Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,259
- 20,891
Kuna madai ambayo yameshakuwa yakitolewa hapa na watu mbali mbali na pia nje ya hapa kuna madai ya aina hiyo ambayo yamekuwa yakitolewa na watu mbali mbali wakimkosoa Mungu kwamba hana Upendo, japokuwa wanaodai hivyo wamekuwa hawasemi ni wapi wanaupata upendo na ni kwa namna gani wanaweza hata kuupima upendo, lakini wamekuwa wakijenga hoja yao kwenye huo huo upendo kumpimia Mungu, yaani msingi wa hoja yao ni upendo.
Nimekuwa nikiulizwa mara nyingi sana kuhusu jambo hili na baadhi ya jamaa zangu hapa na nje ya hapa ni kwa namna gani nimekuwa nikiona mtazamo wa hawa ndugu kuhusu hoja yao ya uwepo wa uovu na mabaya kwa ujumla wake hapa duniani, nimekuwa nikijibu hili mara nyingi sana na bahati mbaya wengi wamekuwa hawayaoni majibu hayo, nimeona leo nitengeneza makala hii ili niweze kujibu swali hili kwa kirefu zaidi.
Kwanza tunapaswa kujua kwamba Mungu ni mkuu sana na kamwe hatuwezi kumsaidia kwenye chochote kwa sababu anajitosheleza kabisa kwa sababu ni Mungu, tunachokwenda kufanya hapa ni kuwasaidia hawa wenzetu hawa wanaodai Mungu anajipinga kwa kanuni yake mwenyewe ya Upendo ili waweze kuona mantiki kwenye upendo wa Mungu ili waweze kubadilika na kumkubali Mungu, lakini pia pia tunakwenda kuwasaidia wale wanaohangaika kifkra kuhusu hoja za hawa watu waweze kupata majibu na kuondoka kwenye mahangaiko hayo.
Ndugu zetu hawa wamekuwa wakihoji kama Mungu kweli ana upendo iweje dunia iwe kama ilivyo leo kwa maana ya kuumba dunia ambayo mabaya kama vile magonjwa, vita na mengineyo yanawezekana kutokea, wanadai kwamba upendo wa Mungu usingemuelekeza kuumba dunia ambayo yote hayo yanawezekana, kwa kifupi wanadai kwamba kama Mungu angekuwa na upendo unaodaiwa kuwa anao basi angeumba dunia tofauti sana na hii
Jambo hili limekuwa haliingii kabisa akilini au kwa lugha nyingine wamekuwa hawaelewii kabisa Mungu anaedaiwa kuwa ana upendo halafu aumbe dunia ambayo ubaya unawezekana, wao wanaona kwamba haiwezekani Mungu mwenye upendo aumbe dunia kama hii
Tunakwenda kujibu swali hili tukitumia maana rahisi sana ya Upendo ambayo itakwenda kumsaidia kila mmoja kupata ushahidi wa Upendo mkuu wa Mungu bila kutumia falsafa au maneno magumu ambayo yatasababisha watu wengine wa kawaida kutoelewa,lengo la makala hii ni kuwasaidia watu wengi kuelewa kirahisi suala hili na sio kinyume chake,tutatumia pia mifano michache sana ambayo nayo pia ni rahisi sana kueleweka kwa wasomaji wetu
Tukianza kujibu swali hili ni lazima kwanza tuweke wazi maana au fasiri ya Upendo ambayo tutajengea hoja yetu kwenye makala hii ambayo pia tutalijibu swali hilo la hawa ndugu zetu, maana ambayo tutajengea hoja ambayo itakwenda kujibu swali hili linalohusu au lililojengwa kwenye Upendo ni ile hali ya kumpatia mtu kile ambacho anakihitaji au kukitaka ikiwa na maana pia ya kumpatia mtu stahiki yake bila kumlazimisha, nitatoa mifano michache ambayo ni ya kawaida sana ili sote tuelewe hili.
Mfano wa kwanza
Hebu chukulia kwamba unaishi na mtu pale nyumbani halafu akawa anapenda sana kula wali na maharage kila siku na wewe mwenyeji wake una uwezo huo wa kumpatia chakula hicho ambacho anakipenda sana halafu ukamnyima chakula hicho na kumpa chakula kingine, kwa kitendo hicho cha kumyima chakula anachokipenda utakuwa haujampenda bali kinyume chake,kumnyima mtu kile ambacho anakihitaji au kukitaka ni ishara ya kutomjali na kama humjali basi humpendi
Mfano wa pili
Chukulia kwamba mtu anataka kulala bila kula chakula cha usiku kwasababu tu hataki kula na huko kulala bila kula ndicho kitu ambacho anakitaka,na wewe ukamruhusu kufanya hivyo,kwa kumruhusu kufanya kile ambacho anakipenda au kukihitaji, hapa maana yake ni kwamba unampenda kwa sababu umempa kile ambacho anakitaka bila kujali madhara ya anachokitaka kwa sababu ni mtu mzima na anajua madhara ya kutokula.
