Ni Mkatoliki 100% ila hizi ni sababu zangu za kwanini Sihudhurii na Sitohudhuria Jumuiya za kila Jumamosi....

Ni Mkatoliki 100% ila hizi ni sababu zangu za kwanini Sihudhurii na Sitohudhuria Jumuiya za kila Jumamosi....

Kama ungekua una akili japo chembe usingeweza kubeza umuhimu wa ibada za jumuia ndogondogo.

Watu wanasema tu ila mimi nimeshuhudia mtu akizikwa na serikali ya mtaa. Hata walokole hawakujihusha nae.
Asikuambie mtu inauma sana kuona ndugu yako anazikwa kama mzoga wa mbwa aliyegongwa barabarani
Hana ndugu huyo mtu? Unatetea ujinga tu
 
Tatizo linakuja pale ambapo Mtu haendi Jumuiya, haendi Kanisani, hatoi michango yoyote ila akipatwa na shida anataka Kanisa limsaidie, nenda Jumuiya kwa ajili ya kusali kama kuna mambo mengine yanakukwaza achana nayo hayo ni mambo ya wanadamu na hakuna aliyemkamilifu.
Wapi Mungu amesema mtu huyo atengwe? Mnajigeuz watoa hukumu sio?
 
1. Jumuiya kumekuwa ni sehemu za Majungu.

2. Jumuiya imekuwa ni sehemu za Kuchunguzana Kimaisha.

3. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Masutano.

4. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Wanaume Kutongoza na Wanawake kutafuta wa Kuwachapa Nao ( Kuwabandua )

5. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Kutishana kuwa kama hauhudhurii basi Ukifa ( Ukifariki ) Kanisa Katoliki halitokuombea ukiwa Jenezani Kwako.

6. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya kila Siku kuja na Michango isiyo na Kichwa wala Miguu.

7. Jumuiya imekuwa ni Gulio Kuu la kila aina ya Unafiki unaoujua na usioujua hapa duniani.

Halafu Wewe Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina wa Jumuiya yangu hivi mnavyonitishia kuwa kama nisipohudhuria Jumuiya Nikifa hamtoniombea mmeshazungumza na Baba Mungu na akawaambieni kuwa ataanza Kunitanguliza Mimi Kaburini kabla yenu? Wapuuzi wakubwa nyie.

Je, mnavyong'ang'ania Kutoniombea GENTAMYCINE pale Nikifa je, ile Siku ninazaliwa mlikuja Agha Khan Hospital mbele ya Sister Brendah na Sister Aghata waliohakikisha Nazaliwa vyema na salama Kuniombea? Wapuuzi wakubwa nyie.

Na nani aliyewadanganyeni kuwa Imani ya Ukatoliki inapimwa kwa Kuja Kwake ( Kuhudhuria ) katika Jumuiya za Kikatoliki kila Jumamosi kama ya hii leo?

Nilichoamua tu na najua hata Mwenyezi Mungu ananibariki nacho ni kwamba nitajitahidi Kuhudhuria Ibada zote za kila Jumapili ( hasa Misa yangu pendwa ya Kwanza ) na kutoa Sadaka na Michango ya Kikanisa kama tu nitakuwa Nimebarikiwa na Uchumi kwa wakati huo na kama sina najua hata Mola / Maulana nae atajua na hatonichukia au kuwa na Usununu ( Kinyongo ) nami.

Nawatakieni nyote Jumuiya njema!!!!
Nakubaliana na wewe💯
 
Unaweza kuwa na point, ila uko totally wrong kwa kuyaleta huku badala uwapelekee wahusika, (M/Kiti wa Jumuiya ) ama paroko wako kabisa.
Pili, Kanisa Katoliki haliwezi kubadili utaratibu wake eti sababu ya mtu au watu wachache wazembe na wavivu na ma cowards kushindwa kuhudhuria jumuiyani na hivyo kutafuta visababu uchwara ambavyo vinaweza kupatikana popote kwenye kikundi cha watu.
Tatu, wewe ni coward na Popoma mkubwa [emoji1787][emoji852][emoji4]
Wewe ni mwenyekiti au Mwekahazina mla michango?
 
