Kwa muda mrefu sasa,Rais Jakaya Kikwete amekuwa akitahadharisha kuhusu kuwapo kwa mgawanyiko wa kidini huko nyumbani.Aliongea hayo wakati wa kampeni zake na amerejea tena katika hotuba yake ya uzinduzi wa Bunge.
Tuweke kando mjadala wa namna Kikwete na CCM walivyoshinda uchaguzi mkuu uliopita hivi majuzi.Tuijadili hoja yake ya udini.Hivi kama amepata ushindi halali,anaposema kuna mgawanyiko wa udini anamaanisha kura zote alipigiwa na Waislamu wenzake au?Maana kama kweli kuna mgawanyiko wa udini basi ni dhahiri kuwa matokeo ya uchaguzi huo yasingempa ushindi wa zaidi ya asilimia 60 ( tuki-neglect uchakachuaji).
Let's call a spade a spade.Hivi leo Kikwete anathubutu kulalamika kuhusu tatizo lisilokuwepo la udini ilhali yeye na wanamtandao wenzake walimwaga sumu kubwa ya udini mwaka 2005 to an extent "akawaingiza mkenge" Waislam wenzie kwa kuwaahidi Mahakama ya kadhi na kuahidi kushughulikia uanachama wa OIC?
Na hata tukiweka hilo kando,hivi ile kauli ya "CHAGUO LA MUNGU" haikutokana na jitihada za Kikwete na wanamtandao wenzie kuwaghilibu viongozi wa dini hadi wakamtangaza kuwa amechaguliwa na Mungu kuwakomboa Watanzania?Actually,huo haukuwa udini per se bali kufuru kwa Mwenyezi Mungu.Na kwa sie tunaofahamu kuwa Mungu si Athumani,na hapendi kuchezewa,ipo siku atawaadhibu wale wote waliotumia jina lake kwa minajili ya kusaka kura.
Mie nilikuwa Tanzania mwaka from Oktoba 2005 hadi April 2006 kwenye fieldwork yangu.Mungu huyohuyo tuliyeambiwa Kikwete ndio Chaguo lake mwaka 2005 anihukumu iwapo sentensi ifuatayo ni ya uzushi.Miongoni mwa maustaadhi niliowaintavyuu kwenye fieldwork yangu walibainisha waziwazi kuwa waliahidiwa na Kikwete na timu yake kuwa laiti angepata urais angeshughulikia vilio mbalimbali vya Waislam.Kwangu,huo sio udini as such kwa vile kuna matatizo ya msingi yanayowakabili Waislam na ambayo awamu mbalimbali za serikali tangu uhuru zimekwepa kuyashughulikia.Eneo moja la msingi ni elimu.Mwalimu Nyerere alikiri katika hotuba yake ya tarehe 9/12/1962 kwamba " wengi wa waliofanikiwa kupata elimu walifanya hivyo kupitia shule za misheni,na hivyo wengi ni Wakristo.Hapa tena,kwahiyo,tuna mgawanyiko ambao uwepo wake unaweza kuwa tishio kwa umoja wetu".Akaendelea kusema, " marafiki zangu,kila mmoja wetu afanye jitihada za kujenga Tanganyika ambayo hakutakuwa na tofauti na migawanyiko".Japo wakati Nyerere anastaafu mwaka 1985 alidai kuwa amefanikiwa kutimiza azma hiyo,ushahidi wa kitaaluma unapingana na kauli hiyo.
Kwahiyo,binafsi kama Mtanzania ninayependa kuona nchi yetu ikiwa na jamii yenye usawa,naamini kuwa viongozi wetu wana jukumu la kulishughulikia suala hili na kulipatia ufumbuzi.Kumekuwa na unafiki mkubwa katika kushughulikia malalamiko ya msingi ya Waislamu.Lakini kwa vile lengo la makala hii sio kuzungumzia suala hilo,nachoweza kuandika kwa kifupi ni kuwa kwa namna moja ua nyingine awamu zote nne za urais zimezembea kuyapatia ufumbuzi malalamiko ya Waislam huku Awamu ya Nne ikiingia madarakani kwa kujitambulisha waziwazi na kwa siri kuwa sio tu inayatambua matatizo na malalamiko ya Waislam lakini pia imedhamiria kuyatatua.Na katika kuonyesha iko serious,ahadi ya Mahakama ya Kadhi ikaingizwa kwenye manifesto ya uchaguzi ya CCM mwaka 2005.