Kumbukeni kwamba mifano yote hiyo hapo juu inawahusu watu wenye utimamu wa akili na ni watu wazima kiumri
Kwa maana hiyo ya Upendo ni wazi kwamba kwa nionavyo mimi imeweza kabisa kuenea kwenye kanuni nzima ya upendo ambayo sio kulazimisha chochote
Sasa tuanze na hoja ya uwepo wa mabaya au uwezekano wa uwepo wa mabaya kama kunakinzana na Upendo au haukinzani
Kwanza tuangalie chanzo cha huu ubaya chanzo chake ni kipi,
Ubaya ulikuwepo kwasababu kwanza Mungu aliumba dunia ambayo ubaya unawezekana,swali litakalofuata hapa ni "kwanini kama alikuwa ana upendo aumbe dunia ambayo ubaya unawezekana"? Jibu la swali hili tutaweza kulijibu kwa kutazama maana ya upendo kama tulivyoiona hapo juu,kwanza kabla ya kujibu swali hilo tunapaswa tujue ni nini kinamfanya Mungu awe Mungu maana anakuwa Mungu kwasababu ya sifa zake
Moja kati ya sifa zinazomfanya Mungu awe Mungu ni uwezo wake wa kujua yote,kama anauwezo huo ni wazi kwamba wakati anaumba viumbe vyote alijua kuna viumbe ambavyo vitataka hayo mabaya,kitendo cha kutaka Mungu aumbe dunia ambayo mabaya hayawezekani ni kutaka kumfanya huyu Mungu afanye mambo kinyume na upendo kwasababu tumeshaona kwamba upendo maana yake ni kumpatia kile ambacho mtu au yoyote anachokitaka bila kujali matokeo yake kwasababu ukimnyima kwasababu tu unajua matokeo yake ni kwenda kinyume cha kanuni ya upendo ambayo ni kutokulazimishana
Kwa maana hii ni kwamba uwepo wa ubaya huu ambao tunauona leo hapa duniani ni matokeo ya upendo wa huyu Mungu ambae alijua yote tangu mwanzo
Watu fulani wanaweza kudhani kwamba nakufuru kwa kumjengea Mungu uwezekano wa kuonekana nae anapenda mabaya kwasababu yapo kwa ruhusa yake,hili sio kweli kwasababu tunapaswa tujue kwamba Mungu hakutaka mabaya lakini kwasababu viumbe vyake au baadhi ya viumbe vyake viliutaka hakuwa na namna tofauti na kuvipa kile ambacho vilitaka japokuwa ubaya hauna shirika na Mungu kwasababu Mungu ni mtakatifu kwa asilimia zaidi ya 100
Kuna jambo ambalo tunapenda kuliweka wazi hapa,jambo lenyewe ni kwamba,Mungu hakuumba chochote kwaajili yake bali kwaajili ya viumbe vitakavyokuwepo hapa duniani,ukiangalia kwa mfano Oxygen,hewa hii ipo kwasababu kuna viumbe vitaihitaji ili viishi au viwe na uhai,Mungu yupo kabla ya hewa hiyo kuwepo na yupo kabla ya uwepo wa chochote hivyo tunapaswa kuvitenda vitu hivi na Mungu kwenye suala la uwepo na dhumuni lake,kwa maana hiyo hata ubaya upo sio kwasababu ya Mungu bali kwasababu ya wale wanaouhitaji sawasawa na hewa ya oksijeni ambayo nayo madhumuni yake yanafanana na ya ubaya
Kwa maana hiyo ni kwamba Mungu hakuumba ulimwengu huu na vyote vilivyomo kwaajili yake yeye bali kwaajili ya viumbe vyake ikiwemo na logic,hivyo ni vyema tukajua hilo na kulitenga
Baada ya kujua hili ni wazi kama tunaweza kuwa tumeshajibu swali lote kwa ujumla wake kwasababu tatizo kuu la uwepo wa ubaya tumeona ni zao la upendo mkuu wa Mungu wa kumpatia kila mmoja kile ambacho anahitaji,lakini tofauti na hili ni kwamba sifa nyingine ya Mungu ni kuweza kila kitu,tunatarajia kwamba Mungu huyu aumbe dunia ambayo kwa kiwango fulani dunia hiyo iakisi uwezo huo wa huyu Mungu
Tukiangalia dunia hii ni kwamba inaakisi uwezo wa huyu Mungu kwa kiwango fulani ambapo tunaona kwamba kuna uwezekano wa kutokea mabaya na mema na mengine ambayo ni mengi na yanaakisi uwezo wa Mungu wa kuweza yote,kuhoji hili lisitokee kwenye ulimwengi ambao umeumbwa na anaeweza yote ni kutaka kumuwekea limit kitu ambacho sio halali
Pamoja na kujibu swali hili bado huwa kuna swali lingine ambalo watu huuliza na ambalo huwasumbua baadhi ya waamini uwepo wa Mungu na swali hili ni la kumhusu Shetani,Watu wamekuwa wakihoji sababu ya huyu Mungu kumuacha Shetani au kumuumba wakati alijua kabisa kwamba ataasi kwasababu Mungu anajua yote
Swali hili nalo linaangukia kwenye kundi la swali la kwanza kwasababu kuacha kumuumba shetani kwasababu tu Mungu alijua atakuja kuasi ni kutompenda Shetani kwasababu hiyo ni kumnyima kile ambacho alipaswa akipate kwa uhuru wake mwenyewe,kwa maana hiyo basi ni wazi kwamba Mungu kuacha Shetani aendelee kuwepo ni kumpa kile ambacho anakitaka ambacho kwa maana yetu ni kwamba Mungu alimpenda Shetani
Pamoja na hayo watu wanaweza kujiuliza kwamba kama uwepo wa yote hayo ni matokeo ya upendo,je mbona sasa Shetani na wanadamu ambao walipenda mabaya wanakuja kuadhibiwa baadae?
