Ni movie gani umewahi kuangalia ikakutoa machozi?

Ni movie gani umewahi kuangalia ikakutoa machozi?

Nawasalimu kwa Jina la jamiiforums, stori ziendelee.

wana JF napenda sana muvi za hisia zile mtu unatazama hadi unatoka machozi.

Tunaomba kwa yeyote anaezifahamu muvi za kutoa machozi aweke hapa jina la muvi tukazitafute.
TSOTSI
 
Remember your Mother (Nigerian)

Hii kaa na leso mkononi buda,, hii hata uwe na roho ya chuma ijapokuwa ulizaliwa na mwanamke utalia tu,, upende usipende
Hii movie nakumbuka enzi tunaiangalia ilikua n mkanda wa VHS tena tukikodisha.

Uncle hapendi tuazime Mikanda ya watu,hiyo siku akakuta tunaangalia nae akakaa chini,toka mwanzo hadi mwishoni

ilifika mahali sebuleni wote kimya kila mtu anavuta makamasi kimya kimya asisikike analia, Tunaemuogopa uncle yakamshinda machozi yakawa yanamtoka akainuka akaondoka nnje tukawa tunamskia analia LIVE LIVE.

Aunt akaondoka na njia yake kulia anapojua,tuliobaki tukaondoka usiku ule hatukufanya maombi ya usiku kila mtu alipita na njia yake ni kama Vile Movie ilienda tonesha kidonda cha kila mtu.

Kwa uncle nadhani ni sababu MAMA yake (bibi) alikua kafariki so nikaelewa movie ilimkumbusha mama ake.

ila ile Movie kama unaiangalia mara ya kwanza na Una Moyo,chozi lazima Umwage yani no discusion REMEMBER YOUR MOTHER story inagusa bwana.
 
Huu mzigo hata Batista anatoa mchozi

Humko_Tumse_Pyaar_Hai.jpg
 
Hii movie nakumbuka enzi tunaiangalia ilikua n mkanda wa VHS tena tukikodisha.

Uncle hapendi tuazime Mikanda ya watu,hiyo siku akakuta tunaangalia nae akakaa chini,toka mwanzo hadi mwishoni

ilifika mahali sebuleni wote kimya kila mtu anavuta makamasi kimya kimya asisikike analia, Tunaemuogopa uncle yakamshinda machozi yakawa yanamtoka akainuka akaondoka nnje tukawa tunamskia analia LIVE LIVE.

Aunt akaondoka na njia yake kulia anapojua,tuliobaki tukaondoka usiku ule hatukufanya maombi ya usiku kila mtu alipita na njia yake ni kama Vile Movie ilienda tonesha kidonda cha kila mtu.

Kwa uncle nadhani ni sababu MAMA yake (bibi) alikua kafariki so nikaelewa movie ilimkumbusha mama ake.

ila ile Movie kama unaiangalia mara ya kwanza na Una Moyo,chozi lazima Umwage yani no discusion REMEMBER YOUR MOTHER story inagusa bwana.
Kuna muvi na music 🎶🎵 (vitamin music) hizi hutupa kumbukumbu nzuriii na mbaya......

Remember your mother ni Moja ya muvi nzuriii nzuriii zaki naijeria kuwai kutokea....

Kuna hii muvi ya 20%% FURAHA IPO WAPI for sure nili wai kuiangalia mara Moja ila sijawai tamani kuiangalia tena May be sabb wakati naitazama nilikua Too emotional 🥺
Hasa hasa lile tukio la mama neema kumwachia mtoto wa siku Moja plus zile hustle alizo pitia 20%%

Hii muvi inagusa sana na imepangiliwa sanaaa yaan alaf ni very touching story
 
Back
Top Bottom