Kama ungekua una akili japo chembe usingeweza kubeza umuhimu wa ibada za jumuia ndogondogo.

Watu wanasema tu ila mimi nimeshuhudia mtu akizikwa na serikali ya mtaa. Hata walokole hawakujihusha nae.
Asikuambie mtu inauma sana kuona ndugu yako anazikwa kama mzoga wa mbwa aliyegongwa barabarani
Hamnaga fahari kwenye kuzikwa hayo mengine mmejiwekea tu kichwani mwenu
 
Michango ya jumuiya makosa mi naona ni ya kanisa.
Maana huko ndo inakotokea... ila kusema kweli michango inachosha.
Mi binafsi siendi jumuiya uvivu wakuamka saa 12, ukichanganya na majungu , ukienda unatwishwa majukumu mazito! Hujadaiwa mchango daaah!!!
Naishia tu kanisani maana kule hamna hata atakae kukaba
Na hapo ni misa ya 2 maana ya kwanza unakutana na kwanzia mwenyekiti wa jumuiya,katibu sijui nani wa WAWATA mara sijui VIWAWA
EEH
 
kiufupi jumuiya zimeanzishwa ili kuongeza kipato cha sadaka mkamuliwe juma pili kanisani alaff jumamosi au juma tano mnakamuliwa tena mkikutana alaf kero ni pale wanataka kusalia ndani kwako mm nawakaribisha nje tu.
nakumbuka kuna siku kulikua na hali ya mvua nkaandaa vitu kwenye garden wakaja mm nkaingia ndani ghafla mvua ikaanza nkajifungia kimya ilipokata na muda umesogea nkatoka nkawaambia kwa leo mambo yashaharibika wakataka kusalia ndani nakawagomea kwanza ndan kwangu hakuna nafasi bas kile kitu wakaenda sema hadi kwa mchungaji na ndo mwanzo na mwisho kwenda jumuiya wakija kwangu sifungui asubuh wanakuta kimyaaaaaaaaaa tena jumamos ndo kabisaaa naamka saa tano
 
Gentamicin Sisi wengine unaotuelezea hayo ya Jumuia Yako hayatuhusu.Wengine sio Wakatoliki.Ushahuri wangu,mambo hayo ni Bora ukayapeleke kwenye Kigango au Parokiani Kwa ufumbuzi hapa hutopata suruhisho na unatuchanganya tusiokuwa Wakatoliki wenzako.
 
Kama nawewe nimkatoliki naumeona mazingira kama hayo umechukua hatuagani, umezungumzia hilojambo kwenye Jumuiya? amaunalileta huku nawewe uonekane umeandika.
Taratibu zakufuata ukiona jambo kama hilo umezifuata?
Kama umewaeleza wanajumuiya wenzako ama viongozi wajumuiya wakapuuza je, ulienda kumueleza paroko katika parokia yenu kwamba kuna muhitaji katika Jumuiya yenu ambae kwa ngazi ya Jumuiya hamnauwezo wa kumsaidia?.
Na ndo maana nimeandika hapa pia. Am not a Catholic lakini ni Mkristo. Kuandika hapa haimaanishi sitaki mabadiliko lakini huu ni mjadala ambao tunaufanya ili ubadilishe fikra zetu. Kama kuna jambo tunakosea ndo tuandike hapa ikiwa ni platform nzuri ya kufikiwa na watu wengi. Kuna atakaesoma hapa na akaona aanzishe au alete mawazo ya kubadilika katika jumuiya yake. Na kuna atakaeona ni upuuzi na akaacha. It all begins with you. Sio every time tunatakiwa kureact negatively...be blessed. And get a lemon too.
 
Haya yoote umesema ukweli mkuu wala haujadanganya chochote, anaepinga na apinge ila ukweli umewafikia
Yaan ni ukweli na nusu mkuu yote haya nmeyaona, Jumuiya ilikua zamani miaka ya nyuma kulikua hakuna hizi habari za mamichango ya ajabu ajabu tulikua tunafurahia jumuiya lakini siku hizi jumuiya zimekua chungu mno michango haiishi

Yaan jumuiya kuna makaunta buku ya mamichango ya kila aina mpaka una data michango mfululizo tena sio kwamba ni michango ya hiari useme km nnayo ntatoa sina siwezi kutoa bali ni lazima uchangie na unakumbushwa deni kila jumuiya kwamba una deni
Elewa miaka ya nyuma kanisa lilikuwa almost fully supported na wazungu sasa mambo yamebadilika mambo yote yanayofanyika lazima pesa itoke kwa waumini.
Kwa hiyo kama hutaki kuchangia mambo ya kanisa unataka nani atoe pesa zake kwa ajili yako?
Nakushauri nenda Mombasa kuna maisha ya bure bure hakuna atakaye kuuliza wewe kutoa pesa yako kamwe.
 