Swali hili nalo linajibika kirahisi sana kwa kutumia maana ya upendo tuliyonayo hapo
Ili kupata jibu la swali hili ni kwamba tunapaswa kujua kwamba mtu anapokosea na ukamuacha bila kumuadhibu unakuwa umemdhulumu,kwa mujibu wa kanuni ya sheria ambayo hata ulimwengu huu unaongozwa nayo ni kwamba ni lazima unapokosea ni haki yako kuadhibiwa,kuachwa na kwenda hivi hivi tu ni kutokutendewa haki na ni kwenda kinyume na upendo pia,yoyote ambae anakosea ni haki yake kupata adhabu hivyo hawa ambao wanatenda mabaya leo ni haki yao kuadhibiwa na huko ndio kwenda sambamba na upendo kwasababu upendo maana yake ni kumpa kila mmoja stahiki yake na sio kudhulumiana,kutokuadhibiwa ni kudhulumiwa
Jibu la swali hili linaweza kusababisha swali kwamba "Mbona huyu Mungu anasema kwamba ukimuomba msamaha anakusamehe"? "Je Mungu huyu si alisema kwamba yeye ni hakimu wa haki na kila kosa ni lazima liadhibiwe,sasa iweje awaache wengine wakati wamekosa hata kama wamemuomba msamaha"? Lakini pia huyu Mungu anawezaje kuwa wa huruma na hapo hapo awe ni hakimu wa haki"?
Hapo kunaweza kuwa na maswali zaidi ya hayo lakini maswali yote yana jibu moja kuu ambalo ni upendo,nitafafanua,kufikia hapa ngoja tu niseme kweli kwamba,ni lazima niingie kwenye msimamo wa Kikristo kwenye kujibu swali hili kwasababu ndio ninauouna una majibu stahiki kwenye mrundikano wa hayo maswali katika msingi wa Upendo
Ni kweli Mungu aliahidi kuiadhibu kila dhambi bila kujali umeomba msamaha au laa na alijua tu kwamba kumsamehe au kusamehe makosa bila kumuadhibu mkosaji na kosa lenyewe kwa ujumla au dhambi ni kwenda kinyume na kanuni ya sheria ambayo inaagiza kila kosa linapaswa kuadhibiwa na Mungu anasema yeye ni hakimu wa haki,je Mungu anaweza kuwa hakimu wa haki halafu akawa na huruma? Jibu la swali hili ni ndio lakini ni Mungu wa kwenye Biblia tu ndio ambae anaweza kuwa hakimu wa haki na hapo hapo kuwa Mungu wa huruma na hili linamthibitisha kuwa ni Mungu kwasababu hakuna kinachomshinda na anaenea kabisa kwenye sifa yake ya kuweza yote
Kimsingi kila binadamu ana makosa kwasababu ya udhaifu wetu wa kibinadamu hivyo kwa maana hii kila mwanadamu ana hatia mbele za Mungu na ni lazima sote tuhukumiwe kwasababu sote tumekosea,lakini je tutapataje kuwa salama? Je ni kwa namna gani? Jibu ni kwa upendo wa Mungu,Je ni kwa namna gani? Jibu lake ni kwa kupitia Yesu Kristo,usijali nitafafanua hili na hapa nitajibu maswali ya wengi sana waliokuwa wanajiuliza kuhusu hili
Kwanza tunapaswa kujua kwamba sheria tunayoizungumza hapa ambayo hatukupaswa kuivunja na ambayo hata Mungu mwenyewe hajaivunja na hata ivunja na muwekaji wa sheria hiyo ni Mungu mwenyewe,sheria hiyo ni ile ya kutokwenda kinyume na upendo na uhalisia,uhalisia ni pamoja na kutokuvuruga mazingira,maana ya upendo na kanuni yake tumeshajifunza huko juu,kwa maana hiyo basi kukosea kwetu kunatupeleka kwenye kuadhibiwa,makosa yote yataadhibiwa kama sheria inavyosema kwamba kila kosa linastahili adhabu
Kwasababu Mungu alimpenda sana Mwanadamu na aliamua kumuumba kwa mfano wake aliamua kutengeneza mpango wa kumfanya mwanadamu huyu aepuke adhabu ambayo hiyo ambayo kwanza aliichagua yeye mwenyewe na pili ni haki yake kuipata kwasababu ambazo tayari tumeshazisema huko juu,kwasababu Mungu anampenda sana mwanadamu alitaka amuepushe mwanadamu huyu na adhabu hiyo
