Ni kwanini unajenga nyumba ya ghorofa?

Ni kwanini unajenga nyumba ya ghorofa?

Kwa Wale wanaopenda kupata Mwongozo sahihi Katika ujenzi wa ghorofa karibuni PM. Nitajitahidi ufikie mahitaji yako kwa gharama nafuu zaidi. Mpaka sasa kupitia uzi huu, nimeweza kutoa ushauri watu wengi walionifata PM, kwa ushauri zaidi. Kuna watu wamekuwa kama wamefunguliwa, maana walikuwa wanatishwa saana juu ya ujenzi wa ghorofa. Kupitia uzi huu,kuna mteja mmoja ambaye nimeanza kusimamia mchakato wa awali (Designing stage). Kwa hiyo msisite kunicheki. Nitafanya yafuatayo:-

1. Designing stage
-Architectural drawings
-Structural drawings
-Bills Of Quantities (BOQ)
-Electrical drawings and other services
drawings
- Building permit application and closely
making follow ups
2. Construction stage
-Day to day supervision
-Team building (Artisans/Fundi)
-Procurement/Manunuzi on your choice.
Ukitaka ushughulikie Wewe Manunuzi
yote, poa tu. Au ukinipa Mimi poa tu.

Nakuhakikishia nitayafikia mahitaji yako kwa gharama nafuu kabisa. Namba zangu 0713678173 professionally ni Quantity Surveyor (QS)
 
Ukizeeka unashindwa kupanda ngazi, unaacha kulala juu unarudi floor ya chini. Mwishowe unaona kelele za mjini huziwezi, unakuwa mpweke unarudi kijijini kwenu. Unaenda kuishi na walewale uliokua nao enzi zile za udogo, ambao ulikuwa unawaona washamba, lakin sasaiv unahitaji kampani yao
 
Hivi kweli nna hela zangu unishawishi nijenge nyumba ya chini..si ntakua chizi..
 
Mna umri gani nyie?
Hamna msingi wa ghorofa la makazi wa zaidi ya 20m, avarage ni 15m tena umetumia mkandarasi kabisa. Kama mmeibiwa kwa ujinga uzembe wenu msijaribu kuhalalisha uzembe wenu hapa.
Mkuu wacha utani basi aiseee….. kuna msingi mpaka wa Million Mia..tena residential house kabisa….kila mtu anajenga kadri ya uwezo wake. wengine 20M ni kujenga nyumba ya kuishi wakati wengine ni kununua mabati ya kuzungushia site......
 
Mkuu wacha utani basi aiseee….. kuna msingi mpaka wa Million Mia..tena residential house kabisa….kila mtu anajenga kadri ya uwezo wake. wengine 20M ni kujenga nyumba ya kuishi wakati wengine ni kununua mabati ya kuzungushia site......
Hapo kweli kabisa kila mbuzi a nakula kwa urefu wa kamba yake
 
Mkuu hapana. Na material zingine tunachukua viwandani kabisa. Sishangai wewe kushangaa ama kukataa hizi gharama.

Nakumbuka enzi hizo kulikua na ugomvi wa majirani wawili. Mmoja na ghorofa mwingine hana. Na yule baba mwenye ghorofa ni engeneer. Yule wa chini ni ndugu yetu na ni wachokozi na wakorofi kwelikweli[emoji28] waakawa wanamtukana yile baba na kusema vibaha ghorofa lake. Nyumba ya wale ndugu zangu ni ya chini lakini kali mno. Nikisema kali ninkali. Sasa yule baba kwa hasira mwenye ghorofa akawaambia " sasa mnaongea nini wakati gharama ya nyumba yenu yote ndo msingi wa ghorofa yangu?" Nilishangaa sana watu wakanielekeza bado sikuelewa. Nilaja kufatilia kbs kwa wahusika wa kada hiyo. Na nikaona wanaojenga. Aisee... inafika. Nimeshuhudia kbs. Basi hapa namm najiliwaza nitajenga langu siku tuu[emoji28]

Niliambiwa watu huona gharama ni ndogo sometimes kwasababu wanajenga kwa kujibana sana na kuacha vitu vingine. Kama ulivyoona wataalam wakiainisha huko juu. Kuna mwingine anataka ujenz ule wa kufata protocols na uimara. Mwingine atapambana kwa mkono unapifikia mkuu. Ndo maana hata nyunba za chini tuu pia gharama hutofautiana.
Million 180 inakujengea ghorofa mjini kabisa
 
Kwa gharama za sasa ghorofa ya kawaida hata 100m unajenga.
 
Pemba mnazi, Kimbiji bado bei iko chini na unaweza kupata eneo la kujenga na kupata upepo mwanana wa kutoka baharini...mkuu nitafute nikupe eka kwa milioni sita tu ujimwage na kupata upepo wa baharini
Na mimi naomba namba yako please ya heka moja
 
Back
Top Bottom