Ni mkoa gani mzuri kwa kuanzia maisha from Zero?

Ni mkoa gani mzuri kwa kuanzia maisha from Zero?

Elias K

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2021
Posts
213
Reaction score
607
Wakuu habari za muda huu!

Baada ya kukaa nyumbani muda mrefu nikifanya kilimo cha kutegemea mvua, mwaka huu kilimo kimeniangusha sana na hata miaka iliyopita mara zote mavuno yalikuwa tofauti na matarajio hivyo nimeamua kuachana na kilimo kwani sioni hatima ya maisha yangu ikiwa tofauti na ya sasa. Unakuta mwaka wenye unafuu katika mavuno napata 160,000 nikiuza ( jasho la mwaka mzima ndiyo hilo).

Nimewaza nikaamua niende mjini nikajitume huwenda mambo yakawa nafuu baadaye.

Naomba ushauri wa mkoa mzuri wa kuanzia maisha from Zero. nina mtaji wa 200,000 na ni tofauti na nauli endapo nitapata uelekeo wa kwenda.

Pia naomba mchanganuo kwa mtaji huu naweza kufanya biashara gani japo sina uzoefu wa kufanya biashara yeyote au kwa mwenye kazi za kutumia nguvu naomba anipe. Tafadhali naombeni Msaada kwa hili na ahsanteni.
 
Mimi nakushauri njoo dar.
Mimi nimekuja mjini hapa na nauli tu, nimeshuka pale kwenye treni sina hata mia mbovu mfukoni,
Mbaya zaidi sikuwa na mwenyeji wa kunipokea au sehemu ya kufikia.
Ila kwa sasa nimepanga chumba changu fresh maisha yanaenda.
 
Mimi nakushauri njoo dar.
Mimi nimekuja mjini hapa na nauli tu, nimeshuka pale kwenye treni sina hata mia mbovu mfukoni,
Mbaya zaidi sikuwa na mwenyeji wa kunipokea au sehemu ya kufikia.
Ila kwa sasa nimepanga chumba changu fresh maisha yanaenda.
Room za kaeaida( za hustlers) shingapi?! Na kwa mtaji huo naweza kudaka fursa gani?!
 
Mimi nakushauri njoo dar.
Mimi nimekuja mjini hapa na nauli tu, nimeshuka pale kwenye treni sina hata mia mbovu mfukoni,
Mbaya zaidi sikuwa na mwenyeji wa kunipokea au sehemu ya kufikia.
Ila kwa sasa nimepanga chumba changu fresh maisha yanaenda.
Dagaa mchele
 
Chumba mimi nimepanga nalipa kodi 20000 kwa mwezi.
Vyumba vipo kuanzia 15000 +
Anayesema eti maoni yangu ni "dagaa mchele" hajui kitu.
Wakati nafika mjini Nilipewa kazi ya kuhudumia kitimoto (napenda sana).
Kurunzi
 
Chumba mimi nimepanga nalipa kodi 20000 kwa mwezi.
Vyumba vipo kuanzia 15000 +
Anayesema eti maoni yangu ni "dagaa mchele" hajui kitu.
Mkuu, Dar kuna chumba cha bei hiyo? Mbona nilisikia maisha ni ghali sana huko?!
 
Shukrani. Room za kaeaida( za hustlers) shingapi?! Na kwa mtaji huo naweza kudaka fursa gani?!
Room30-40 fursa zipo nyingii kuuza matunda&mbogamboga, kuchukua mchele&chenga kyela&mbarali na kuuza town, kuna mishe za kuchoma viazi,nyama,kuna mishe za kuuza mitumba mwanjelwa kuna mishe za kulima mahindi&mpunga.
 
Mimi nakushauri njoo dar.
Mimi nimekuja mjini hapa na nauli tu, nimeshuka pale kwenye treni sina hata mia mbovu mfukoni,
Mbaya zaidi sikuwa na mwenyeji wa kunipokea au sehemu ya kufikia.
Ila kwa sasa nimepanga chumba changu fresh maisha yanaenda.
Nakumbuka uzi wako mi nilikuwa najua ni jokes tu za kujaza server za JF kumbe ilikuwa kweli big up sana
 
Back
Top Bottom