Kwanza Mungu hakutaka kumuumba kiumbe mwingine kwasababu hakutaka kwenda kinyume na mipango yake,hivyo aliamua kumtengenezea mwanadamu huyu mpango wa kumuepusha na adhabu ambayo aliitaka mwenyewe,lakini kwasababu Mungu ni wa upendo hakutaka kumlazimisha mwanadamu huyu kufuata mpando wake [Mungu] kwasababu kufanya hivyo ni kwenda kinyume na upendo,hivyo kukubaliana na mpango wa Mungu ni hiyari na sio lazima kwasababu Mungu anaupendo wa hali ya juu sana
Kwa kupitia maisha yale yale ambayo binadamu aliyachagua Mungu aliamua kutengeneza mpango kwenye maisha hayo hayo kumuokoa mwanadamu na adhabu ya kuikaidi sheria ambayo ni haki yake,lakini je kama akiiepuka adhabu hii Mungu si atakuwa amevunja sheria yake ya kutokumpa haki yake mwanadamu huyu ambayo ni adhabu kwasababu alikosea? Jibu ni hapana na nitaeleza hili
Baada ya kuona kumsamehe mwanadamu bila mwanadamu huyo kulipa au kugharamia makosa yake ni kuvunja kanuni ya sheria,Mungu aliamua kulipa gharama ile yeye mwenyewe kwa kuamua kuadhibiwa kwasababu ya makosa ya mwanadamu huyo.Mungu aliamua kuja duniani na kuadhibiwa bila kosa lolote na hadi kufa na kumfanya mwanadamu huyu kuwa huru
Je kwa Mungu kuadhibiwa,huyu mwanadamu anapaswa afanye nini ili apate msamaha wa adhabu yake? Au inakuwa hivyo tu automatic? Jibu lake ni hapana bali kuna ambacho Mungu anahitaji mwanadamu huyu akifanye kwasababu kumsamehe hivi hivi bila huyu mwanadamu huyo kujua au kuulizwa kama anahitaji msamaha huo basi Mungu anakuwa hajamtendea haki huyu mwanadamu na atakuwa amevunja kanuni ya upendo,kwa maana hiyo Mungu huyu ameweka mpango kwamba kila mwanadamu ambae atataka asiingie kwenye malipo ya makosa yake yote anapaswa kukubali malipo ya dhambi au makosa yake kwa Mungu mwenyewe kuadhibiwa na kufa kwa niaba yake,hii ina maana kwamba wewe na mimi,kama hatutaki kuja kuwajibika sisi kama sisi kwa makosa yetu wenyewe na tuliyoyachagua kwasababu ya uhuru wa kuchagua basi tukubali leo hii kwamba Mungu alitulipia makosa yetu hayo
Tunachopaswa ni kukiri au kukubali bila shuruti kwamba Mungu alitulipia gharama za malipo ya dhambi zetu kwa kupigwa na sisi tutakuwa huru na adhabu inayotungoja kwasababu ya makosa yetu,kama hutaki huna haja ya kukubali bali wewe endelea tu na maisha yako na utakuja kulipa mwenyewe adhabu yako
Kwa maana hii ni kwamba Mungu ameweza kumuondoa mwanadamu kwenye adhabu ya makosa yake mwenyewe kwa kutoadhibiwa lakini kwa kutumia upendo wake mkuu kwa kuamua kuyabeba yote haya yeye mwenyewe,lakini pia amefanya haya bila kuvunja sheria yake mwenyewe kwa kuadhibu kila kosa kama alivyoahidi na sio kuacha tu.Kwahiyo Mungu ameweza kuwa hakimu wa haki na hapo hapo kuwa Mungu mwenye huruma ya ajabu
Unaweza kujiuliza kwamba huyu Mungu alikujaje duniani na kulipa makosa yetu,jibu lake ni kwamba alikuja na kufahamika kama Yesu Kristo,hivyo unapaswa kukubali kuwa Yesu Kristo ni mwokozi wa maisha yako kwa maana ya kufia dhambi zako wewe
Siku ya mwisho wote tutahukumiwa kama wakosaji na kutakiwa kupelekwa kwenye adhabu yetu lakini yule ambae alitufia atatushika mkono na kutuambia njooni kwangu ninyi mliokubali kafara yangu kwa makosa yenu mfurahi pamoja nami milele na tutapona kwenye adhabu hiyo ya milele
Kwahiyo ndugu yangu Mungu wa kwenye Biblia ndie Mungu kwasababu ni Mungu wa Upendo wa kutisha na ni hakiku wa kweli,karibu kwake
Kupitia yote hayo tumeweza kuona ni kwa namna gani Mungu anakuwa ni Mungu wa upendo wote bila kujikinza na Mungu wetu ni Mungu anaeishi kila siku na hata sasa
Karibuni Mkuu wa chuo , Wickama , Ishmael , Ntuzu , christine ibrahim , Kaunga na wengine wote kwenye mjadala huu ili tukosoane na kujifunza pamoja
Nawakutakia tafakuri njema na mbarikiwa nyote ......!!