Waislam wanajua,na sie tusio Waislam pia tunajua,kwamba ahadi hiyo ilikuwa ni danganya toto tu.Miaka mitano baadaye,suala la Mahakama ya Kadhi na kujiunga limeendelea kuwa ngonjera kama ilivyo kwa "maisha bora kwa kila Mtanzania".
Kwahiyo,Kikwete aliingia madarakani kwa kutumia udini lakini sio kwa vile yeye ni Muislam bali alitambua kilio cha Waislam kisha akakitumia kama turufu yake (kwa ahadi kuwa angeshughulikia matatizo yake) kisha baada ya kupata madaraka akajifanya hahusiki na suala hilo (refer kauli ya Kikwete kuwa aliyeanzisha hoja ya Kadhi ni Agustino Mrema-anaedansi nae hapo chini.What a cheap excuse!).Kwa lugha nyepesi,kilichojitokeza ni utapeli kwa kutumia matatizo ya kidini.
Kikwete analalamika kuhusu udini wakati kwa miaka mitano iliyopita Tanzania imekuwa na Rais na Makamu wa Rais Waislam.Na kwa vile Makamu wa sasa nae ni Muislam,inamaanisha kuwa kwa miaka 10 Tanzania itakuwa imekuwa chini ya Rais na Makamu wa Rais Waislam.Hakuna anayelalamika kwa vile wengi wetu tuna upeo mkubwa zaidi ya wa Kikwete anayetaka kulazimisha kuwa tuna mgawanyiko wa kidini.Ishu ya Rais na Makamu wake kutoka dini moja ni muhimu kwa vile Rais asipokuwepo nchini urais unakaimiwa na Makamu wake.Na likitokea lolote la kutokea,Makamu huyo atakuwa Rais kwa muda.
Sasa huyu Mkwere anapotuambia kuna mgawanyiko wa udini anaashiria kitu gani?Wakristo hawajalalamika muundo wa uongozi wa juu wa CCM ambapo idadi ya Waislam ni kubwa kuliko ya Wakristo (rejea wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM).Kikwete hakuwahi kuekemea jitihada zilizokuwa zikifanywa na magazeti ya Kiislam kujenga picha kuwa Dkt Wilbroad Slaa ni mgombea alietumwa na Kanisa Katoliki.Kikwete hakukemea pale Daily News na Habari Leo,magazeti yanayoendeshwa kwa fedha za walipa kodi,yalifuata mkumbo wa magazeti hayo ya Kiislam kumtambulisha Dkt Slaa kama mgombea aliyetumwa na Kanisa.Hakukemea kwa vile nafsini mwake alikuwa na imani potofu kama hiyo ya wababaishaji hao kuwa Dkt Slaa ana ajenda ya Ukristo.
Tatizo ni kwamba Katiba yetu haitoi fursa ya kumkalia kooni Kikwete.Tatizo jingine ni kukosekana kwa ujasiri huko nyumbani wa kumkalia kooni Kikwete kisheria kwa tuhuma za kuhatarisha usalama wa taifa.Laiti Idara ya Usalama wa Taifa ingekuwa serious basi ni wazi wangemshauri Kikwete aache kuhatarisha usalama wa taifa kwa kauli zake zisizoambatana na uthibitisho kuwa kuna mgawanyiko wa kidini.Au inawezekana wanausalama wetu ndio wanamhadaa Kikwete kuwa kuna mgawanyiko wa udini?
Au inawezekana kuna tatizo kubwa zaidi kuhusu Kikwete,kwamba anaona vitu ambayo sie wengine hatuvioni?Je ni maono ya Sheikh Yahya?Au je kelele hizo za mgawanyiko wa kidini ni maandalizi ya kuihujumu Chadema,au pengine kumuibulia kesi Dkt Slaa kwa kigezo cha kucbochea vurugu za kidini?
Jamani,hata mwezi haujapita na tayari tunashuhudia mazingaombwe tusiyohitaji.Mara TAKUKURU wanamsafisha Chenge.Mara Kikwete anaendeleza ngonjera za mgawanyiko wa udini,mara Kikwete anamchagua Zakia Meghji kuwa mbunge licha ya mwanamama huyo kuhusishwa na suala la EPA ( na taarifa kuwa ana uhusiano wa kifamilia na Kikwete).
Tuspokuwa makini,2010-2015 itashuhudia miujiza ambayo haijawahi kutokea mahala popote duniani katika ulingo wa uongozi na siasa.Sad news is,sie kama wahanga tunaweza tusipate wasaa wa "kushangaa" na kujiuliza "what the hell is going on?"
KULIKONI UGHAIBUNI: Udini Anaozungumzia Kikwete ni Upi?