Ni muda wa kanisa katoliki kuongozwa na waafrika wanaoongoza kwa waumini na imani kuliko wazungu wanaozidi kutoamini Mungu

Yaani yeye ndo katengeneza mfumo mzima, mtu akiwa shoga ina maana yeye karuhusu, sasa kama ni kitu kibaya kwanini aruhusu kimpate mtu?

Mnasingiza nguvu za giza, Mungu si ndiye aliyeruhusu uwepo wa hizo nguvu? kila kitu ni kwasababu yake.
Hakuna ushahidi wowote wa kisayansi unaoonesha ushoga hutokana na maumbile,ni utashi tu wa mtu Kama kuvuta sigara na kunywa pombe,sisi waislam QUR'AN inasema 'na tumekufanyieni njia mbili,imma mfuate njia ya kushukuru au ya kukufuru'..hapo Kuna utashi wa mtu,tumepewa utashi lakini tumehadharishwa na mustakabalu/matokeo yake
 
Nimecheka had machozi, ila ndo ukweli wenyewee
 
Kila kinachotokea duniani kimeruhusiwa na huyo Mungu. Ndo muweza wa yote
 
Hongera mkuu wa kushtukia utapeli wa Dini.
Saivi nikiamua kutoa sadaka naenda Kwa wasio jiweza. Mwaka Jana nili mnunulia mama mmoja vitenge wao wanaita java pair 3 na Hela 20k yule mama alito machozi huwezi amini alilia sana akisema Mungu hajanijalia mtoto lkn Leo hii amenipa mtoto huyu alishukuru sana. Nilikuwa na pikipiki nikamuaga akasema chukua kuku yoyote bandani humo ukale na wajukuu zangu ...kwangu ukawa mtihani mwingine nikakataa akachukua jogoo kubwa sana nikapewa kutokana na maneno Yale kuongea Kwa sauti ya juu mama mmoja akawa amekuja akaniambia chukua Wala usikatae. Nikachukua!

Baada ya siku kama mbili akaenda kuwashuru wazazi wangu Tena japo nilkuwa sijawaambia nao kawashukuru huku analia. Baada ya mavuno kaniitia karanga debe2 Tena.

Hivo sadaka zangu nawapa watu ambao naona huyu ni mhitaji na hata hospital Huwa naenda sema ndo Nina awamu2 naenda hospital nimejifunza huko ukienda uende umefungasha hasa at least Kwa mwaka mara1 hivi
 
Dini hizi zishakuwa za kipumbavu sana Unakuta mtu ana elimu yake kabisa halafu anapelekeshwa na Dini oneni Sasa zinakotupeleka. Inatia hasira sana yaani siku zote umeenda kanisan na pengine umefunga kula na kunywa mifungi kazaa unakuja sikia kiongozi wako wa dini anabariki watu wanaotatuliana marinda!! Inahuzunisha sana ni matusi makubwa sana kwangu na familia yangu
 
sasa si unaona, yaani Mungu anakasirishwa na kitu alichoruhusu mwenyewe, labda kama anafanya hivyo makusudi ili apate watu wa kuchoma milele....
Huyo mungu atakuwa Ana roho mbaya Sana, matatizo atengeneze mwenyewe alafu anakuja kuhukumu viumbe wake Kwa kufanya

makosa,ambayo yeye(mungu) kawawekea (Kawa tegeshea) makusudi ili wakosee Tu, awapeleke motoni .

Huyu mungu ni mkatili Sana, halafu pia Hana Kazi ya kufanya
 
Mimi naona ni muda muafaka, waumini wa kweli wa kikatoliki, wenye imani na Mwenyezi Mungu mmoja warudi kwenye Uislam.

Wakatoliki wengi wenye imani ya kweli wanarudi kwenye Uislam kwa kukimbia mafundisho ya kupotosha yanayoingizwa kwenye Kanisa Katoliki. Jionee:

Your browser is not able to display this video.
 
Si Wakatoliki, Waanglikana, Wasabato, Walutheri wala Waislam watakubali kuwa na kiongozi Mwafrika hata siku moja, it will never happen. Ni ujinga wetu tu sisi Waafrika kufuata dini za watu ambazo hazina umuhimu wowote maishani mwetu sie Waafrika.
 
Uislam si dini ya maana, wacha kujidanganya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…