Nimekuwa nikiulizwa mara nyingi sana kuhusu jambo hili na baadhi ya jamaa zangu hapa na nje ya hapa ni kwa namna gani nimekuwa nikiona mtazamo wa hawa ndugu kuhusu hoja yao ya uwepo wa uovu na mabaya kwa ujumla wake hapa duniani, nimekuwa nikijibu hili mara nyingi sana na bahati mbaya wengi wamekuwa hawayaoni majibu hayo, nimeona leo nitengeneza makala hii ili niweze kujibu swali hili kwa kirefu zaidi.
Kwanza tunapaswa kujua kwamba Mungu ni mkuu sana na kamwe hatuwezi kumsaidia kwenye chochote kwa sababu anajitosheleza kabisa kwa sababu ni Mungu, tunachokwenda kufanya hapa ni kuwasaidia hawa wenzetu hawa wanaodai Mungu anajipinga kwa kanuni yake mwenyewe ya Upendo ili waweze kuona mantiki kwenye upendo wa Mungu ili waweze kubadilika na kumkubali Mungu, lakini pia pia tunakwenda kuwasaidia wale wanaohangaika kifkra kuhusu hoja za hawa watu waweze kupata majibu na kuondoka kwenye mahangaiko hayo.
Ndugu zetu hawa wamekuwa wakihoji kama Mungu kweli ana upendo iweje dunia iwe kama ilivyo leo kwa maana ya kuumba dunia ambayo mabaya kama vile magonjwa, vita na mengineyo yanawezekana kutokea, wanadai kwamba upendo wa Mungu usingemuelekeza kuumba dunia ambayo yote hayo yanawezekana, kwa kifupi wanadai kwamba kama Mungu angekuwa na upendo unaodaiwa kuwa anao basi angeumba dunia tofauti sana na hii
Jambo hili limekuwa haliingii kabisa akilini au kwa lugha nyingine wamekuwa hawaelewii kabisa Mungu anaedaiwa kuwa ana upendo halafu aumbe dunia ambayo ubaya unawezekana, wao wanaona kwamba haiwezekani Mungu mwenye upendo aumbe dunia kama hii
Tunakwenda kujibu swali hili tukitumia maana rahisi sana ya Upendo ambayo itakwenda kumsaidia kila mmoja kupata ushahidi wa Upendo mkuu wa Mungu bila kutumia falsafa au maneno magumu ambayo yatasababisha watu wengine wa kawaida kutoelewa,lengo la makala hii ni kuwasaidia watu wengi kuelewa kirahisi suala hili na sio kinyume chake,tutatumia pia mifano michache sana ambayo nayo pia ni rahisi sana kueleweka kwa wasomaji wetu
Tukianza kujibu swali hili ni lazima kwanza tuweke wazi maana au fasiri ya Upendo ambayo tutajengea hoja yetu kwenye makala hii ambayo pia tutalijibu swali hilo la hawa ndugu zetu, maana ambayo tutajengea hoja ambayo itakwenda kujibu swali hili linalohusu au lililojengwa kwenye Upendo ni ile hali ya kumpatia mtu kile ambacho anakihitaji au kukitaka ikiwa na maana pia ya kumpatia mtu stahiki yake bila kumlazimisha, nitatoa mifano michache ambayo ni ya kawaida sana ili sote tuelewe hili.
Mfano wa kwanza
Hebu chukulia kwamba unaishi na mtu pale nyumbani halafu akawa anapenda sana kula wali na maharage kila siku na wewe mwenyeji wake una uwezo huo wa kumpatia chakula hicho ambacho anakipenda sana halafu ukamnyima chakula hicho na kumpa chakula kingine, kwa kitendo hicho cha kumyima chakula anachokipenda utakuwa haujampenda bali kinyume chake,kumnyima mtu kile ambacho anakihitaji au kukitaka ni ishara ya kutomjali na kama humjali basi humpendi
Mfano wa pili
Chukulia kwamba mtu anataka kulala bila kula chakula cha usiku kwasababu tu hataki kula na huko kulala bila kula ndicho kitu ambacho anakitaka,na wewe ukamruhusu kufanya hivyo,kwa kumruhusu kufanya kile ambacho anakipenda au kukihitaji, hapa maana yake ni kwamba unampenda kwa sababu umempa kile ambacho anakitaka bila kujali madhara ya anachokitaka kwa sababu ni mtu mzima na anajua madhara ya kutokula.
