Ni kwanini unajenga nyumba ya ghorofa?

Labda huko mwisho wa lami lakini si maeneo yanayofikika kwa urahis, Huwezi kusema umepata kiwanja kwa bei rahisi wakati gari za abiria kukupeleka huko unatembea umbali zaidi ya km50 kutoka town centre.
Siyo singida tu...hata Dar vipo..
 
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
 
Labda huko mwisho wa lami lakini si maeneo yanayofikika kwa urahis, Huwezi kusema umepata kiwanja kwa bei rahisi wakati gari za abiria kukupeleka huko unatembea umbali zaidi ya km50 kutoka town centre.
Mkuu kuna maeneo kabisa unaenda kituo cha daladala kwa mguu dakika 10 na bei pouwa tu. Ingawa mpaka feri ni kilomita 37
 
Ni mtindo wa maisha ambao tumeiga nje. Ni kama hii miaka ya karibuni umezuka mtindo wa kuwa na mgongo mkubwa wa paa.
Wenyewe wanaita "msauzi".

Kila ukipita ni MSAUZI. Wanaigana kama manyumbu!

Mwingine niliona kafumua bati lake akaweka jipya lenye staili ya MSAUZI.
 
Mie nimejenga ghorofa kwa kuwa niliweka nadhiri toka mtoto. Enzi hizo dingi alikuwa anatuchukua krismasi anatupeleka kwenye swimming pool pale Police Officers Mess Oysterbay, sasa nilivyokuwa naona mijengo maeneo ya kule nilijiwekea nadhiri nikipata hela lazima nijenge ghorofa.

Niliweka ki-balcony cha kunywea wine nje ya chumba changu juu toka nihamie sijawahi kukaa hapo zaidi ya kupasafisha tu mavi ya njiwa wa jirani ambao wamepageuza kama kijiwe chao
 
Km 37 kutoka town centre mbali sana hapo ni sawa na mtu atoke arusha mjini akanunue kiwanja kikatiti huko ndani ndani halafu aseme amenunua mjini, Hapo no sawa na kupoteza ela yako sababu hata ukija kutaka kuuza au kutaka uiweke dhamana wale watu wanaofanya valuasheni huwa wanaangalia nyumba kiwanja kiko umbali gani kutoka city centa kwa hio jinsi nyumba kuwanja chako kinavyokua mbali na mji ndivyo unavyojiweka mbali na mafanikio. Nunua kiwanja mjini.
Mkuu kuna maeneo kabisa unaenda kituo cha daladala kwa mguu dakika 10 na bei pouwa tu. Ingawa mpaka feri ni kilomita 37
 
Mkuu una ujumbe gani kwa wanaokaa maeneo kama kibaha au kongowe? Maana ni zaidi ya 40km kutoka city centre
 
Huu ni ubishi ambao sina hakika kama unakusaidia ...nyie ndio wale wa huko mbali siwezi kukaa mimi sio

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
Hallafu wanajikuta mjini hawapawezi na huko mbali hawapawezi maana panapanda bei panawashinda wakati kipindi hapajachangamka walipachukulia poa
 
Ni kukosa hela tu ndo maana mawazo yanakujia hivyo,Ukitoka hapo utamshauri Rais atumie IST,sukari isiweke kwenye chai,mikate ya kazi gni,chipsi zina kazi gani,kwanini Yutong waweke sit za 2×2 badala ya 3×3,yani basi tu
 
Mkuu una ujumbe gani kwa wanaokaa maeneo kama kibaha au kongowe? Maana ni zaidi ya 40km kutoka city centre
Mimi nimeazimia kupandisha Ghorofa mwakani nina eneo kubwa tu Kibaha! kwenye maisha huwa napenda kufanya tofauti na wengine wanavyofanya....kama kujenga Nyumba ya Chini nimeshajenga na wengine wengi wanajenga sana aina hiyo ya Nyumba so lazima kila unapotaka kufanya kitu haipendezi kufanya kitu kile kile nimesoma mawazo ya watu wengi hapa nadhani wanaile Ghorofa ni Ghali asee ukitaka vitu rahisi huku Duniani vitu vikubwa utaishia kuviona kwa wengine tu....ukweli Ghorofa inaheshima yake mtu akiwa na dhamira hakishindikani kitu

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Miye napenda sababu ktk familia woote wamejenga nyumba za chini. Ili niwe tofauti kidogo.
 
Ni sawa na maeneo ya Mwembemkavu sijui kule maeneo ya Tuangoma, mpaka ufike feri dah! Ila ndio kumekucha sasa hivi watu wanaangusha mijengo ya kimsauth kibao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…