Ni kweli mtu akitumia dawa ya UKIMWI hawezi kumuambukiza mwenzake hata bila kutumia kinga?

Ni kweli mtu akitumia dawa ya UKIMWI hawezi kumuambukiza mwenzake hata bila kutumia kinga?

Wataalamu wa afya huko mahospitalini wanasema ili kujiridhisha uko salama ni sharti upime mara 3 ikimaanisha unapima tarehe 1 January 2024, utarudia tena kupima 1 February 2024, utamalizia kupima mara ya tatu 1 March 2024, majibu yakifanana basi hapo upo salama

Ila utashangaa hivi sasa Yohana na Mwajuma wamekutana kwenye Kilimanjaro Express, wameshuka Shekilango wanapitia pharmacy wananunua kipimo wanapima wanasoma -ve wanaelekea Sinza kutest mitambo
Kwa Muongozo upi?
Muongozo halali wa Upimaji Ni kweli utapima at Start then baada ya mwezi mmoja then baada ya miezi mitatu au Mwaka inategemea kama hauko kwenye Hali hatarishi ya kuweza ku be exposed kwenye Maambukizi..

Upimaji wa aina yoyote Unategemea na hali ya client anayeenda kupima na hali ya Kuwa exposed na Maambukizi..

Kwa mfano Unaweza ukaja wewe mama wa nyumbani ukapima kulingana na Miongozo nikakuambia rudi baada ya mwezi kupima na baada ya mwezi nikakumbia utarudi baada ya miezi mitatu..

Hali itakuwa tofauti na yule sex Workers (Anayejiuza) au Anayeishi na Mtu mwenye maambulizi ambaye yeye nitamwambia Arudie kupima kila mwezi kutokana na exposed Status yake..
Hapo sijui umenielewa..

Upimaji wa HIV una algorism yake na mipaka yake sidhani kama kupima kila Mwezi kwa mtu ambaye hayuko Exposed inaruhisiwa..
 
USalama upo Ila hautakiwi kujiona salama kuliko mwingine ikiwa bado unaishi..

Kwa mfano kwenye IPC (Infection Prevention and Control) sasa kwenye rule za Standard precaution Huwa tunajielimisha kila siku Kuwa..
Rule number one ni Consider everyone susceptible to infection and Contagious...
hiyo haijalishi hata mke wako unatakiwa utake precaution...Na ndo maana ukija Hospitali hata kama nakujua Nitavaa Gloves..


Ukiishi kwa kufuata Roles na Miiko nakuhakikishia magonjwa utakuwa unayasikia tu..
hii ya mke na mume imekaaje sasa ?

wanaishi pamoja hlf hakuna anayemwamini mwenzake?

sasa watakuwa wanapima mara kwa mara au?

ghafla bn vuuu unamwinua mamsapu twende kucheki ngoma!??[emoji848][emoji848]
 
hii ya mke na mume imekaaje sasa ?

kama wanaishi pamoja hlf hakuna anayemwamini mwenzake?

watakuwa wanapima mara kwa mara au?

ghafla bn vuuu unamwinua mamsapu twende kucheki ngoma!??[emoji848][emoji848]
Kwni tangu mlipoona weww na mkeo Hamjawahi kwenda tena kupima/hamna desturi ya kupima😳😳🥺🥺🥺..

HIV inaambukizwa kwa njia nyingi sio lazma njia ya ngono..

Haina maana ya kulima mara kwa mara ila desturi ya kupima hata kila baada ya Miezi sita au kila baada ya mwaka..

Kingine Kuishi Pamoja sio.Kigezo.cha Kuaminiana..

Na precaution sio kwenye kufanya Ngono tu..
Kumkinga na Tabia Hatarishi ambazo unajua zinaweza kupelekea mkapata maambukizi..
 
Kiukweli Kuna watu wenye roho ngumu na upendo wa ajabu. Nimeona kisa kimoja kutokea Mbagala. Kuna couple ambayo wakati wakifunga ndoa wote walikuwa negative, then later ikabainika mama kachepuka na kapata UKIMWI.

Yule baba hakumuacha mkewe, mpaka leo wapo wakija kuchukua na kupima wanakuja wote, nimewaona kwa macho yangu na kuwahudumia kwa mikono yangu. Huu mwaka wa 19 bado baba ni negative na tumemfundisha tu namna ya kupractice sexual isiyoleta michubuko.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Kuna level ya viral load (idadi ya virusi vya HIV kwenye damu) ikifikia kuwa undetected (kutoonekana kwenye damu) inakuwa huwezi kumuambukiza mwenza wako hata mkijamiiana bila ya kinga.

Ila inataka ujasiri wa hali ya juu. Yani nikijua una ngoma sidhani hata kama mnara utasoma achilia mbali kupiga kavu.

Kama ni kweli jamaa anakula mzigo kavu basi mwamba jasiri hasa.
Yupo ninae mfahamu wana watoto wawili huko Busokelo Mbeya na mwanamke hajapata maambukizi
 
100% Ni kweli..
Na watu wengi sana wanaishi ni Serodiscordant..
Sisemi Kwa ushabiki bali nimeshuhudia sana..
Watu wengi ambao mara Nyingi tunaruhusu mahusiano hayo ni wale waliopima HVL na mara nyingi Huwa Zinasoma TND..("Target Not Detected")

Huyu ana Percent chini ya 0.01 ya kumuambika mwingine na hata wakinamama wakifika Hapa huwa wanaruhusiwa kuwa na watoto yaani kuchukua mimba na kuzaa..
Watu hawajiulizi kwanini Serostatus (Maambukizi) ya Watu hayaongezeki na yanazidi kupungua?

Kwanini siku hizi Idadi ya watoto Wadogo wenye maambukizi imepungua Sana tofauti na Zamani..

Jibu Ni moja Tu kuwa inawezekana na mifano ninayo na nimeiona si chini ya couple 100 zikiishi hivyo na kwa furaha

Kama kuna mtu mwenye swali namkaribisha maana hii ni moja ya Sehemu zangu za kujidai
Mtu wa hivyo, kwa vile vipimo vyetu ambavyo watu wengi tunajipima akipima itasoma positive au negative
 
Back
Top Bottom