Kumbukeni kwamba mifano yote hiyo hapo juu inawahusu watu wenye utimamu wa akili na ni watu wazima kiumri
Kwa maana hiyo ya Upendo ni wazi kwamba kwa nionavyo mimi imeweza kabisa kuenea kwenye kanuni nzima ya upendo ambayo sio kulazimisha chochote
Sasa tuanze na hoja ya uwepo wa mabaya au uwezekano wa uwepo wa mabaya kama kunakinzana na Upendo au haukinzani
Kwanza tuangalie chanzo cha huu ubaya chanzo chake ni kipi,
Ubaya ulikuwepo kwasababu kwanza Mungu aliumba dunia ambayo ubaya unawezekana,swali litakalofuata hapa ni "kwanini kama alikuwa ana upendo aumbe dunia ambayo ubaya unawezekana"? Jibu la swali hili tutaweza kulijibu kwa kutazama maana ya upendo kama tulivyoiona hapo juu,kwanza kabla ya kujibu swali hilo tunapaswa tujue ni nini kinamfanya Mungu awe Mungu maana anakuwa Mungu kwasababu ya sifa zake
Moja kati ya sifa zinazomfanya Mungu awe Mungu ni uwezo wake wa kujua yote,kama anauwezo huo ni wazi kwamba wakati anaumba viumbe vyote alijua kuna viumbe ambavyo vitataka hayo mabaya,kitendo cha kutaka Mungu aumbe dunia ambayo mabaya hayawezekani ni kutaka kumfanya huyu Mungu afanye mambo kinyume na upendo kwasababu tumeshaona kwamba upendo maana yake ni kumpatia kile ambacho mtu au yoyote anachokitaka bila kujali matokeo yake kwasababu ukimnyima kwasababu tu unajua matokeo yake ni kwenda kinyume cha kanuni ya upendo ambayo ni kutokulazimishana
Kwa maana hii ni kwamba uwepo wa ubaya huu ambao tunauona leo hapa duniani ni matokeo ya upendo wa huyu Mungu ambae alijua yote tangu mwanzo
Watu fulani wanaweza kudhani kwamba nakufuru kwa kumjengea Mungu uwezekano wa kuonekana nae anapenda mabaya kwasababu yapo kwa ruhusa yake,hili sio kweli kwasababu tunapaswa tujue kwamba Mungu hakutaka mabaya lakini kwasababu viumbe vyake au baadhi ya viumbe vyake viliutaka hakuwa na namna tofauti na kuvipa kile ambacho vilitaka japokuwa ubaya hauna shirika na Mungu kwasababu Mungu ni mtakatifu kwa asilimia zaidi ya 100
Kuna jambo ambalo tunapenda kuliweka wazi hapa,jambo lenyewe ni kwamba,Mungu hakuumba chochote kwaajili yake bali kwaajili ya viumbe vitakavyokuwepo hapa duniani,ukiangalia kwa mfano Oxygen,hewa hii ipo kwasababu kuna viumbe vitaihitaji ili viishi au viwe na uhai,Mungu yupo kabla ya hewa hiyo kuwepo na yupo kabla ya uwepo wa chochote hivyo tunapaswa kuvitenda vitu hivi na Mungu kwenye suala la uwepo na dhumuni lake,kwa maana hiyo hata ubaya upo sio kwasababu ya Mungu bali kwasababu ya wale wanaouhitaji sawasawa na hewa ya oksijeni ambayo nayo madhumuni yake yanafanana na ya ubaya
Kwa maana hiyo ni kwamba Mungu hakuumba ulimwengu huu na vyote vilivyomo kwaajili yake yeye bali kwaajili ya viumbe vyake ikiwemo na logic,hivyo ni vyema tukajua hilo na kulitenga
Baada ya kujua hili ni wazi kama tunaweza kuwa tumeshajibu swali lote kwa ujumla wake kwasababu tatizo kuu la uwepo wa ubaya tumeona ni zao la upendo mkuu wa Mungu wa kumpatia kila mmoja kile ambacho anahitaji,lakini tofauti na hili ni kwamba sifa nyingine ya Mungu ni kuweza kila kitu,tunatarajia kwamba Mungu huyu aumbe dunia ambayo kwa kiwango fulani dunia hiyo iakisi uwezo huo wa huyu Mungu
Tukiangalia dunia hii ni kwamba inaakisi uwezo wa huyu Mungu kwa kiwango fulani ambapo tunaona kwamba kuna uwezekano wa kutokea mabaya na mema na mengine ambayo ni mengi na yanaakisi uwezo wa Mungu wa kuweza yote,kuhoji hili lisitokee kwenye ulimwengi ambao umeumbwa na anaeweza yote ni kutaka kumuwekea limit kitu ambacho sio halali
Pamoja na kujibu swali hili bado huwa kuna swali lingine ambalo watu huuliza na ambalo huwasumbua baadhi ya waamini uwepo wa Mungu na swali hili ni la kumhusu Shetani,Watu wamekuwa wakihoji sababu ya huyu Mungu kumuacha Shetani au kumuumba wakati alijua kabisa kwamba ataasi kwasababu Mungu anajua yote
Swali hili nalo linaangukia kwenye kundi la swali la kwanza kwasababu kuacha kumuumba shetani kwasababu tu Mungu alijua atakuja kuasi ni kutompenda Shetani kwasababu hiyo ni kumnyima kile ambacho alipaswa akipate kwa uhuru wake mwenyewe,kwa maana hiyo basi ni wazi kwamba Mungu kuacha Shetani aendelee kuwepo ni kumpa kile ambacho anakitaka ambacho kwa maana yetu ni kwamba Mungu alimpenda Shetani
Pamoja na hayo watu wanaweza kujiuliza kwamba kama uwepo wa yote hayo ni matokeo ya upendo,je mbona sasa Shetani na wanadamu ambao walipenda mabaya wanakuja kuadhibiwa baadae?
