Ni kwanini unajenga nyumba ya ghorofa?

Ni kwanini unajenga nyumba ya ghorofa?

Wazungu walijenga nyumba za ghorofa kutokana na uhaba wa ardhi kwao. Nimekutana na Wafrika Magharibi pia mawazo yao ni ya kujenga ma ghorofa. Nikipowauliza sababu waliniambia kwao ardhi ni ghali sana. Kupata kiwanja cha kujenga nyumba inakulazimu uwe na kuanzia milioni 20 kwa pesa ya Tanzania. Wanasema ukijenga ghorofa hukosi mpangaji na wewe unapata na sehemu yako ya kuishi kwa amani.

Wengine wanasema wanajenga ghorofa kuyaona matunda ya mafanikio yake kwa macho. Sasa ninajiuliza sisi ardhi tunayo kubwa sana. Mpaka sasa bei ya kiwanja ni wastaniwa milioni tano mijini. Ni kwanini unawaza kujenga ghorofa kama una wazo hilo au ni kwanini ulijenga ghorofa?

Ardhi milioni tano mijini???😳😳

viwanja vya wapi hivyo na vina ukubwa gani?.
 
Dada cha kushangaza hapa Arusha hakuna kiwanja cha milion 5,labda huko ndani kijijini kabisa.
Kuna jirani yangu hapa anauza miguu kumi kwa kumi na tatu kwa milion kumi na nne. Yan ni balaa
Kuna kakangu naona nar anaishi Arusha ananunuaga mashamba halaf anakata viwanja anauza mil 5. Hatua 20 kwa 20.
Same ways na mbezi shamba same thing same price. Na mitaa naona hadi moshono kbs
 
Gharama za ghorofa na nyumba ya kawaida hazipishani sana hapa nazungumzia nyumba ya ghorofa moja lakini ardhi haiongezeki ila idadi ya watu inaongezeka baada ya miaka 50 inawezekana na sisi tutakuwa huko ni vizuri tukachukua tahadhari mapema
Mkuu hapa umeongopa. Gharama ya msingi wa ghorofa unaijua kweli? Yaan ule msingi ni nyumba kamili na chench inabaki tusiongopeane
 
Kutoka posta hadi hapo ni shi ngapi na na masaa mangapi?
Pia je vile vya kukatiana kwa ya chini kabisa vina range kwenye sh. ngapi
Kama unafanya kazi mitaa ya Posta sikushauri uishi mitaa hii. Ni almost impossible.
Ila kama unataka kuhodhi ardhi, this area has all the trimmings of becoming a very vibrant and independent urban area.

Kwa kijana, ningekushauri ununue ardhi huku. Kuna ujenzi wa factories, sports complexes, Shule na vyuo, hotels na watu wengi wanashusha nyumba za maana huku ingawa ni early stages.

Ni 22 km from ferry/posts na Bei elekezi ni 5,000shs per sqm. Market price ni 10,000 mpaka 20,000 per sqm na karibu kote kuna town plan.
In early 2000s, 3mil ilinipa 35 acres...(Not to be bragging)
 
Mkuu una ujumbe gani kwa wanaokaa maeneo kama kibaha au kongowe? Maana ni zaidi ya 40km kutoka city centre
Yaan kibaha na kongowe imechangamka balaa. Kazini kwetu staff 9 wote wamejenga kibaha na kongowe. Na hawana presha wanagurahia balaa. Mpk nashangaa
 
Kama unafanya kazi mitaa ya Posts sikushauri yoshi mitaa hii. Ni almost impossible.
IlA kama unataka kuhodhi ardhi, this area has all the trimmings of becoming a very vibrant and independent urban area.

Kwa kijana, ningekushauri anunue ardhi huku. Kuna ujenzi wa factories, sports complexes, Shule na vyuo, hotels na watu wengi wanashusha nyumba za maana huku ingawa ni early stages.

Ni 22 km from ferry/posts na Bei elekezi ni 5,000shs per sqm. Market price ni 10,000 mpaka 20,000 per sqm na karibu more kuna town plan.
In early 2000s, 3mil ilinipa 35 acres...
Kwa kibada pakoje mkuu?
 
Kujenga gorofa labda apartment upangishe vinginevyo ni kusababisha ugomvi wakati ukifa na kila mmoja atataka gorofa lako.
Pili unapozeeka una sukari, pressure, moyo,mguu kwishney yaani utatesa tu watu kukubeba.
Jenga nyumba ya chini tu bana.
Kwani si huwa kunajenhwa rooms za juu na chini? Wananchi jamani
 
Kwa watu kadhaa waliokua wanajenga nimeona msingi range 45mil to 55. Na ni hizo hizo room 4 za kulala ukiacha store na vingine. Hapa naenda site ya ndugu yangu katumia 55.
Ebwanaaaaeeeh....umenikata stimu[emoji848]

Ntaweza kujenga ghorofa kweli maana ndo ndoto yangu[emoji848][emoji848]

Hizo 55 katumia kwenye msingi tuu?
 
Nyumba ni Ghorofa ndugu tusidanganyane, ni Umasikini tu unapelekea hayo yote. Angalia Umasikini unavyotesa watu kwenye hiyo vid hapo chini

 
Ebwanaaaaeeeh....umenikata stimu[emoji848]

Ntaweza kujenga ghorofa kweli maana ndo ndoto yangu[emoji848][emoji848]

Hizo 55 katumia kwenye msingi tuu?
Yes. Katumia nondo ile yenyewe. Na wala usiogope gharama. Yaan unaogopa gharama? Aah wapi. Mbona unajenga tu wallah ukiamua. Yaan ukiamua unajenga nakuhakikishia. Kitu ukishakidhamiria mbona unakivunja vunja. Halaf si lazima ujenge kwa mkupuo. Yaan unaweza jenga kwa hatua. Ngoja nije pm
 
Km 37 kutoka town centre mbali sana hapo ni sawa na mtu atoke arusha mjini akanunue kiwanja kikatiti huko ndani ndani halafu aseme amenunua mjini, Hapo no sawa na kupoteza ela yako sababu hata ukija kutaka kuuza au kutaka uiweke dhamana wale watu wanaofanya valuasheni huwa wanaangalia nyumba kiwanja kiko umbali gani kutoka city centa kwa hio jinsi nyumba kuwanja chako kinavyokua mbali na mji ndivyo unavyojiweka mbali na mafanikio. Nunua kiwanja mjini.
Usilinganishe Dar na Arusha ,
 
Back
Top Bottom