1. Jumuiya kumekuwa ni sehemu za Majungu.

2. Jumuiya imekuwa ni sehemu za Kuchunguzana Kimaisha.

3. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Masutano.

4. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Wanaume Kutongoza na Wanawake kutafuta wa Kuwachapa Nao ( Kuwabandua )

5. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya Kutishana kuwa kama hauhudhurii basi Ukifa ( Ukifariki ) Kanisa Katoliki halitokuombea ukiwa Jenezani Kwako.

6. Jumuiya imekuwa ni sehemu ya kila Siku kuja na Michango isiyo na Kichwa wala Miguu.

7. Jumuiya imekuwa ni Gulio Kuu la kila aina ya Unafiki unaoujua na usioujua hapa duniani.

Halafu Wewe Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina wa Jumuiya yangu hivi mnavyonitishia kuwa kama nisipohudhuria Jumuiya Nikifa hamtoniombea mmeshazungumza na Baba Mungu na akawaambieni kuwa ataanza Kunitanguliza Mimi Kaburini kabla yenu? Wapuuzi wakubwa nyie.

Je, mnavyong'ang'ania Kutoniombea GENTAMYCINE pale Nikifa je, ile Siku ninazaliwa mlikuja Agha Khan Hospital mbele ya Sister Brendah na Sister Aghata waliohakikisha Nazaliwa vyema na salama Kuniombea? Wapuuzi wakubwa nyie.

Na nani aliyewadanganyeni kuwa Imani ya Ukatoliki inapimwa kwa Kuja Kwake ( Kuhudhuria ) katika Jumuiya za Kikatoliki kila Jumamosi kama ya hii leo?

Nilichoamua tu na najua hata Mwenyezi Mungu ananibariki nacho ni kwamba nitajitahidi Kuhudhuria Ibada zote za kila Jumapili ( hasa Misa yangu pendwa ya Kwanza ) na kutoa Sadaka na Michango ya Kikanisa kama tu nitakuwa Nimebarikiwa na Uchumi kwa wakati huo na kama sina najua hata Mola / Maulana nae atajua na hatonichukia au kuwa na Usununu ( Kinyongo ) nami.

Nawatakieni nyote Jumuiya njema!!!!

Hiyo ni juu yako mwenyewe.Kuchagua kunyoa au kusuka .Halafu hawajakulazimishi, na wala wewe ukiacha si kwamba jumuiya zitakufa.
 
Ujawai kosa sabb ila muda mwingi unautumia kusisaka Papuchi [emoji3][emoji3][emoji3]
 
kiufupi jumuiya zimeanzishwa ili kuongeza kipato cha sadaka mkamuliwe juma pili kanisani alaff jumamosi au juma tano mnakamuliwa tena mkikutana alaf kero ni pale wanataka kusalia ndani kwako mm nawakaribisha nje tu.
nakumbuka kuna siku kulikua na hali ya mvua nkaandaa vitu kwenye garden wakaja mm nkaingia ndani ghafla mvua ikaanza nkajifungia kimya ilipokata na muda umesogea nkatoka nkawaambia kwa leo mambo yashaharibika wakataka kusalia ndani nakawagomea kwanza ndan kwangu hakuna nafasi bas kile kitu wakaenda sema hadi kwa mchungaji na ndo mwanzo na mwisho kwenda jumuiya wakija kwangu sifungui asubuh wanakuta kimyaaaaaaaaaa tena jumamos ndo kabisaaa naamka saa tano
Bahati nzuri Kanisa Katoliki lina Mapadre tu. Hao Wachungaji wanapatikana KKKT, Anglikana, nk.
 
Back
Top Bottom