Swali hili nalo linajibika kirahisi sana kwa kutumia maana ya upendo tuliyonayo hapo
Ili kupata jibu la swali hili ni kwamba tunapaswa kujua kwamba mtu anapokosea na ukamuacha bila kumuadhibu unakuwa umemdhulumu,kwa mujibu wa kanuni ya sheria ambayo hata ulimwengu huu unaongozwa nayo ni kwamba ni lazima unapokosea ni haki yako kuadhibiwa,kuachwa na kwenda hivi hivi tu ni kutokutendewa haki na ni kwenda kinyume na upendo pia,yoyote ambae anakosea ni haki yake kupata adhabu hivyo hawa ambao wanatenda mabaya leo ni haki yao kuadhibiwa na huko ndio kwenda sambamba na upendo kwasababu upendo maana yake ni kumpa kila mmoja stahiki yake na sio kudhulumiana,kutokuadhibiwa ni kudhulumiwa
Jibu la swali hili linaweza kusababisha swali kwamba "Mbona huyu Mungu anasema kwamba ukimuomba msamaha anakusamehe"? "Je Mungu huyu si alisema kwamba yeye ni hakimu wa haki na kila kosa ni lazima liadhibiwe,sasa iweje awaache wengine wakati wamekosa hata kama wamemuomba msamaha"? Lakini pia huyu Mungu anawezaje kuwa wa huruma na hapo hapo awe ni hakimu wa haki"?
Hapo kunaweza kuwa na maswali zaidi ya hayo lakini maswali yote yana jibu moja kuu ambalo ni upendo,nitafafanua,kufikia hapa ngoja tu niseme kweli kwamba,ni lazima niingie kwenye msimamo wa Kikristo kwenye kujibu swali hili kwasababu ndio ninauouna una majibu stahiki kwenye mrundikano wa hayo maswali katika msingi wa Upendo
Ni kweli Mungu aliahidi kuiadhibu kila dhambi bila kujali umeomba msamaha au laa na alijua tu kwamba kumsamehe au kusamehe makosa bila kumuadhibu mkosaji na kosa lenyewe kwa ujumla au dhambi ni kwenda kinyume na kanuni ya sheria ambayo inaagiza kila kosa linapaswa kuadhibiwa na Mungu anasema yeye ni hakimu wa haki,je Mungu anaweza kuwa hakimu wa haki halafu akawa na huruma? Jibu la swali hili ni ndio lakini ni Mungu wa kwenye Biblia tu ndio ambae anaweza kuwa hakimu wa haki na hapo hapo kuwa Mungu wa huruma na hili linamthibitisha kuwa ni Mungu kwasababu hakuna kinachomshinda na anaenea kabisa kwenye sifa yake ya kuweza yote
Kimsingi kila binadamu ana makosa kwasababu ya udhaifu wetu wa kibinadamu hivyo kwa maana hii kila mwanadamu ana hatia mbele za Mungu na ni lazima sote tuhukumiwe kwasababu sote tumekosea,lakini je tutapataje kuwa salama? Je ni kwa namna gani? Jibu ni kwa upendo wa Mungu,Je ni kwa namna gani? Jibu lake ni kwa kupitia Yesu Kristo,usijali nitafafanua hili na hapa nitajibu maswali ya wengi sana waliokuwa wanajiuliza kuhusu hili
Kwanza tunapaswa kujua kwamba sheria tunayoizungumza hapa ambayo hatukupaswa kuivunja na ambayo hata Mungu mwenyewe hajaivunja na hata ivunja na muwekaji wa sheria hiyo ni Mungu mwenyewe,sheria hiyo ni ile ya kutokwenda kinyume na upendo na uhalisia,uhalisia ni pamoja na kutokuvuruga mazingira,maana ya upendo na kanuni yake tumeshajifunza huko juu,kwa maana hiyo basi kukosea kwetu kunatupeleka kwenye kuadhibiwa,makosa yote yataadhibiwa kama sheria inavyosema kwamba kila kosa linastahili adhabu
Kwasababu Mungu alimpenda sana Mwanadamu na aliamua kumuumba kwa mfano wake aliamua kutengeneza mpango wa kumfanya mwanadamu huyu aepuke adhabu ambayo hiyo ambayo kwanza aliichagua yeye mwenyewe na pili ni haki yake kuipata kwasababu ambazo tayari tumeshazisema huko juu,kwasababu Mungu anampenda sana mwanadamu alitaka amuepushe mwanadamu huyu na adhabu hiyo
