabato ambayo kwa mfumo wa sasa imeangukia Ijumaa dakika chache kabla jua halijazama mpaka jumamosi lisaa baada ya jua kuzama, kisha baada ya hapo zinahesabiwa upya siku sita na ikifika ya saba inakuwa Sabato.

Hata Yesu aliikuta siku ya Sabato, aliiabudu, aliisifia na kuitetea (Marko 2), miaka nenda rudi hado sasa ukienda Israel wanaendeleza huu utaratibu, siku ya jumamosi maduka hufungwa na shughuli nyinginezo husimama.

Yesu ni Pumziko letu kiroho hata tunapofanya kazi nzito tukiwa hoi taaban lakini siku ya sabato tunaweka kando shughuli hizo tunapumzisha na miili
Nionyeshe walipoandika jumamosi
 
Ipo hivyo tangu enzi za Musa, Yesu, mpaka sasa ukienda Israel utaweza kuona maduka siku ya leo hayafunguliwi
Sabato ni Sheria. Lakini unafahamu kuwa Yesu ni mwisho wa Sheria? Aliyemwamini Yesu hayupo chini ya Sheria, anaishi kwa imani. Hao wanaofunga maduka kwa vigezo vya Sabato siku wakimwamini Yesu hawatafanya hivyo tena!
 
Sabato ni siku maalum ya kupumzika na kumuabudu alieiweka
"Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe"
Warumi 14:6

Muhimu siyo siku ya kuabudu bali unayemwabudu. Kama unaabudu katika roho na kweli, siku si tatizo.
 
Kufa kwa Yesu kulikuwa mwisho wa Amri 10 ?

ni ruhusa kuua ?
Ni ruhusa kuiba ?
Ni ruhusa kuabudu miungu mingine?
Ni ruhusa kuzini ?
Aliyemwamini Yesu hahitaji kuambiwa amwamini Mungu kwa kuwa tayari hiyo imani ni sehemu ya maisha yake.

Aliyemwamini Yesu hahitaji kuambiwa asiue kwa kuwa utu wake mpya haumwongozi kutenda mabaya bali mema.

Sheria ni kwa ajili ya watu waliokuwa kiroho. Walio na uzima wa Mungu mioyoni mwao hawawezi kuua, hiyo si asili yao.
 
Kwa hiyo mazingira yanabadili amri ya Mungu?
Wasabato ni wanafiki sana ...kama wangekua wanafuata sheria zote kama za Wayahudi hapo labda tungewaamini. Sheria mojawapo ya Sabato ya Wayahudi ni kutokuwasha moto siku ya Sabato yaani kwa mazingira ya leo hutakiwi kuwasha hata taa za nyumba au kuendesha gari kwenda huko kanisani kwao(manake ili gari liwake lazima "ignition" itokee). Sasa ukiwauliza Wasabato hawana jibu la kueleweka
 
Kila siku ni siku ya Mungu lakini sio kila siku ni sabato kwasababu Huwezi kupumzika kila siku
Sabato walivyokuwa wakiiadhimisha Wayahudi haikuwa halisi, bali ni mfano wa Sabato iliyotarajiwa kuletwa na Yesu Kristo.

Kuna Sabato ya Agano jipya, lakini siyo kama inayofuatwa na waumini wa SDA.

Sabato ya Agano jipya haizingatii siku bali hali ya rohoni. Ni ile hali ya kupata pumziko moyoni kwa sababu ya kuliamini Neno la Mungu.

Wengi wa wanaojiita Wasabato hawana pumziko lolote! Bado wanasumbuliwa na dhambi, hofu, mashaka, magonjwa, wachawi, n.k. Kuna mpaka Wachungaji ambao wanaomhofia kulogwa na waumini wao japo wote ni Wasabato.

Sabato ya Agano jipya ni pale mtu anapoziamini ahadi za Mungu kikamilifu kiasi cha kuongozwa na hizo ahadi. Akifikia hiyo hatua, hatakuwa na hofu yoyote wala hataweza kutishwa na kitu chochote.
 
Huo ni mjadala mwengine kabisa fungulia uzi wake, hapa kinachozungumziwa ni sabato, Siku aliyoitoa Mungu kuturuhusu kupumzika nasi kwa kumshukuru tunajumuika nyumba za ibada kumshukuru kisha kurudi majumbani kupumzika.

Siku, Siku, Siku !!!!
Imeandikwa, "mtawatambua kwa matunda yao"

Kati ya watu wanaoshija Sabato na Wakristo wanaojiamini Neno la MUNGU ni wepi wameweza kuwa na matunda mazuri katika:
1. Kuishi maisha yenye ushuhuda kwa wasioamini

2. Kuwa na uwezo wa kuwasaidia wengine kwa kulitumia Neno la Mungu

3. Kutokuogopa wachawi

4. Kutokuendeshwa na maisha ya dhambi

5. Kuogopwa na mapepo kama Yesu alivyokuwa akiogopwa na mapepo
 
Mwenye amri zake 10 aliempa Musa azilete tuziabudu (akiwemo na Yesu aliezitii)
Yesu ni BWANA wa Sabato, maana yake ni mkubwa kuliko Sabato. Anayemtii mwingine ni mkubwa au mdogo? Au hukusoma jinsi waalimu wa Sheria walivyokuwa wakimkasirikia Yesu kwa kutokuifuata Sabato?
 
Back
Top Bottom