Ni mkoa gani mzuri kwa kuanzia maisha from Zero?

Ni mkoa gani mzuri kwa kuanzia maisha from Zero?

Mimi nakushauri njoo dar.
Mimi nimekuja mjini hapa na nauli tu, nimeshuka pale kwenye treni sina hata mia mbovu mfukoni,
Mbaya zaidi sikuwa na mwenyeji wa kunipokea au sehemu ya kufikia.
Ila kwa sasa nimepanga chumba changu fresh maisha yanaenda.
Nakukubali sana mwanangu...😜
 
tukutane kesho saa mbili asb kwa mkuu wa wilaya nilishanunua pete miaka miwili iliyopita we njoo na suti tu
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 Wacha niende Karume kesho kulokota Esuti kwa Disii itakuwa keshokutwa sasa
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 Wacha niende Karume kesho kulokota Esuti kwa Disii itakuwa keshokutwa sasa
Mkuu kesho kutwa mbali sana unaweza kubadilisha mawazo nitumie vipimo vyako naenda Kwa fundi sasa hivi
 
mwezi ulopita nilikuwa mkoani Iringa , nilipita maeneo mengi ya mjini na baadhi ya vijiji wilayani kilolo nikaanza kushawishika kuishi huko kutokana na mandhari na fursa tofauti tofauti zilizopo , kwanza kabisa ukifika maeneo ya iringa mjini utaona kuwa kuna hakuna wafanya biashara wengi kama ilivyo mikoa mingine ,pili hata wafanya biashara walokuwepo maeneo tofauti tofauti wanafanya biashara zinazofanana

Niliona baadhi ya mitaa ambyo ni maarufu ikiwa na watu wengi wakitembea kutafuta mahitaji maeneo yao.nilianza kushawishika zaidi kufanya biashaa ya mavazi ,chakula na vinywaji kwa baadhi ya maeneo lakini pia niliona Iringa panafaa sana kwa mtu anaetafutamaisha au yule anaweanza kujitegemea .maana bei za nyumba za kupangani rahisi,bei za vyakula ni rahisi bei za mavazi zipo juu kidogo tofauti na dsm .

Binafsi nitarudi tena iringa nikiwa kama raia wa huko nikijishughulisha na biashara ndogo ndogo au hata biashara kubwa pia maana ukifika maeneo ya ilula unakaribishwa na matenga ya nyanya yakiuzwa kwa bei rahisi mno lakini cha ajabu ukiwa mjini nyanya unazipata soko kuu tu na wala huoni watu wakiuza bidhaa hiyo barabarani kama dsm ,ukifika mtela bwawani utakutana na wateja na wauzaji wa samaki wakitoa bwawani hapo wakisafirisha toka iringa kwenda mikoa mingine hapa tz,imani yangu ni kwamba ukiwa kwenye CHAIN VALUE ya hii biasharaya samaki hata ukiwa na tsh 50000 unatoboa , na pia ukipita barabara ya Iringa Dodoma utaona maeneo mengi na vijiji tofaiti tofauti lakini huwezi ona mtu auze soda ,maji au hata leso japo kuna maeneo mabasi na malori yanasimama kwa muda mrefu

nakushauri utembeehuko uone kama kutakufaa au jaribu kwenda mkoa mwingine na wa nyumbani kwako
Iringa mjini maisha ni ghali kuliko dar
Amini usiamini

Afu hakuna fursa hapo labda ufanye biashara inayolenga wateja wanachuo coz kuna vyuo vingi sana

Ila vyuo vikifungwa iringa ni kama lindi tuu dadek
 
Nenda Mbeya kaishi Simike, Sokomatola au Ghana kwa wajane.

Kama ni Moshi kaishi Njoro.

Kama ni Dar Tandika, Vingunguti au Buguruni.

Iringa kaishi Kitanzini, Makorongoni. Frelimo au Kihodombi.

HIZO SEHEMU HATA VYUMBA VYA ELFU 7,10 AU 15 UNAPATA.
 
Sasa masta hapo, inabid uzungushe vitu mkononi, manake ununue vitu kwa wachina/ wahindi uzungushe... otherwise kutobos ni kipande sana kwa hiyo capital mzee...
Sasa usijeuliza ni vitu gani...
Mkoa unaweza chagua
1.Dar..japo mahitaji si mengi kivile
2.Tabora
3.Singida..vijijini... kama manyoni nk unaweza pambana

Kila la kher
 
Nakumbuka uzi wako mi nilikuwa najua ni jokes tu za kujaza server za JF kumbe ilikuwa kweli big up sana
Ile haikuwa Jokes hata kidogo mkuu.
watu wengi walijua mimi ni tapeli.
ila wachache walijitosa kunisaidia bila hata kunijua nitokako hasa.
walinisaidia freshi tu mpaka leo nalisukuma gurudumu la mihangaiko.
 
Back
Top Bottom