Kwanza Mungu hakutaka kumuumba kiumbe mwingine kwasababu hakutaka kwenda kinyume na mipango yake,hivyo aliamua kumtengenezea mwanadamu huyu mpango wa kumuepusha na adhabu ambayo aliitaka mwenyewe,lakini kwasababu Mungu ni wa upendo hakutaka kumlazimisha mwanadamu huyu kufuata mpando wake [Mungu] kwasababu kufanya hivyo ni kwenda kinyume na upendo,hivyo kukubaliana na mpango wa Mungu ni hiyari na sio lazima kwasababu Mungu anaupendo wa hali ya juu sana
Kwa kupitia maisha yale yale ambayo binadamu aliyachagua Mungu aliamua kutengeneza mpango kwenye maisha hayo hayo kumuokoa mwanadamu na adhabu ya kuikaidi sheria ambayo ni haki yake,lakini je kama akiiepuka adhabu hii Mungu si atakuwa amevunja sheria yake ya kutokumpa haki yake mwanadamu huyu ambayo ni adhabu kwasababu alikosea? Jibu ni hapana na nitaeleza hili
Baada ya kuona kumsamehe mwanadamu bila mwanadamu huyo kulipa au kugharamia makosa yake ni kuvunja kanuni ya sheria,Mungu aliamua kulipa gharama ile yeye mwenyewe kwa kuamua kuadhibiwa kwasababu ya makosa ya mwanadamu huyo.Mungu aliamua kuja duniani na kuadhibiwa bila kosa lolote na hadi kufa na kumfanya mwanadamu huyu kuwa huru
Je kwa Mungu kuadhibiwa,huyu mwanadamu anapaswa afanye nini ili apate msamaha wa adhabu yake? Au inakuwa hivyo tu automatic? Jibu lake ni hapana bali kuna ambacho Mungu anahitaji mwanadamu huyu akifanye kwasababu kumsamehe hivi hivi bila huyu mwanadamu huyo kujua au kuulizwa kama anahitaji msamaha huo basi Mungu anakuwa hajamtendea haki huyu mwanadamu na atakuwa amevunja kanuni ya upendo,kwa maana hiyo Mungu huyu ameweka mpango kwamba kila mwanadamu ambae atataka asiingie kwenye malipo ya makosa yake yote anapaswa kukubali malipo ya dhambi au makosa yake kwa Mungu mwenyewe kuadhibiwa na kufa kwa niaba yake,hii ina maana kwamba wewe na mimi,kama hatutaki kuja kuwajibika sisi kama sisi kwa makosa yetu wenyewe na tuliyoyachagua kwasababu ya uhuru wa kuchagua basi tukubali leo hii kwamba Mungu alitulipia makosa yetu hayo
Tunachopaswa ni kukiri au kukubali bila shuruti kwamba Mungu alitulipia gharama za malipo ya dhambi zetu kwa kupigwa na sisi tutakuwa huru na adhabu inayotungoja kwasababu ya makosa yetu,kama hutaki huna haja ya kukubali bali wewe endelea tu na maisha yako na utakuja kulipa mwenyewe adhabu yako
Kwa maana hii ni kwamba Mungu ameweza kumuondoa mwanadamu kwenye adhabu ya makosa yake mwenyewe kwa kutoadhibiwa lakini kwa kutumia upendo wake mkuu kwa kuamua kuyabeba yote haya yeye mwenyewe,lakini pia amefanya haya bila kuvunja sheria yake mwenyewe kwa kuadhibu kila kosa kama alivyoahidi na sio kuacha tu.Kwahiyo Mungu ameweza kuwa hakimu wa haki na hapo hapo kuwa Mungu mwenye huruma ya ajabu
Unaweza kujiuliza kwamba huyu Mungu alikujaje duniani na kulipa makosa yetu,jibu lake ni kwamba alikuja na kufahamika kama Yesu Kristo,hivyo unapaswa kukubali kuwa Yesu Kristo ni mwokozi wa maisha yako kwa maana ya kufia dhambi zako wewe
Siku ya mwisho wote tutahukumiwa kama wakosaji na kutakiwa kupelekwa kwenye adhabu yetu lakini yule ambae alitufia atatushika mkono na kutuambia njooni kwangu ninyi mliokubali kafara yangu kwa makosa yenu mfurahi pamoja nami milele na tutapona kwenye adhabu hiyo ya milele
Kwahiyo ndugu yangu Mungu wa kwenye Biblia ndie Mungu kwasababu ni Mungu wa Upendo wa kutisha na ni hakiku wa kweli,karibu kwake
Kupitia yote hayo tumeweza kuona ni kwa namna gani Mungu anakuwa ni Mungu wa upendo wote bila kujikinza na Mungu wetu ni Mungu anaeishi kila siku na hata sasa
Karibuni Mkuu wa chuo , Wickama , Ishmael , Ntuzu , christine ibrahim , Kaunga na wengine wote kwenye mjadala huu ili tukosoane na kujifunza pamoja
Nawakutakia tafakuri njema na mbarikiwa nyote ......!!